Linda Akili Yako
1. Mukusanyiko wa muzunguko wa mwaka wa utumishi wa 2013 una kichwa gani, na programu hiyo ina kusudi gani?
1 Yesu aliwafundisha wanafunzi wake wamupende Yehova kwa moyo wao wote, kwa nafsi yao yote, na kwa akili yao yote. (Mt. 22:37, 38) Mwaka huu, kusudi la mikusanyiko yetu, ni kusema, mukusanyiko wa wilaya, wa muzunguko, na wa pekee, ni kutusaidia ili tuufanye utu wetu wa ndani uwe na nguvu. Tunakumbuka kama kichwa cha mukusanyiko wa wilaya kilikuwa “Linda Moyo Wako!” Programu ya mukusanyiko wa pekee wa mwaka wa utumishi wa 2013 una kichwa “Linda Zamiri Yako.” Na mikusanyiko ya muzunguko ambayo itaanza mwezi wa 9 itakuwa na kichwa “Linda Akili Yako,” na itategemea andiko la Mathayo 22:37. Kusudi la programu hiyo ni kusaidia kila mumoja wetu achunguze mawazo yake ili kuyafanya yamufurahishe Yehava zaidi.
2. Tunapaswa kutafuta majibu ya maulizo gani wakati wa mukusanyiko wetu wa muzunguko?
2 Mambo Tutakayofundishwa: Tutakapofuata programu ya mukusanyiko wa muzunguko, tunapaswa kutafuta majibu ya maulizo haya, ambayo yanarudilia mambo makubwa ya mukusanyiko huo:
• Namna gani tunaweza kuepuka ‘mawazo ya watu’?
• Namna gani tunaweza kusaidia ili kuondoa kitambaa kinachopofusha akili za watu?
• Sisi tunataka kuwa na mutazamo gani wa akili?
• Kutafakari kwa njia inayofaa kuna faida gani?
• Namna gani tunaweza kuacha Yehova aongoze mawazo yetu?
• Namna gani bwana, bibi, wazazi, na watoto wanaweza kusaidia ili familia iwe na furaha?
• Namna gani tunaweza kuwa tayari kwa ajili ya ile siku ya Yehova?
• Inamaanisha nini kukaza akili yetu kwa ajili ya utendaji?
• Wale wanaotumia mambo wanayojifunza wanapata baraka gani?
3. Sababu gani ni lazima kuhuzuria siku zote mbili, kufuata kwa uangalifu, na kutumia mambo tutakayojifunza?
3 Shetani anatupiganisha ili kuharibu akili zetu. (2 Kor. 11:3) Kwa hiyo, sisi pia tunapaswa kufanya nguvu ili kulinda mawazo yetu, kuyafanya yamupendeze Yehova. Ni lazima tuendelee kuiga akili ya Kristo ili kushindana na uvutano wa ulimwengu huu usiofuata sheria. (1 Kor. 2:16) Hivyo basi, tufanye mipango ili kuhuzuria siku mbili zote za mukusanyiko. Tufuate kwa uangalifu. Kutumia habari ya maana itakayotolewa kwenye mukusanyiko kutatusaidia tukaze akili zetu juu ya utumishi wa Ufalme na kuufanya kwa bidii.—1 Pet. 1:13.