Mkusanyiko wa Wilaya wa Mashahidi wa Yehova wa 2008
1 Mtume Paulo alitia moyo Wakristo Waebrania kukusanyika pamoja na kutiana moyo “zaidi kwa kadiri” walivyoona kuwa siku hiyo ilikuwa inakaribia. (Ebr. 10:24, 25) Kuna mambo mengi yanayohakikisha kwamba “siku” ambayo Paulo alizungumzia inakaribia sana! Kwa hiyo, tunatazamia kukusanyika pamoja na ndugu na dada zetu ili kupokea mafundisho ya kiroho yanayoweza kutuongoza katika hizi “siku za mwisho” zinazoendelea kuwa mbaya sana. (2 Tim. 3:1) Tutakuwa na nafasi ya kufanya hivyo kwenye mkusanyiko wa wilaya wa 2008 unaokuja.
2 Huzuria Siku Zote Tatu: Tunawatia moyo kuhuzuria mkusanyiko siku zote tatu. Kwa ‘kukusanyika pamoja sisi wenyewe,’ hatutakosa mafundisho yatakayotolewa kwenye mkusanyiko. (Ebr. 10:25) Anza kujitayarisha sasa. Julisha bwana wako wa kazi mbele ya wakati ili afanye mipango inayohitajiwa. Ikiwa watoto wako watakuwa shuleni wakati wa mkusanyiko wenu, julisha walimu wao kuhusu mipango yenu. Uwajulishe kwamba mkusanyiko ni sehemu ya ibada yenu. Uwe hakika kwamba Yehova atabariki bidii yako ya kutia faida za Ufalme pa nafasi ya kwanza.—Mt. 6:33.
3 Saidia Wengine Wahuzurie: Paulo aliomba pia ndugu zake ‘kufikiriana mmoja na mwenzake.’ (Ebr. 10:24) Je, ndugu na dada katika Funzo lenu la Kitabu la Kutaniko wanahitaji msaada ili kuhuzuria mkusanyiko? Je, unaweza kusaidia watu unaojifunza nao Biblia wahuzurie mkusanyiko pamoja nawe, hata ikiwa wanaweza kuhuzuria siku moja tu? Unapowajulisha watu wa familia yako wasioamini kuhusu mipango yako ya mkusanyiko, uwaalike waende pamoja nawe. Bidii yako yenye kuchochewa na upendo inaweza kutokeza baraka usizotazamia.
4 Huzuria Mkusanyiko wa Mahali Ambapo Kutaniko Lenu Limealikwa: Barua yenye kuonyesha mahali pote ambapo mkusanyiko utafanywa itabandikwa kwenye ubao wa matangazo kisha kuchunguza nyongeza hii kwenye Mkutano wa Utumishi. Inapendekezwa kwamba wote wafikirie katika sala mahali ambapo watahuzuria mkusanyiko katika mwaka wa 2008. Ili kuhakikisha kwamba kutakuwa viti, vitabu, vyumba vya kupangia vya kutosha n.k., tunawatia moyo kuhuzuria mkusanyiko wa mahali ambapo kutaniko lenu limealikwa. Hata hivyo, ikiwa hali zako hazikuruhusu kuhuzuria mkusanyiko mahali ambapo kutaniko lenu limealikwa, basi uko huru kuhuzuria mkusanyiko wa mahali pengine.
5 Upangishaji: Ikiwa unapenda kupangishwa katika nyumba ya ndugu au katika Jumba la Ufalme, tunapendekeza kwamba mwandishi aandike mbele ya wakati majina ya wahubiri wote wanaotaka kupangishwa na kuyatuma kwenye Biro ya Upangishaji kwenye mji wa mkusanyiko. Kwenye karatasi hiyo atatia jina, ikiwa mtu ni mwanaume au mwanamke, miaka ya kuzaliwa na uhusiano wa Kifamilia wa kila muhubiri. Hilo litasaidia ndugu wanaohusika na Biro ya Upangishaji, wawe na wakati wa kutosha ili kupata mahali pa kupangisha wote. Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko itachunguza sifa za kila mhubiri mbele ya kutuma maombi hayo kwenye Biro ya Upangishaji. Tukiisha kupewa mahali pa kupanga, halitakuwa jambo lenye kufaa kufanya mipango yetu wenyewe baadaye ili kwenda kukaa pamoja na ndugu au rafiki mwingine. Jambo hilo linaweza kuvuruga kazi ya ndugu wanaoshugulika na Biro ya Upangishaji. Hata hivyo, ikiwa yeyote anakusudia kukaa pamoja na mshiriki wa familia; asiye ndugu wa kiroho; hapaswi kuomba mwandishi atie jina lake kwenye karatasi ya wenye kuomba kupangishwa.
