“Njia Ya Maisha Anayoikubali Mungu”—Kusanyiko La Wilaya 1998
1 Kila mwaka, waabudu wa Yehova ni wenye furaha wanapofikiria kukutana kwa hesabu kubwa wakati wa makusanyiko ya wilaya. Wanaonyesha hivyo roho iliyotia alama watumishi waaminifu wa Yehova waliofanyiza Israeli la kale ambao waliimba kwa furaha maneno ya Zaburi 122 wakati wa safari yao ya kwenda Yerusalemu ili kumwabudu Yehova. Tunasoma kwenye mstari wa kwanza: “Nilifurahi wakati waliponiambia: ‘Twende kwa nyumba ya [YEHOVA!]’ ” Makusanyiko hayo yanaonyesha pia kwamba maneno ya Isaya 2:2, 3 ni yenye kutimia sasa.
2 Mwaka huu, tuna sababu ya pekee ya kushangilia, kwa kuwa kusanyiko letu litakuwa na hali ya kimataifa itakayotokana na maelfu ya wajumbe kutoka nchi nyingi za dunia ili kuhudhuria kwenye mamia ya makusanyiko makubwa zaidi. Wamishonari wanaopita katika familia zao watakuwako vilevile kwenye hesabu ya kutosha ya makusanyiko. Hivyo, programu itapambwa na mambo yaliyoonwa na ripoti kuhusu mahubiri ya Ufalme katika nchi za kigeni.
3 Pangeni kimbele mambo yenu vizuri ili kuweza kuhudhuria kwenye siku tatu za karamu hiyo nono ya kiroho, tangu wimbo wa kuanza hadi sala ya mwisho. Mtakapochukua mipango kwa ajili ya kuhudhuria kwenye kusanyiko, onyesheni upendo kwa kufikiria wale wanaohitaji msaada, zaidi wale ambao wanapendezwa na ukweli tangu hivi karibuni, ili kwamba wao pia waweko kwenye vipindi vyote. Lingekuwa kati ya mambo ya muhimu zaidi kuchunguza habari zilizo katika nyongeza hii pamoja na watu wanaojifunza Biblia pamoja nanyi na ambao wanapanga kuhudhuria kwenye kusanyiko. (Gal. 6:6, 10) Siku ya Tano na Siku ya Posho, kusanyiko litaanza kwa muziki pa saa 3:30 na litamalizika yapata saa 11. Programu ya Siku ya Yenga asubuhi itaanza pa saa 3:30, na kusanyiko litamalizika yapata saa 10. Habari zifuatazo zitawasaidia katika matayarisho yenu.
4 Bila shaka, makutaniko yaliyo katika maeneo ambamo makusanyiko ya kimataifa yatafanyika tu ndio yatakayoalikwa kuyahudhuria. Ni jambo la lazima kwamba kila mmoja aheshimu mipaka hiyo ili kwamba makusanyiko yote yaweze kupangwa kwa njia yenye utaratibu. Kila kusanyiko litakuwa na hali ya kimataifa itakayoonekana kupitia utoaji wa sehemu fulani za programu na ripoti, na pia kuwako kwa wamishonari.
5 Upangishaji unafanyika kwa kawaida nyumbani kwa watu mmoja mmoja. Tunapaswa kuonyesha shukrani kwa akina ndugu na dada hao wanaokubali kutupangisha. Kwa upande mwingine, lingekuwa jambo lisilokuwa nzuri kwamba wale wanaotolewa ukaribishaji huo waweze kuutumia vibaya na kulazimisha kwamba wapangishwe wakati mrefu kabla au baada ya kusanyiko. Upangishaji unatolewa tu MUDA WA kusanyiko. Wale wanaofaidika na aina hiyo ya upangishaji wanapaswa kuheshimu mali ya yule anayewapangisha, kutoharibu jambo lolote, kutokwenda mahali wasikoalikwa, na kuangalia kwamba watoto wao watende vivyo hivyo. Ikiwa wale wanaowapangisha wanakabiliana na tatizo lolote katika hali hiyo, wanapaswa kujulisha mara moja idara ya upangishaji, itakayofurahi kuwatolea msaada wake.
