Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Apr. 15
“Karibu kila mtu anakubaliana kwamba mojawapo ya siri ya kuwa na maisha yenye furaha ni kupashana habari vizuri, hata hivyo watu wengi wana magumu ya kupashana habari vizuri. Kwa nini inakuwa hivyo? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linatoa mapendekezo kuhusu namna ya kusitawisha ufundi mbalimbali wa kupashana habari.” Soma Yakobo 1:19.
Amkeni! Apr.
“Watu wengi wanasema kwamba msalaba unawasaidia wajisikie kuwa karibu zaidi na Mungu. Hata hivyo, wengine wanajiuliza: Je, ni jambo linalofaa kuheshimu sana chombo kilichotumiwa ili kumuua Yesu? Je, kweli Yesu alikufa kwenye msalaba? Habari ya mwanzoni kwenye ukurasa wa 12 inazungumzia maulizo hayo kutokana na maoni ya Biblia.” Soma Matendo 5:30.
Mnara wa Mlinzi Mei 1
“Mamilioni ya watu ulimwenguni pote wanateseka kutokana na umaskini. Unafikiri ni jambo gani linaloweza kufanywa ili kuwasaidia? [Acha mtu ajibu. Kisha soma 1 Petro 2:21.] Gazeti hili linazungumzia jinsi tunavyoweza kufuata mfano wa Yesu katika kuhangaikia maskini.”
Amkeni! Mei
“Je, umekwisha kujiuliza kwa nini tunazeeka? [Acha mtu ajibu.] Maelezo ya Biblia kuhusu sababu inayofanya tuzeeke yanaonyesha jinsi ambavyo Mungu amefanya iwezekane kwetu kufurahia maisha yasiyo na mwisho. [Soma Isaya 25:8.] Gazeti hili la Amkeni! linazungumzia mawazo fulani ya kisasa kuhusu jinsi tunavyofikia kuzeeka.”