Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 2/97 uku. 3-4
  • “Imani Katika Neno La Mungu”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Imani Katika Neno La Mungu”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Julai 11-13 Kinshasa (F, LI-1) KIN-1, KIN-3, KIN-4, KIN-7, KIN-8, KIN-10, KIN-12, KIN-13 Julai 18-20 Kinshasa (LI-2) KIN-2, KIN-5, KIN-6, KIN-9, KIN-11, BZ-3, BZ-6
  • Julai 25-27 Gemena (LI) E-1, E-14
  • Agosti 1-3 Gbadolite (LI) E-5, E-9, E-19
  • Agosti 8-10 Popokabaka (LI) B-7, sehemu ya B-13
  • Agosti 15-17 Bukavu (SW) KI-1, KI-11, KI-12
  • Agosti 22-24 Goma (SW) KI-2, KI-6, KI-14
  • Agosti 29-31 Butembo (SW) KI-7, KI-9
  • Septemba 5-7 Mbuji-Mayi (F, SH) KA-2, KA-8, KA-16, KA-17, KA-20, KA-25
  • Septemba 12-14 Kabinda (SH) KA-5, KA-13
  • Septemba 19-21 Mwene Ditu (SH) KA-3, KA-24
  • “Njia Ya Maisha Anayoikubali Mungu”
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • “Walimu wa neno la Mungu”—Mkusanyiko wa Wilaya 2001 wa Mashahidi wa Yehova
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • “Neno la Unabii la Mungu” Kusanyiko la Wilaya la Mashahidi wa Yehova 1999
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • “Watendaji wa neno la mungu”—mkusanyiko wa wilaya 2000 wa mashahidi wa Yehova
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 2/97 uku. 3-4

“Imani Katika Neno La Mungu”

—Kusanyiko La Wilaya 1997

1 Katika kipindi chetu, Yehova anatumia makusanyiko ya wilaya ya kila mwaka ili kuelimisha watu wake wanaokusanyika na kuwaonjesha undugu wa Kikristo. Makusanyiko ya wilaya 1996 “Wajumbe wa Amani ya Kimungu” katika Zaïre na Congo yalikusanya watu 317,872; ni wengi ndio walioonyesha shukrani yao kwa ajili ya mawazo yenye kuburudisha yaliyotolewa na pia kwa ajili ya faida za ziada kuhusu kuondolewa kwa idara ya chakula zilizowaletea, kama vile shangwe ya kupitisha wakati katika ushirika na akina ndugu na dada zao na kwa kujengana wamoja kwa wengine. Wanafunzi 4,350 wanaoazimia kama wajumbe wa amani ya kimungu walibatizwa kama mfano wa wakfu wao kwa Mungu. Jambo la kwamba tulifaidika na programu yenye kusisimua mwaka jana lingepaswa kutuchochea kufanya bidii yetu yote ili kuhudhuria kwenye makusanyiko ya wilaya 1997 “Imani Katika Neno la Mungu.” Kwa sababu ya matatizo mengi ambayo wanadamu wanakumbana nayo siku zetu, tunataka sote hakika kualika kwenye makusanyiko hayo wale wanaojifunza Biblia pamoja nasi. Kwa kila mmoja wa sisi tunaopenda kumtumikia Yehova kwa imani katika wakati huu wa mwisho, makusanyiko hayo yatatutolea vitia-moyo na nguvu kwa upande wa kiroho.

2 Panga mambo yako vizuri mbele ya wakati ili kuweza kuhudhuria kwenye siku tatu za karamu nono hiyo ya kiroho, tangu wimbo wa kufungua mpaka sala ya kumalizia. Katika hali nyingi, kusanyiko mnaloalikwa kwalo ni lile lililo karibu na makao yenu. Sosaiti ilifanya bidii yote ili kukurahisishia mambo kwa upande huo. Mahali pengi papya pa makusanyiko paliongezeka kwa yale ya mwaka wa nyuma ili kuwezesha kwa kila mmoja wetu kulishwa kiroho pamoja na watu wote wa nyumba yake. (Kumb. 31:12) Huu sasa ndiyo wakati wa kufikiri kwa yale mtakayokuwa na uwezo wa kufanya ili kukusanya fedha za kutosha kwa safari yenu wote. Kwa shukrani kwa bidii iliyofanywa na Sosaiti, tunatazamia kwamba kila mmoja ahudhurie kwenye kusanyiko ambalo mzunguko wake unaalikwa. Hata hivyo, ikiwa kuna sababu ya kweli kwamba unapaswa kuhudhuria kwenye kusanyiko lingine, jisikie huru kufanya hivyo.