6 Zijapokuwa ‘nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo’ tunazoishi, tunatumaini kwamba wengi ndio watakaofungua milango yao kwa waombaji wa mahali pa kukaa, kama ilivyokuwa huko Kinshasa au mahali pengine, ndugu zetu walipolazimika kukimbia vita. Ni jambo la kuhuzunisha kusikia kwamba mahali pengi ndugu wanajionyesha kidogo sana kuwa tayari kufanya hivyo kwa ajili ya wakusanyikaji. Hatungetaka bila shaka kwamba magumu ya sasa yatufanye tupunguze upendo wetu wamoja kwa wengine kwa kujizuiza kuwa wakaribishaji-wageni ikiwa tuna uwezo wa kufanya hilo.—Mt. 24:14; Ebr. 13:1, 2; Yn. 13:35.
7 Wahubiri fulani, na vilevile watoto wao, wana mahitaji ya pekee; inatuomba basi tujionyeshe wenye kujali kuwaelekea. Kutaniko kwa ujumla, na wazee kibinafsi, wangepaswa kuangalia kwamba washughulikie watu hao na si kutwika daraka lao kwa idara ya upangishaji ya kusanyiko. Wazee na washiriki wengine wa kutaniko wanaojua hali yao wanaweza kuonyesha upendo kwa kuwatolea msaada unaohitajiwa. Hilo linaomba mara nyingi kwamba wahubiri wahangaikie mahitaji ya watumishi wa wakati wote, watu wazee-wazee, au vilema, nk. Kwa mfano, tunaweza kuwasaidia kwa kuwapeleka au kwa kuwatunza kwa njia mbalimbali—Yak. 2:15-17; 1 Yn 3:17, 18.
8 Wale Watakaohudhuria Kwenye Kusanyiko Lingine: Mara nyingi, kusanyiko mnakoalikwa ni lile lililo karibu zaidi na makao yenu. Hata hivyo, ikiwa kwa sababu yenye kufaa mnapaswa kuhudhuria kwenye kusanyiko lingine, jisikieni huru kufanya hivyo.
9 Ushirikiano Wenu ni wa Lazima: Uendeshaji mzuri na mafanikio ya idara ya upangishaji vinategemea ushirikiano wa kila mmoja. (Ebr. 13:17) Ni kwa sababu hiyo tunaomba kwa wote kushirikiana na idara ya upangishaji iliyowekwa na Sasaiti. Hivyo, tutapunguza kwa kiasi matatizo tunayopambana nayo.
10 Huku tukijitayarisha kuhudhuria kwenye makusanyiko ya wilaya 1998 “Njia ya Maisha Anayoikubali Mungu,” pamoja na ndugu na dada zetu, na tufikirie pia utegemezo wa kimwili na wa kifedha tunaoweza kutoa kwa matayarisho ya karamu hiyo ya kiroho! Kama vile Waisraeli na Wakristo wa kwanza, tusiende huko mikono mitupu.—Kumb. 16:16, 17; 2 Kor. 8:12.
[List of locations on page 4]
MAKUSANYIKO YA WILAYA 1998-1999
JULAI 3-5
KINSHASA (F): KIN-4; KIN-7; KIN-10.
JULAI 10-12
BANDUNDU (LI): B-1; B-10.
BUMBA (LI): E-4; E-12; E-15; E-20; E-22; O-3; Sehemu O-10; O-15.
GOMA (F; SW): KI-2; KI-6; KI-14.
KINSHASA (LI-1): KIN-1; KIN-3; KIN-8; KIN-12; KIN-13; Sehemu BC-3.
LUBUMBASHI (F; SW): Sehemu K-1; K-2; K-13.
TSHIKAPA (F; SH): KA-6; KA-22; KA-23; KA-31.
JULAI 17-19
BUKAVU (F; SW): KI-1; KI-11; KI-12.
GBADOLITE (LI): E-5; E-9; E-19.
KANANGA (F; SH): KA-1; KA-9; KA-14; KA-18; KA-19; KA-28; KA-30.
