Mpango Mpya kwa Ajili ya Wahudumu Wakristo
1. Ni mpango gani mpya ulioanza tangu mwaka wa 1938, na kwa kusudi gani?
1 Katika mwaka wa 1938, Tengenezo la Yehova lilianzisha mpango mpya. Makutaniko yalialikwa kwenye mikusanyiko iliyoitwa assemblées de zone, ambayo inaitwa sasa mikusanyiko ya mzunguko. Kwa kusudi gani? Informant (inayoitwa sasa Huduma Yetu ya Ufalme) ya mwezi wa 1, 1939, inajibu: ‘Mikusanyiko hiyo ni sehemu ya Tengenezo la Kitheokrasi la Yehova ili kuongoza kazi yake ya Ufalme. Mafundisho yanayotolewa kwenye misanyiko hiyo ni ya lazima sana kwa kila mutu ili atimize inavyofaa kazi aliyogawiwa.’ Tunapofikiria ongezeko la watangazaji wa Ufalme toka hesabu ya watangazaji 58,000 tu katika 1938 kufikia watangazaji zaidi ya 7,000,000 katika 2009, ni wazi kwamba mikusanyiko ya mzunguko, inatimiza kusudi layo la kusaidia wahubiri “watimize kazi waliyogawiwa”!
2. Ni habari gani zitakazotolewa kwenye mkusanyiko wetu wa mzunguko wa mwaka mpya wa utumishi?
2 Kichwa cha Mkusanyiko wa Mzunguko wa Mwaka Ujao: Tunangojea programu itakayoanza mwezi wa 9 na kitia-moyo kitakachotolewa. Mkusanyiko huo utakuwa na kichwa: “Ninyi Si Sehemu ya Ulimwengu” kutoka katika andiko la Yohana 15:19. Ni hotuba gani zilizopangwa, ambazo bila shaka zitasaidia wahubiri? Ni hotuba kama vile “Utumishi wa Wakati Wote Unatulinda—Namna Gani?” itakayotolewa Siku ya Posho; siku hiyo tutafurahia pia hotuba-mfululizo yenye sehemu tatu, yenye kichwa “Usiambukizwe na . . .” “Mnyama-Mwitu,” “Kahaba Mkubwa,” na “Wanabiashara Wanaosafiri.” Siku ya Yenga tutasikiliza hotuba-mfululizo yenye kichwa “Umpende Yehova, Wala Si Ulimwengu.” Hotuba nyingine zitakazotolewa ni kama vile, “Muendelee Kuishi Kama ‘Wageni na Wakaaji wa Muda’” na “Ujipe Moyo! Unaweza Kuushinda Ulimwengu.”
3. Ni faida gani tunazoweza kupata kwa kuhuzuria mkusanyiko wa mzunguko unaokuja?
3 Kisha kuhuzuria mkusanyiko wa mzunguko wa hivi karibuni, dada mmoja ambaye alianza kupuuza kazi ya kuhubiri aliandika kwamba programu hiyo ilimusaidia achunguze upya hali zake na kukusudia “kuhubiri na kuacha kutoa visababu visivyofaa!” Bila shaka programu ya mkusanyiko ya mwaka mpya wa utumishi itatusaidia sisi wote kumpenda Yehova kuliko kuupenda ulimwengu. (1 Yoh. 2:15-17) Ujikaze kuhuzuria na kuwa mwangalifu ili ufaidike kabisa na mpango huo wenye upendo kwa ajili ya wahudumu Wakristo!