3 Utakapochukua mipango ili kuhudhuria kwenye kusanyiko la wilaya, onyesha upendo kwa kufikiria wale wanaohitaji msaada, ni kusema wale wanaopendezwa hivi karibuni na ukweli, ili waweko pia kwenye vipindi vyote. Lingekuwa jambo lenye kufaa kuchunguza maelezo yanayopatikana katika makala hii pamoja na watu wanaojifunza Biblia pamoja nawe na wanaopanga kuhudhuria kwenye kusanyiko. (Gal. 6:​6, 10) Siku ya Tano na Siku ya Posho, kusanyiko litaanza na muziki pa saa 3:30 na litamalizika yapata saa 10:30. Programu ya Siku ya Yenga asubuhi itaanza pa saa 3:​30, na kusanyiko litamalizika yapata saa 11:50. Maelezo yafuatayo yatakusaidia katika kujitayarisha kwako.

4 Watu wanapangishwa kwa ukawaida katika nyumba za watu binafsi. Tunapaswa kuonyesha shukrani kwa akina ndugu na dada wanaokubali kutupangisha. Zaidi ya hilo, halingekuwa jambo nzuri kwa wale wanaokaribishwa namna hiyo kutumia vibaya ukarimu huo na kulazimisha kwamba wapangishwe kwa muda mrefu kabla au kisha kusanyiko. Upangishaji unatolewa tu katika kipindi cha kusanyiko. Wale wanaofaidika na kupangishwa namna hiyo wanapaswa kuheshimu mali ya watu wanaowakaribisha, kutokuharibu kitu chochote, kutokwenda nafasi ambako hawaalikwi, na kuwa wangalifu ili watoto wao watende vivyo hivyo. Ikiwa wenye nyumba wanakabiliana na matatizo fulani kwa upande huo, wanapaswa papo hapo kujulisha idara ya upangishaji, ambayo itafurahi kuwatolea msaada wayo. Kuendesha mambo vizuri na matokeo mazuri ya idara ya upangishaji kunategemea ushirikiano wa kila mmoja. (Ebr. 13:17) Tuliripotiwa kwamba wengine wanaacha kwa makusudi nyumba waliyopewa ili kwenda kwa nyingine ambako labda kuna rafiki au mtu wanayejuana naye. Kufanya hivyo kunatatiza kazi ya ndugu wa idara ya upangishaji. Tunawaomba wote kushirikiana na idara hiyo.

5 Watu wazee-wazee au vilema, watumishi wa wakati wote au wengine wanahitaji labda msaada ili kuhudhuria kwenye kusanyiko. Wale ambao ni watu wa ukoo wao, wazee au washiriki wa kutaniko wanaojua hali yao hasa wanaweza kwa upendo kufanya la lazima, na si kuacha daraka lao kwa akina ndugu wanaoshughulika na kusanyiko.​—Ona 1 Timotheo 5:4.

6 Bila shaka kwamba Yehova anatoa tegemezo lake kwa yale yanayofanyika kwa ajili ya makusanyiko ya kila mwaka. Kwa kuwa hesabu ya kutosha ya ndugu wanaosafiri kwenda kwenye kusanyiko la wilaya wanahitaji kupangishwa, tunaweza kuwa hakika kwamba Yehova atatosheleza kama ifaavyo mahitaji yao. Kwa kuwa maulizo hayo yanahusiana na ibada ya kweli, tungepaswa kufuata kwa shangwe maagizo yanayotolewa. Tuonyeshe kwamba sisi ni waaminifu katika yale yaliyo madogo zaidi sana; tutaweza hivyo kupokea faida nyingi zinazongoja wale ambao Yehova anapenda.​—Lk. 16:10.

7  Isaya 33:20 linasema: “Angalia Sayuni, muji wa makutano yetu!” Tunaweza kufikiria akilini umati mkubwa wenye furaha uliokuwa ukijaza Yerusalemu na uliokuwa ukiitikia kwa hiari amri ya Yehova ya kuwa tu wenye furaha. (Kumb. 16:15) Makusanyiko yetu ya wilaya yanatutolea nafasi ya pekee ya kupokea mafundisho ya kimungu na kufaidika na ushirika wenye thamani wa akina ndugu na dada zetu. Basi Yehova na abariki bidii ambayo mnafanya ili kujitayarisha kuhudhuria kwenye kusanyiko la wilaya 1997 “Imani Katika Neno la Mungu.”