6 Tunawatolea maagizo fulani hapa kuhusu namna ya kushugulikia upangishaji katika Jumba la Ufalme. Halmashauri ya Mkusanyiko wa Wilaya itampatia mzee fulani mgawo ili asimamie mpango huo. Atakuwa na msaidizi, kwa kawaida mzee mwingine au mtumishi wa huduma mwenye kustahili, aliye na sifa za kiroho. Jumba linapaswa kugawanywa katika sehemu mbili: sehemu moja kwa ajili ya dada na watoto wao, na pia mabinti na sehemu nyingine kwa ajili ya ndugu na washiriki wengine wa kiume. Jumba la Ufalme litatumiwa kwa kulala tu. Wote wanapokuwa mahali pa mkusanyiko mchana, kazi ya ulinzi itapangwa kwa zamu ili kuzuia vitu vya ndugu visiibwe. Ndugu wenye kujiheshimu, wenye sifa za kiroho ndio wanaopaswa kutumiwa ili kufanya kazi ya ulinzi. Haitaruhusiwa kupikia chakula ndani ya Jumba la Ufalme. Kibanda cha muda kinaweza kujengwa katika uwanja, ili kitumiwe kuwa mahali pa kupikia muda wa mkusanyiko tu. Mwishoni mwa mkusanyiko, kibanda hicho kitabomolewa. Ni jambo la maana kwamba Jumba la Ufalme na vilevile uwanja, vilindwe katika hali ya usafi na utaratibu. Inafaa kuwa waangalifu ili kitu chochote kisiharibiwe. Wale wanaokaa katika Jumba la Ufalme watafanya yote wawezayo ili waonyeshe mwenendo unaostahili Wakristo wa kweli, kati yao wenyewe na vilevile kuelekea majirani.—1 Kor. 10:31.
7 Matendo Mazuri: Tunapotii amri ya Yehova ya kukusanyika pamoja ili kuabudu ‘tunajifaidi wenyewe.’ Jambo la maana zaidi ya hilo, ni kwamba hilo linatutolea nafasi ya kutukuza jina la Yehova. (Isa. 48:17) ‘Matendo yetu mazuri yanaonekana wazi mbele ya watu wote’ kwenye mikusanyiko ya wilaya, na watu fulani wamechochewa kuonyesha maoni yao kuhusu matendo yetu mazuri. (1 Tim. 5:25) Alipowaona ndugu wakitengeneza uwanja wa mkusanyiko, mtu mmoja alisema hivi: “Nilipoona picha katika vitabu vyenu kuhusu paradiso, nilikuwa nifikiri kwamba ‘Mashahidi ni waotaji ndoto kabisa.’ Lakini sasa ninaona kwamba wanaweza kufanya dunia kuwa paradiso!” kisha alitoa mitungi miwili yenye maua akisema: “Tafazali, chukueni mitungi hii yenye maua, ili mimi pia nishiriki katika kazi munayofanya.” Katika mji mmoja ambako mikusanyiko imefanywa kwa miaka mingi, msimamizi mmoja wa hoteli alisema hivi: “Watu wengi katika mji wanazungumza kuhusu Mashahidi wa Yehova na mambo tunayoweza kujifunza kutokana na mikusanyiko yenu. Tunajua namna watu wenu wanavyofanya usafi wa kituo cha jamii (kama vile commune) na tunawaona mukifanya usafi wa mahali pa kuegeshea magari. Ni jambo lenye kupendeza kuwa pamoja nanyi muda wa kipindi cha mkusanyiko wenu. Tunatumaini kwamba tunaweza kuendelea kushirikiana nanyi katika miaka inayokuja.” Mwenendo wa ndugu zetu ambao unafanya watu watoe maelezo hayo unapaswa kufurahisha moyo wa Mungu wetu, Yehova!
