Programu Mpya ya Mkusanyiko wa Mzunguko
Yehova anastahili kutukuzwa. Namna gani tunamtukuza Yehova? Ni nini kinachofanya iwe vigumu kwa wengi kumtukuza Yehova? Ni baraka gani wanazopata wale wenye kumtukuza Mungu leo? Programu ya mkusanyiko wa mzunguko ya mwaka wa utumishi wa 2008 itatoa majibu yenye kutosheleza kwa maulizo hayo. Programu hiyo ni yenye kichwa: “Fanyeni Mambo Yote kwa Utukufu wa Mungu.” (1 Kor. 10:31) Fikiria mambo yanayotungojea muda wa siku mbili za ufundishaji mkubwa wa kiroho.
Mwangalizi wa wilaya atazungumzia vichwa: “Kwa Nini Kumtukuza Mungu?” na “Uwe Mfano Katika Kutimiza Matakwa ya Mungu.” Atatoa hotuba ya watu wote yenye kichwa: “Ni Watu Gani Wanaomtukuza Mungu?,” na hotuba ya kumalizia yenye kichwa: “Kumtukuza Mungu kwa Umoja Ulimwenguni Pote.” Ataongoza pia Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Mwangalizi wa mzunguko atazungumzia vichwa: “Furahia Kuangaza Utukufu wa Mungu,” “Sikiliza Mahitaji ya Mzunguko,” na “Endeleeni ‘Kuwekwa Imara Katika Kweli,’” kichwa chenye kutegemea andiko la 2 Petro 1:12. Pia tutajifunza jinsi “Utumishi wa Upainia Unavyomtukuza Mungu.” Hotuba ya kwanza kati ya hotuba-mfululizo mbili zenye kuchochea watu wafikiri ni yenye kichwa: “Kumtukuza Mungu Katika Sehemu Zote za Maisha Yetu,” itazungumzia kwa undani sana maana ya maneno yenye kupatikana kwenye 1 Wakorintho 10:31. Hotuba-mfululizo yenye kichwa: “Kutoa Utumishi Mtakatifu ili Kumtukuza Yehova” itazungumzia sehemu mbalimbali za ibada yetu. Tutafurahia pia kuwa na kifupi cha funzo la Mnara wa Mlinzi na mazungumzo kuhusu andiko la Siku ya Yenga. Kutakuwa pia nafasi kwa ajili ya ubatizo.
Watu walio wengi wanakataa kumtambua Mungu. Wengi wanakengeushwa akili na mipango ya wanadamu na hilo linafanya wasifikirie utukufu wa Yehova. (Yoh. 5:44) Lakini tunasadiki kwamba ni jambo la maana sana kutumia wakati ili kufikiria jinsi ya “Kufanya Mambo Yote kwa Utukufu wa Mungu.” Fanya mpango ili uhuzurie na ufaidike na vipindi vyote vine.