Mkusanyiko wa Wilaya wa Mashahidi wa Yehova wa 2009
1. (a) Ni baraka gani ambazo tutapata kwa kuhuzuria siku zote tatu za mkusanyiko wa wilaya? (b) Ni mipango gani tunayopaswa kufanya sasa?
1 Sisi wote tunangojea kwa hamu mkusanyiko wa wilaya wa 2009 na nafasi mpya za kukusanyika pamoja na Wakristo wenzetu wenye kumsifu Yehova, “wanaotambua uhitaji wao wa kiroho.” (Mt. 5:3) Kwa kuwa siku ya Yehova inakaribia kwa haraka, tunatia moyo kila mmoja kuhuzuria siku zote tatu ili afaidike kabisa kwa kuungana kwa uchangamfu pamoja na Wakristo wenzetu na pia kutiwa moyo kiroho ili kubaki imara katika imani. (Sef. 1:14) Tuwajulishe walimu na wakubwa wa kazi kwamba mkusanyiko ni sehemu ya maana ya ibada yetu. Tufanye mipango yetu kwa bidii mbele ya wakati, na tutafute baraka ya Yehova; hivyo tunaweza kuwa hakika kwamba atatutegemeza.—Isa. 50:10.
2. Ni hali gani inayofanana na ile ya mikusanyiko ya kimataifa tunayoweza kutazamia hata ikiwa hatukualikwa kuhuzuria mkusanyiko wa kimataifa?
2 Mikusanyiko ya Kimataifa: Kwa kuwa mikusanyiko hii itafanywa katika inchi chache na miji michache, ni wale wanaoalikwa tu ndio watahuzuria. Tunapounga mkono mpango huo, hilo litafanya kusiwe msongamano. (1 Kor. 14:40; Ebr. 13:17) Hata hivyo, mikusanyiko mingi ya wilaya itakuwa na hali yenye kufanana na ile ya mikusanyiko ya kimataifa, kwa kuwa wamishonari wengi, Wanabetheli wanaotumikia katika inchi za kigeni, na watumishi wa kimataifa watahuzuria mikusanyiko katika inchi zao.
3. Katika kutaniko letu, namna gani tunaweza kuwaonyesha watu fulani upendo wa Kikristo?
3 Tuwasaidie Wengine Wahuzurie: Je, kuna watu fulani katika kutaniko lenu wanaohitaji msaada ili kuhuzuria mkusanyiko? Tunaposaidia wengine kufanya hivyo, ‘tunaendelea kuangalia, si faida za kibinafsi za mambo yetu wenyewe tu, bali pia faida za kibinafsi za wengine.’—Flp. 2:4.
4-6. (a) Ni mambo gani ya maana tunayopaswa kuweka akilini wakati tuna lazima ya kupangishwa, na kwa nini? (b) Ni mipango gani inayopaswa kuchukuliwa ikiwa ndugu na dada wanapangishwa katika Jumba la Ufalme? (c) Ni mambo gani fulani tunayopaswa kufikiria tunapojitayarisha kuhuzuria mkusanyiko wa wilaya? (Ona kisanduku kwenye ukurasa wa 4.)
4 Upangishaji: Upangishaji katika mji wa mkusanyiko utafanywa kwa kawaida katika nyumba za ndugu, katika Majumba ya Ufalme ao katika nyumba za washiriki wa jamaa. Karatasi yenye kuonyesha mahali pote ambapo mkusanyiko utafanywa itawekwa kwenye ubao wa matangazo wa kutaniko kisha kuchunguza nyongeza hii kwenye Mkutano wa Utumishi. Inapendekezwa kwamba wote wafikirie katika sala mahali ambapo watahuzuria mkusanyiko katika mwaka wa 2009.
5 Ikiwa unapenda kupangishwa katika nyumba ya ndugu ao katika Jumba la Ufalme, tunapendekeza kwamba mwandishi aandike mbele ya wakati majina ya wahubiri wote wanaotaka kupangishwa na kuyatuma kwenye Biro ya Upangishaji katika mji wa mkusanyiko. Kwenye karatasi hiyo atatia jina la kila mhubiri, ataonyesha ikiwa ni mwanaume ao ni mwanamuke, miaka yake ya kuzaliwa na uhusiano wa kifamilia wa wahubiri (ikiwa ni washiriki wa familia moja). Hilo litasaidia ndugu wanaohusika na Biro ya Upangishaji, wawe na wakati wa kutosha ili kupata mahali pa kupangisha wote. Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko itachunguza sifa za kila mhubiri mbele ya kutuma maombi hayo kwenye Biro ya Upangishaji. Tukiisha kupewa mahali pa kupanga, halitakuwa jambo lenye kufaa kufanya mipango yetu wenyewe baadaye ili kwenda kukaa pamoja na ndugu ao rafiki mwingine. Jambo hilo linaweza kuvuruga kazi ya ndugu wanaoshugulika na Biro ya Upangishaji. Hata hivyo, ikiwa yeyote anakusudia kukaa pamoja na mshiriki wa familia asiye ndugu wa kiroho, hapaswi kuomba mwandishi atie jina lake kwenye karatasi ya wenye kuomba kupangishwa.