8 Yesu alisema kwamba maisha yetu yanategemea kabisa kusikiliza “kila neno linalotoka katika kinywa cha Yehova.” (Mt. 4:4) Kwenye mikusanyiko yetu ya kila mwaka, Yehova anatutolea ‘chakula cha kiroho wakati unaofaa,’ chakula kinachotayarishwa na “mtumwa mwaminifu na mwenye busara.” (Mt. 24:45) Kazi nyingi inafanywa ili kutayarisha na kutoa karamu hii ya kiroho. Na tuonyeshe shukrani yetu kwa Yehova anayetuhangaikia kwa upendo. Tutaonyesha shukrani hiyo kwa kuhuzuria na kuwa wasikivu kwenye kila sehemu ya programu.
[Maulizo ya Funzo]
1. (a) Kwa nini shauri la Paulo kwa Wakristo Waebrania lina maana ya pekee na pia ni lenye uharaka zaidi sana leo? (Soma Waebrania 10:24, 25.) (b) Wakati ujao tutakuwa na nafasi gani itakayotufanya tutumie shauri la Paulo?
2. (a) Kwa nini ni jambo la maana kuhuzuria siku zote tatu za mkusanyiko? (b) Namna gani tutaanza kujitayarisha ili tuhuzurie mkusanyiko?
3. Ni katika njia gani tunaweza kuonyesha kwamba tunawafikiria wengine?
4. Kwa nini tunapaswa kuhuzuria mkusanyiko wa mahali ambapo kutaniko letu limealikwa?
5. Ni mambo gani ya maana tunayopaswa kuweka akilini wakati tuna lazima ya kupangishwa, na kwa nini?
6. (a) Ni mipango gani inayopaswa kuchukuliwa ikiwa ndugu na dada wanapangishwa katika Jumba la Ufalme? (b) Ni mambo gani fulani unayopaswa kufikiria unapojitayarisha kuhuzuria Mkusanyiko wa Wilaya? (Ona kisanduku “Mambo Fulani ya Kufikiria . . .”)
7. (a) Ni katika njia gani tunaweza kumtukuza Yehova tunapohuzuria mkusanyiko wetu? (b) Kwa sababu ya matendo mazuri na mwenendo mzuri wa ndugu zetu, ni maelezo gani yalitolewa na watazamaji na msimamizi wa hoteli?
8. Namna gani Mathayo 4:4 inaonyesha umaana wa kuwa wasikivu kwa kila sehemu ya programu?
[Kisanduku kwenye ukurasa wa 3]
Saa za Programu
――
Siku ya Tano na Siku ya Posho
3:20 asubuhi - 10:55 kisha mchana-kati
Siku ya Yenga
3:20 asubuhi - 10:00 kisha mchana-kati
[Kisanduku kwenye ukurasa wa 4]
Mambo Fulani ya Kufikiria Unapotazamia Kuhuzuria Mkusanyiko wa Wilaya
1. Ikiwa unaombwa kufanya safari ndefu ili kuhuzuria mkusanyiko, hivyo basi anza kuchunga feza mapema zaidi iwezekanavyo ili uweze kupata feza za kutosha zitakazokusaidia kusafiri na kuwa na chakula kwa ajili yako mwenyewe na familia yako.
2. Fikiria pia kutegemeza mipango ya mkusanyiko kupitia zawadi zako za kujipendea. ‘Mtu yeyote asionekane mbele za Yehova mikono mitupu,’ lakini ‘Mheshimu Yehova kwa vitu vyako vyenye samani’—Kum. 16:16; Met. 3:9.
3. Wakati wa mkusanyiko, tunatukuza jina la Yehova kupitia mwenendo wetu mzuri, na mavazi yetu safi na yenye heshima.—1 Kor. 10:31.
4. Kusudia kuunga mkono ndugu wanaokaribisha watu mahali pa mkusanyiko na ndugu wengine wenye kuwa na daraka la kulinda utaratibu. Usichungie watu viti, isipokuwa washiriki wa karibu wa familia yako na wale wanaosafiri pamoja nawe.
5. Ili ufaidike kabisa na kipindi cha kisha mchana-kati, tumia tu chakula chepesi wakati wa kupumzika. Chakula kizito kinaweza kuleta usingizi.—Luka 8:18.
6. Usafi unamletea Yehova heshima. Mwishoni mwa kila kipindi, kila mmoja wetu anaweza kutimiza daraka lake ili kuacha mahali pa mkusanyiko pakiwa safi kwa kuokota vikaratasi na uchafu wa aina yoyote na kuutupa katika mahali au vyombo vya kutupia uchafu vilivyotayarishwa kwa kusudi hilo.—1 Pet. 1:15, 16.