[List of locations on page 4]

MAKUSANYIKO YA WILAYA 1997

TAREHEMAHALIMIZUNGUKO INAYOALIKWA

Julai 11-13 Kinshasa (F, LI-1) KIN-1, KIN-3, KIN-4, KIN-7, KIN-8, KIN-10, KIN-12, KIN-13 Julai 18-20 Kinshasa (LI-2) KIN-2, KIN-5, KIN-6, KIN-9, KIN-11, BZ-3, BZ-6

Brazzaville (F) CO-1, CO-4, CO-5, sehemu ya CO-7, sehemu ya CO-8

Matadi (LI) BZ-1, BZ-5

Mbandaka (LI) E-2, E-7, E-16, E-17, E-23, E-24

Isiro (LI) HZ-2, partie HZ-17, HZ-18

Boende (LI) E-3, E-6, E-13, E-27

Julai 25-27 Gemena (LI) E-1, E-14

Dungu (LI) HZ-6, HZ-13, sehemu ya HZ-17

Kisangani (F, LI) HZ-1, HZ-7, HZ-14

Lisala (LI) E-8, E-11, E-18, E-21

Pointe-Noire (F, MK) CO-2, CO-6, sehemu ya CO-8

Kimpese (LI)BZ-2, BZ-4, BZ-7, BZ-8

Agosti 1-3 Gbadolite (LI) E-5, E-9, E-19

Kisangani (SW) HZ-5, HZ-9, HZ-16

Bandundu (LI) B-1, B-10

Buta (LI) HZ-8, HZ-11

Bumba (LI) E-4, E-12, E-15, E-20, E-22, HZ-3, HZ-10, HZ-15

Ouesso (F) CO-3, sehemu ya CO-7

Agosti 8-10 Popokabaka (LI) B-7, sehemu ya B-13

Lodja (OT) KA-4, sehemu ya KA-11, KA-12, KA-27, KA-32

Mulongo (KU) S-8, sehemu ya S-9, S-10, S-14, S-16

Kindu (SW) KI-3, KI-13

Buja/Uvira (RU, SW) BU-1, BU-2, BU-3, KI-8

Nioki (LI) B-4, B-6, B-14, B-15

Agosti 15-17 Bukavu (SW) KI-1, KI-11, KI-12

Bunia (SW) HZ-4, HZ-12

Kamina (KU, SW) sehemu ya S-7, partie S-9, S-15

Lubumbashi (F, SW) sehemu ya S-1, S-2, S-13

Kole (OT) KA-7, sehemu ya KA-11, sehemu ya KA-21, KA-26

Tembo (LI) B-17, sehemu ya B-13

Agosti 22-24 Goma (SW) KI-2, KI-6, KI-14

Beni (SW) KI-5, KI-10

Likasi (F, SW) sehemu ya S-1, S-17, S-20, S-23

Kime (KU) S-4, S-6, sehemu ya S-7, S-24

Ilebo (LI, SH) KA-10, KA-15, sehemu ya KA-21, KA-29

Kirungu/Moba (SW) S-12, S-18, S-19

Agosti 29-31 Butembo (SW) KI-7, KI-9

Kolwezi (F, SW) sehemu ya S-1, S-3

Pepa (SW) S-11, S-25

Kananga (F, SH) KA-1, KA-9, KA-14, KA-18, KA-19, KA-28, KA-30

Kikwit (F, MK) B-2, B-22, B-24, sehemu ya B-19

Bokungu (LI) E-10, E-25, E-26

Septemba 5-7 Mbuji-Mayi (F, SH) KA-2, KA-8, KA-16, KA-17, KA-20, KA-25

Tshikapa (F, SH) KA-6, KA-22, KA-23, KA-31

Bulungu (MK) B-5, partie B-19, B-20

Septemba 12-14 Kabinda (SH) KA-5, KA-13

Sandoa (DR, SW) S-5, S-21

Idiofa (MK) B-8, B-16, sehemu ya B-18

Septemba 19-21 Mwene Ditu (SH) KA-3, KA-24

Kongolo (SW) KI-4, S-22

Gungu (MK) B-11, B-12, sehemu ya B-18, B-23

Kenge (MK) B-3, B-9, B-21

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine