Programu Mpya ya Mkusanyiko wa Mzunguko
Namna gani inawezekana kusimama imara zidi ya wale wanaopinga vikali ibada ya kweli? Namna gani tunaweza siku zote kushinda nguvu zinazojaribu kuturudisha katika ulimwengu usiomwogopa Mungu? Mkusanyiko wa mzunguko kwa ajili ya mwaka wa utumishi wa 2009 utatoa majibu kwa maulizo hayo ya maana. Mkusanyiko huu una kichwa: “Endelea Kuushinda Uovu kwa Wema.” (Rom. 12:21) Programu itakuwa na habari zinazoonyeshwa hapa chini.
Mwangalizi wa wilaya atatoa hotuba zifuatazo: “Tumetiwa Nguvu Ili Kuushinda Uovu kwa Wema,” “Uwe Mwangalifu—Usijitumainie Kupita Kiasi,” “Karibuni Uovu Wote Utakwisha Kabisa,” na “Kufanya Imani Yetu Iwe Nguvu Ili Kuushinda Ulimwengu.” Mwangalizi wa mzunguko atatutolea hotuba yenye kichwa “Sasa Ndio Wakati wa Kukaa Macho!,” inayotegemea andiko la Waroma 13:11-13, na “Usijionyeshe Kuwa Umevunjika Moyo Siku ya Taabu,” inayotegemea andiko la Methali 24:10. Pia tunangojea kwa hamu sehemu ya mwangalizi wa mzunguko yenye kichwa “Sikiliza Mahitaji ya Mzunguko.” Hotuba nyingine yenye kujenga itakuwa na kichwa “Je, Unaweza ‘Kuwa Katika Huduma Hii’ Ukiwa Painia?” Hotuba-mfululizo ya kwanza ni yenye kichwa “Simama Imara Zidi ya Njia za Udanganyifu za Shetani.” Itatusaidia tutambue na kuepuka njia za udanganyifu za Shetani katika mambo ya teknolojia, kujiburudisha, na elimu. Hotuba-mfululizo yenye kichwa “Tujipatie Nguvu Ili Kumpinga Shetani Katika Siku Hizi za Uovu” itatuonyesha jinsi ya kutumia vizuri kabisa shauri lililoongozwa na roho lililo katika andiko la Waefeso 6:10-18.
Kuna uhusiano wa karibu kati ya kuushinda uovu kutoka chanzo chake, na kuhubiri ujumbe wa Ufalme. (Ufu. 12:17) Haishangazi kwamba Shetani anashambulia Mashahidi wa Yehova bila kuacha! (Isa. 43:10, 12) Lakini Shetani atashindwa kabisa kwa kuwa tumekusudia sana ‘kuendelea kuushinda uovu kwa wema.’ Fanya mipango ili kufaidika kabisa na vipindi vyote vine vya mkusanyiko huu wa mzunguko.