KINSHASA(LI-2): KIN-2; KIN-5; KIN-6; KIN-9; KIN-11.
LIKASI (F; SW): Sehemu K-1; K-17; K-20; K-23.
NIOKI (LI): B-4; B-6; B-14; B-15.
JULAI 24-26
BUNIA (SW): O-4; O-12.
GEMENA (LI): E-1; E-14.
ILEBO (LI; SH): KA-10; KA-15; Sehemu KA-21; KA-29.
KISANGANI (LI): Sehemu O-1; O-7; Sehemu O-8; Sehemu O-10; Sehemu O-14.
KOLWEZI (F; SW): Sehemu K-1; K-3; Sehemu K-5.
UVIRA (SW): KI-8; Sehemu BU-1.
JULAI 31-AGOSTI 2
BENI (SW): KI-5; KI-10.
BRAZZAVILLE (F; MK): CO-1; CO-5; Sehemu CO-3; Sehemu CO-7; Sehemu CO-8.
BUJUMBURA (RU): Sehemu BU-1; BU-2; BU-3.
KISANGANI (F; SW): Sehemu O-1; O-5; O-9; Sehemu O-14; O-16.
LISALA (LI): E-8; E-11; E-18; E-21.
MATADI (LI): BC-1; BC-5.
SANDOA (DR): Sehemu K-5; K-21.
AGOSTI 7-9
BUTEMBO (SW): KI-7; KI-9.
ISIRO (LI): O-2; Sehemu O-17; O-18.
KIMPESE (LI): BC-2; Sehemu BC-3; BC-4; Sehemu BC-6; BC-7; BC-8.
MBANDAKA (LI): E-2; E-7; E-16; E-17; E-23.
MBUJI-MAYI (F; SH): KA-2; KA-8; KA-16; KA-17; KA-20; Sehemu KA-25.
POINTE-NOIRE (F; MK): CO-2; CO-6; Sehemu CO-8.
AGOSTI 14-16
BUTA (LI): Sehemu O-8; O-11.
DUNGU (LI): O-6; O-13; Sehemu O-17.
KABINDA (F; SH): KA-5; KA-13; Sehemu KA-32.
KINDU (SW): KI-3; KI-13.
MANONO (KU): Sehemu K-10; K-14; Sehemu K-16.
POPOKABAKA (LI): Sehemu BC-6; B-7; Sehemu B-13; Sehemu B-21.
AGOSTI 21-23
BOENDE (LI): E-3; E-6; Sehemu E-13; E-24.
KONGOLO (SW): KI-4; K-22.
LODJA (OT): KA-4; KA-11; KA-12; Sehemu KA-26; KA-27; Sehemu KA-32.
MULONGO (KU): Sehemu K-8; Sehemu K-10; Sehemu K-16.
MWENE DITU (F; SH): KA-3; KA-24; Sehemu KA-25.
OUESSO (F): Sehemu CO-3; Sehemu CO-7.
TEMBO (LI): B-17; Sehemu B-13.
AGOSTI 28-30
BOKUNGU (LI): E-10; Sehemu E-13.
KALEMIE (SW): Sehemu K-12; K-18; K-19.
KAMINA (KU; SW): Sehemu K-4; Sehemu K-6; K-7; K-15.
KENGE (MK): B-3; B-9; Sehemu B-21.
KINKONDJA (KU): Sehemu K-8; K-9; Sehemu K-10; Sehemu K-16.
KOLE (OT): KA-7; Sehemu KA-21; Sehemu KA-26.
SEPTEMBA 4-6
KABONGO (KU): Sehemu K-4; Sehemu K-6; K-24.
KIKWIT (F; MK): B-2; Sehemu B-19; B-24.
KIRUNGU/MOBA (SW): Sehemu K-12; Sehemu K-19.
SEPTEMBA 11-13
BULUNGU (MK): B-5; Sehemu B-19; B-20.
PEPA (SW): K-11; K-25.
SEPTEMBA 18-20
IDIOFA (MK): B-8; B-16.
OKTOBA 2-4
MUKEDI (MK): Sehemu B-18; B-23.
OKTOBA 9-11
GUNGU (MK): B-11; B-12.