Programu Mpya ya Mkusanyiko wa Mzunguko
Ulimwengu unapenda kutufanya sisi tuamini kwamba mfumo wa mambo wa sasa utaendelea milele kama ulivyo. Lakini, Neno la Mungu linatuambia kwamba mambo hayataendelea kuwa vile yalivyo. (1 Yoh. 2:15-17) Neno la Mungu linatusaidia tuelewe kwamba ‘kujiwekea hazina duniani’ ni kazi bure. Ili kuwatia nguvu watu wa Mungu, programu ya mkusanyiko wa mzunguko ya mwaka wa utumishi wa 2007 itazungumzia kichwa “Jiwekeeni Hazina Mbinguni.”—Mt. 6:19, 20.
Andiko la Waefeso 2:2 linaposema juu ya “mamlaka ya hewa, roho ambayo sasa hutenda katika wana wa kutotii,” jambo hilo linatia ndani kufikiria sana ufuatiaji wa vitu vya kimwili. Kama tu vile hewa inavyoenea mahali pote na kila mtu anaweza kuipumua, ndivyo “roho ya ulimwengu” inavyoenea mahali pote katika ulimwengu huu. (1 Kor. 2:12) Kwa kuwa roho ina uvutano wenye nguvu, ndiyo sababu inaitwa kuwa “mamlaka.” Programu mpya ya mkusanyiko wa mzunguko itatusaidia kuepuka kufikiria sana ufuatiaji wa vitu vya ulimwengu na kulinda kabisa katika akili jambo lililo la maana zaidi. (Mt. 6:33) Pia, programu hiyo itatusaidia kumtegemea Yehova tunapotimiza kazi yetu ya kuhubiri ijapokuwa mikazo na majaribu tunayoweza kukutana nayo.
Fanya nguvu ili uhuzurie siku hizo zote mbili na pia ‘ukazie uangalifu zaidi kuliko ilivyo kawaida.’ (Ebr. 2:1) Andika mambo ya lazima kwa ufupi; mambo ambayo unaweza kutumia kipekee katika maisha yako na katika kazi yako ya kuhubiri. Kwa kuhuzuria programu hiyo ya kiroho yenye kuleta faida mwanzo mpaka mwisho, utatiwa moyo na kutiwa nguvu ili kuendelea ‘kuweka hazina mbinguni’!