Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 1/08 uku. 7
  • Kisanduku cha Maulizo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kisanduku cha Maulizo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Jinsi ya Kutumia Kitabu “Upendo wa Mungu” Ili Kuongoza Mafunzo ya Biblia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2009
  • Biblia Inafundisha— Kitabu Chetu cha Lazima cha Kujifunzia Biblia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2006
  • Kisanduku Cha Maulizo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Jinsi Ya Kufanya Wanafunzi Kwa Msaada Wa Kitabu Ujuzi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2008
km 1/08 uku. 7

Kisanduku cha Maulizo

◼ Ni vitabu gani viwili ambavyo tunapaswa kutumia ili kujifunza Biblia na watu wenye kupendezwa?

Kitabu chetu cha kwanza cha kutumia ili kuanzisha na kuongoza mafunzo ya Biblia ni kitabu Biblia Inafundisha. Ijapokuwa si vibaya kutumia kitabu kingine, kama vile trakti yenye kufaa, ili kuanzisha funzo la Biblia, tunapaswa kujikaza kuhamishia funzo hilo haraka iwezekanavyo katika kitabu Biblia Inafundisha. Kutumia kitabu Biblia Inafundisha ili kuanzisha mafunzo kumeleta matokeo mazuri.

Tunapomaliza kujifunza kitabu Biblia Inafundisha, na ikiwa mwanafunzi ni mwenye kufanya maendeleo, hivyo basi tunapaswa kujifunza kitabu Mwabudu Mungu. (Kol. 2:7) Kusudi la kitabu hicho limeelezwa hivi kwenye ukurasa wake wa 2: “Biblia inawahimiza wote wanaompenda Mungu ‘wafahamu kiakili . . . upana na urefu na kina’ cha kweli zake muhimu sana. (Waefeso 3:18) Kitabu hiki kimechapishwa kwa kusudi hilo. Tunatumaini kwamba kitakusaidia kukua kiroho na kukuwezesha kuendelea kutembea kwenye njia nyembamba inayoongoza kwenye uhai katika ulimwengu mpya wa Mungu wenye uadilifu.”

Ikiwa, mbele ya kumaliza vitabu vyote viwili, mwanafunzi anatimiza matakwa yote yanayoombwa ili kubatizwa, funzo linapaswa kuendelea mpaka kumaliza kitabu cha pili. Hata ikiwa mwanafunzi amebatizwa, mhubiri anayeongoza funzo anaweza kuripoti saa, ziara za kurudia, na funzo la Biblia. Mhubiri anayemsindikiza yule mwenye kuongoza funzo na kushiriki katika funzo hilo anaweza pia kuripoti saa.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine