Kazi ya Kuhubiri Nyumba kwa Nyumba
1 ‘Wale wanaozoea kueneza Kweli watakubali kwamba kampanye ya kuhubiri nyumba kwa nyumba kwa kutumia kitabu L’AURORE DU MILLÉNIUM ni njia yenye matokeo zaidi ya kuhubiri Kweli wakati huu.’ Maneno hayo yanayotoka katika Phare de la Tour de Sion ya tarehe 1 mwezi wa 7, 1893 yalionyesha samani ya mahubiri ya nyumba kwa nyumba. Watu ulimwenguni pote wameona kazi hiyo kuwa alama yenye kutambulisha wazi Mashahidi wa Yehova. Kwa kuwa ni jambo gumu kupata watu nyumbani katika maeneo fulani, je, njia hiyo ingali yenye kufaa?
2 Kazi Hiyo Inapatana na Maandiko na Ni ya Maana: Kazi ya kuhubiri nyumba kwa nyumba inapatana na Maandiko. Yesu aliagiza wanafunzi wake 70 waende wawili-wawili kwenye nyumba za watu. (Luka 10:5-7) Wakati kidogo kisha kufa kwa Yesu, Biblia inasema hivi kuhusu wanafunzi wake: “Kila siku katika hekalu na nyumba kwa nyumba wakaendelea bila kuacha kufundisha na kutangaza habari njema.” (Mdo. 5:42) Mtume Paulo pia alifundisha kwa bidii nyumba kwa nyumba.—Mdo. 20:20.
3 Kazi ya kuhubiri nyumba kwa nyumba inaendelea kuwa njia ya maana ya kueneza habari njema leo. Inatusaidia ‘kutafuta’ wale wanaostahili kwa kutumia ufundi na kwa njia ya utaratibu. (Mt. 10:11) Kwa kawaida watu ni wenye kutulia sana nyumbani. Kuzungumza nao uso kwa uso kwa kusikiliza sauti yao, kuona ishara zao za uso, na kutazama vitu vinavyowazunguka, kutatusaidia tutambue mambo yanayowapendeza na yale wanayohangaikia. Kwa kawaida, kuhubiri nyumba kwa nyumba kunatutolea nafasi bora ya kuendelea na mazungumzo zaidi.
4 Tengeneza Programu Yako: Mtume Paulo alikuwa tayari kufanya mabadiliko katika mambo yake “kwa ajili ya habari njema.” (1 Kor. 9:23) Labda tunaweza kutengeneza programu yetu ili kuhubiri wakati ambapo watu wengi zaidi wanaweza kupatikana nyumbani, kama vile magaribi, miisho-juma, au wakati wa mapumziko. Andika namba za nyumba ambako haukukuta watu, na ujaribu tena kuwarudilia siku nyingine au wakati mwingine.
5 Hata wale walio na matatizo ya afya wanaweza kuhubiri nyumba kwa nyumba. Labda tunaweza kufanya mipango watusindikize mahali ambapo wanaweza kufika kwa urahisi, hilo litawasaidia wahubiri kulingana na hali yao. Dada mmoja aliyekuwa na matatizo ya kupumua alikuwa na uwezo wa kuhubiri nyumba moja tu kila dakika 30. Hata hivyo, alitosheka na kuwa mwenye furaha kabisa alipohubiri na wengine.
6 Watu wengi walio mfano wa kondoo wanaendelea kupatikana kupitia mahubiri ya nyumba kwa nyumba. Mhubiri mmoja aligonga kwenye mlango na mtu aliyekuwa ndani ya nyumba alimjibu hivi: “Ingia. Ninajua wewe ni nani. Nilikuwa nikimwomba Mungu anitumie mtu fulani ili anisaidie, kisha nikasikia mtu akigonga mlangoni. Mungu alinisikiliza na anakutuma kwangu.” Matokeo hayo yanaonyesha kwamba Yehova anabariki namna hii ya kuhubiri. (Mt. 11:19) Uwe na programu ya kuhubiri nyumba kwa nyumba kwa ukawaida.
[Maulizo ya Funzo]
1. Ni ulizo gani linalotokezwa kuhusiana na mahubiri ya nyumba kwa nyumba, na kwa nini?
2. Kazi ya kuhubiri nyumba kwa nyumba inapatana na Maandiko gani?
3. Ni faida gani mbalimbali zinazotokana na kuhubiri nyumba kwa nyumba?
4. Tunawezaje kufanya kazi ya kuhubiri nyumba kwa nyumba iwe na matokeo zaidi?
5. Tunawezaje kusaidia wale walio na matatizo ya afya wahubiri nyumba kwa nyumba?
6. Kwa nini tunapaswa kuwa na programu ya kuhubiri nyumba kwa nyumba kwa ukawaida?