6 Tunawatolea maagizo fulani hapa kuhusu namna ya kushugulikia upangishaji katika Jumba la Ufalme. Halmashauri ya Mkusanyiko wa Wilaya itampatia mzee fulani mgawo ili asimamie mpango huo. Atakuwa na msaidizi, kwa kawaida mzee mwingine ao mtumishi wa huduma mwenye kustahili, aliye na sifa za kiroho. Jumba linapaswa kugawanywa katika sehemu mbili: sehemu moja kwa ajili ya dada na watoto wao, na pia mabinti, na sehemu nyingine kwa ajili ya ndugu na washiriki wengine wa kiume. Jumba la Ufalme litatumiwa kwa kulala tu. Wote wanapokuwa mahali pa mkusanyiko mchana, kazi ya ulinzi itapangwa kwa zamu ili kuzuia vitu vya ndugu visiibwe. Ndugu wenye kujiheshimu, wenye sifa za kiroho, ndio wanaopaswa kutumiwa ili kufanya kazi ya ulinzi. Haitaruhusiwa kupikia chakula ndani ya Jumba la Ufalme. Kibanda cha muda kinaweza kujengwa katika uwanja, ili kitumiwe kuwa mahali pa kupikia muda wa mkusanyiko tu. Mwishoni mwa mkusanyiko, kibanda hicho kitabomolewa. Ni jambo la maana kwamba Jumba la Ufalme na vilevile uwanja, vilindwe katika hali ya usafi na utaratibu. Inafaa kuwa waangalifu ili kitu chochote kisiharibiwe. Wale wanaokaa katika Jumba la Ufalme watafanya yote wawezayo ili waonyeshe mwenendo unaostahili Wakristo wa kweli, kati yao wenyewe na vilevile kuelekea majirani.—1 Kor. 10:31.
7. Ni nini tunalopaswa kuhangaikia kwanza tunapojitayarisha kwa ajili ya Mkusanyiko wa Wilaya wa 2009, na tunapouhuzuria?
7 Matendo Yanayomletea Mungu Utukufu: Tunapoonyesha matunda ya roho katika utendaji wetu wote, kwa kuangalia zaidi sana namna yetu ya kusema na kujiendesha tunapokuwa pamoja na wengine katika mji wa mkusanyiko, tunahakikisha zaidi kwamba watu wa Yehova wana mwenendo mzuri na tunaepuka kuwakwaza wengine. (1 Kor. 10:31; 2 Kor. 6:3, 4) Katika njia hizo, na tumtukuze Mungu kupitia mwenendo wetu na kuhuzuria kwetu mkusanyiko wa wilaya wa 2009!—1 Pet. 2:12.
[Kisanduku Kwenye Ukurasa wa 3]
Programu:
――
Siku ya Ine
(Inahusu Mkusanyiko wa Kimataifa tu)
7:20 - 10:55 kisha midi
Siku ya Tano na Siku ya Posho
3:20 asubuhi - 10:55 kisha midi
Siku ya Yenga
3:20 asubuhi - 10:00 kisha midi
[Kisanduku Kwenye Ukurasa wa 4]
Mambo Fulani ya Kufikiria Unapotazamia Kuhuzuria Mkusanyiko wa Wilaya:
1 Ikiwa unaombwa kufanya safari ndefu ili kuhuzuria mkusanyiko, hivyo basi, anza kuchunga feza mapema zaidi iwezekanavyo ili uweze kupata feza za kutosha zitakazokusaidia kusafiri na kuwa na chakula kwa ajili yako mwenyewe na familia yako.
2 Fikiria pia kutegemeza mipango ya mkusanyiko kupitia zawadi zako za kujipendea. ‘Mtu yeyote asionekane mbele za Yehova mikono mitupu,’ lakini ‘Mheshimu Yehova kwa vitu vyako vyenye samani.’—Kum. 16:16; Met. 3:9.
3 Wakati wa mkusanyiko, tunatukuza jina la Yehova kupitia mwenendo wetu mzuri na mavazi yetu safi na yenye heshima.—1 Kor. 10:31.
4 Kusudia kuunga mkono ndugu wanaokaribisha watu mahali pa mkusanyiko na ndugu wengine walio na daraka la kulinda utaratibu. Usichungie watu viti, isipokuwa washiriki wa familia yako na wale wanaosafiri pamoja nawe.
5 Ili ufaidike kabisa na kipindi cha kisha midi, tumia tu chakula chepesi wakati wa kupumzika. Chakula kizito kinaweza kuleta usingizi.—Luka 8:18.
6 Usafi unamletea Yehova heshima. Mwishoni mwa kila kipindi, kila mmoja wetu anaweza kutimiza daraka lake ili kuacha mahali pa mkusanyiko pakiwa safi kwa kuokota vikaratasi na uchafu wa aina yoyote na kuutupa katika mahali ao vyombo vilivyotayarishwa kwa kusudi hilo.—1 Pet. 1:15, 16.