Programu Mpya ya Mkusanyiko wa Mzunguko
Katika siku hizi za mwisho za ulimwengu huu wa kale wenye kuchafuka, ni jambo la maana kulinda mavazi yetu ya kiroho na utambulisho wetu wa Kikristo. (Ufu. 16:15) Kwa hiyo, ni jambo lenye kufaa kwamba kichwa cha programu ya mkusanyiko wa mzunguko katika mwaka wa utumishi wa 2006 kiwe “Mjivike Utu Mpya.”—Kol. 3:10.
Siku ya Kwanza ya Mkusanyiko: Hotuba-mfululizo ya kwanza yenye kichwa, “Kuonyesha Sehemu Mbalimbali za Utu Mpya,” itakazia jinsi kusitawisha utu mpya kunavyotuletea faida katika kila sehemu ya maisha zetu. Tunasitawishaje utu mpya? Hilo litachunguzwa katika hotuba mbili za mwisho za siku ya kwanza ya mkusanyiko, “Ujitie Nidhamu Ili Kutafakari Inavyofaa” na “Elimu Inayotokeza Utu Mpya.”
Siku ya Pili ya Mkusanyiko: Wazo la kwamba jinsi utu mpya unavyokuwa na uvutano juu ya ulimi wetu litazungumziwa katika hotuba-mfululizo ya pili yenye kichwa, “Kusitawisha Ulimi wa Wenye Hekima.” Hotuba ya watu wote ni yenye kichwa, “Je, Wewe Ni Mwenye Kushinda Yule Mwovu?” ambacho kitakazia uhitaji wa kubaki macho kuhusu njia za ujanja za Shetani. Hotuba mbili za mwisho za mkusanyiko zenye vichwa, “Endelea Kujitunza Bila Doa Kutokana na Ulimwengu” na “Siku Baada ya Siku Tufanye Upya Utu Wetu wa Ndani,” zitatusaidia kuacha maoni na mwenendo vinavyopingana na njia za uadilifu za Mungu na kubaki imara katika ibada yetu kwa Yehova.
Tunatazamia kabisa kupokea kitia moyo hicho ili kujivika na kudumisha utu mpya.