Kisanduku cha Maulizo
◼ Ni vitabu gani viwili ambavyo tunapaswa kutumia ili kujifunza Biblia na watu wenye kupendezwa?
Kitabu chetu cha kwanza cha kutumia ili kuanzisha na kuongoza mafunzo ya Biblia ni kitabu Biblia Inafundisha. Ijapokuwa si vibaya kutumia kitabu kingine, kama vile trakti yenye kufaa, ili kuanzisha funzo la Biblia, tunapaswa kujikaza kuhamishia funzo hilo haraka iwezekanavyo katika kitabu Biblia Inafundisha. Kutumia kitabu Biblia Inafundisha ili kuanzisha mafunzo kumeleta matokeo mazuri.
Tunapomaliza kujifunza kitabu Biblia Inafundisha, na ikiwa mwanafunzi ni mwenye kufanya maendeleo, hivyo basi tunapaswa kujifunza kitabu Mwabudu Mungu. (Kol. 2:7) Kusudi la kitabu hicho limeelezwa hivi kwenye ukurasa wake wa 2: “Biblia inawahimiza wote wanaompenda Mungu ‘wafahamu kiakili . . . upana na urefu na kina’ cha kweli zake muhimu sana. (Waefeso 3:18) Kitabu hiki kimechapishwa kwa kusudi hilo. Tunatumaini kwamba kitakusaidia kukua kiroho na kukuwezesha kuendelea kutembea kwenye njia nyembamba inayoongoza kwenye uhai katika ulimwengu mpya wa Mungu wenye uadilifu.”
Ikiwa, mbele ya kumaliza vitabu vyote viwili, mwanafunzi anatimiza matakwa yote yanayoombwa ili kubatizwa, funzo linapaswa kuendelea mpaka kumaliza kitabu cha pili. Hata ikiwa mwanafunzi amebatizwa, mhubiri anayeongoza funzo anaweza kuripoti saa, ziara za kurudia, na funzo la Biblia. Mhubiri anayemsindikiza yule mwenye kuongoza funzo na kushiriki katika funzo hilo anaweza pia kuripoti saa.