Mambo ya Kukumbuka Kuhusu Ukumbusho
Wazee wanapaswa kufuata kwa uangalifu maagizo yafuatayo wanapotayarisha Ukumbusho:
◼ Muwe waangalifu kwamba mkate na divai visipitishwe mbele ya jua kutua.
◼ Mutafute na kutayarisha mbele ya wakati aina ya mkate unaofaa na divai inayofaa.—Ona Mnara wa Mlinzi wa tarehe 15 mwezi wa 2, 2003, ukurasa wa 14-15.
◼ Sahani, bilauri, meza, na nguo ya meza vyenye kufaa vinapaswa kuletwa kwenye jumba na kupangwa mbele ya wakati.
◼ Jumba la Ufalme ao mahali pengine ambapo mutafanyia mkutano, panapaswa kusafishwa kabisa mbele ya wakati.
◼ Ndugu wakaribishaji na wale watakaopitisha mkate na divai wanapaswa kuchaguliwa na kupewa maagizo mbele ya wakati kuhusu kazi yao, utaratibu wenye kufaa wa kufuata, na umaana wa kuvaa na kujipamba kwa heshima.
◼ Wazee wanapaswa kuchukua mipango ili kumupelekea mkate na divai mtiwa-mafuta yeyote aliye mzaifu kimwili na ambaye hana uwezo wa kuhuzuria.
◼ Ikiwa inapangwa kwamba makutaniko mawili ao zaidi yatumie Jumba la Ufalme lilelile, itaomba makutaniko yatengeneze programu vizuri ili kuepuka msongamano usio wa lazima katika ukumbi ao kwenye mwingilio wa vijia vya watu wote vilivyo karibu na barabara na kwenye mahali pa kuegeshea magari.
◼ Ikiwa munapanga kutumia mahali pengine kuliko Jumba la Ufalme, Muhakikishe kwamba kuna vifaa vya sauti vyenye kufaa ili wasikilizaji wote waweze kumsikiliza msemaji vizuri.