Kujikumbusha Kusanyiko La Pekee La Siku Moja
Habari hii itatumiwa kwenye programu ya Mkutano wa Utumishi muda mfupi kabla na baada ya kutaniko kuhudhuria kusanyiko la pekee la siku moja katika mwaka wa utumishi wa 2006. Mwangalizi msimamizi atafanya mpango ili maulizo hayo yazungumziwe kimbele na yatumiwe baadaye kwa kujikumbusha, kama ilivyoonyeshwa katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Agosti 2004, ukurasa wa 4. Wakati wa kujikumbusha huko, maulizo yote yachunguzwe, mkikazia jinsi tunavyoweza kutumia katika maisha habari iliyotolewa.
KIPINDI CHA ASUBUHI
1. Inamaanisha nini mtu kudumisha jicho lake likiwa rahisi, na kwa nini hilo ni jambo gumu leo? (Kutokana na habari “Kwa Nini Kudumisha Jicho Lako Likiwa Rahisi?”)
2. Tunafaidikaje kwa Kudumisha Jicho Rahisi? (Kutokana na habari “Vuna Baraka kwa Kudumisha Jicho Likiwa Rahisi”)
3. Ni hatari gani inayotokana na shughuli (au kazi) zinazoweza kuonekana kuwa za kawaida? (Kutokana na habari “Kudumisha Jicho Rahisi Katika Ulimwengu Mwovu”)
KIPINDI CHA KISHA MCHANA-KATI
4. Wazazi na watu wengine wanawezaje kutia moyo vijana wafuatilie miradi ya kiroho? (Kutokana na habari “Wazazi Wanaolenga Mishale Yao Sawasawa” na “Vijana Wanaojitahidi Kufikia Miradi ya Kiroho”)
5. Tunawezaje kutembea tukiwa wenye kusonga mbele pamoja na tengenezo la Yehova (a) tukiwa mtu mmoja mmoja? (b) tukiwa familia? (c) tukiwa kutaniko? (Kutokana na habari “Tazama Mbele Kadiri Unavyotembea Pamoja na Tengenezo la Yehova”)