Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Mei 15
“Je, unafikiri kwamba tutaona wakati wowote ulimwengu usio na umaskini? [Acha mtu ajibu.] Ona lile ambalo Mungu anaahidi. [Soma Isaya 65:21.] Toleo hili la Mnara wa Mlinzi linazungumzia jinsi ahadi hiyo itakavyokuwa jambo halisi.” Fanya mpango wa kurudi ili kuzungumza ulizo: Badiliko hilo lililoahidiwa litatimizwa wakati gani?
Amkeni! Mei 22
“Watu wengi zaidi wamesikia kwamba mazoezi ya kimwili ni ya maana kwa ajili ya afya nzuri, lakini wengi wanakubali kwamba hawafanyi mazoezi ya kimwili vya kutosha. Sivyo? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia faida za mazoezi ya kimwili ya kawaida na linapendekeza njia mbalimbali ambazo katika hizo tunaweza kufanya mazoezi yawe na nafasi katika maisha zetu zenye shughuli nyingi.”
Mnara wa Mlinzi Juni 1
“Ingawa karibu kila mtu anazungumzia amani, muungano wa ulimwengu umewaponyoka wanadamu. Je, unafikiri kwamba kutimiza jambo hilo ni ndoto tu? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linavuta uangalifu kwenye serikali ambayo ina uwezo wa kuunganisha ulimwengu.” Soma Zaburi 72:7, 8, na ufanye mpango wa kurudi ili kuzungumzia jinsi hilo litakavyofanyika.
Amkeni! Juni 8
“Je, umetambua kwamba watu wengi wana wasiwasi kuhusu kuenea kwa magonjwa ya kansa ya ngozi? [Acha mtu ajibu.] Toleo hili la Amkeni! linazungumzia kwa nini leo sisi tunaweza kuwa katika hatari kubwa zaidi na kile tunachoweza kufanya ili kujilinda wenyewe.” Malizia kwa kushiriki pamoja na msikilizaji ahadi yenye kufariji inayopatikana katika andiko la Ayubu 33:25.