Funzo la Biblia la Pekee na la Familia Ni Utendaji wa Lazima!
1 Kama ilivyokuwa katika karne ya kwanza, Baraza Linaloongoza linahangaikia sana hali njema ya watu wa Yehova. (Mdo. 15:6, 28) Kwa kuwa ziki kubwa inakaribia, ni jambo la maana sana kila mhubiri wa Ufalme awe na urafiki wenye nguvu sana pamoja na Yehova. Namna gani mutatumia wakati ambao hapo mbele ulipangwa kwa ajili ya Funzo la Kitabu la Kutaniko? Wote wanatiwa moyo kutumia wakati huo kwa ajili ya ibada ya familia. Kutumia kwa hekima wakati huo kutatuwezesha kuchimba kabisa ndani ya Neno la Mungu lililoongozwa na roho, na kuchota maji yake yenye kutoa uzima.—Zb. 1:1-3; Rom. 11:33, 34.
2 Ibada ya Magaribi ya Familia: Baba wa familia wanatiwa moyo kutimiza daraka lao mbele ya Yehova ili kuhakikisha kwamba wanafuata programu ya kawaida na ya maana ya funzo la Biblia la familia. (Kum. 6:6, 7) Ndugu ambao hawajaoa na dada ambao hawajaolewa wasio na daraka la kushugulikia familia, wanaweza kutumia wakati huo kwa ajili ya funzo la pekee la Biblia na kufanya utafiti. Ni jambo la maana sisi wote ‘tujinunulie wakati unaofaa’ wa kujifunza na kufikiri sana kuhusu habari tunazojifunza, ili tuendelee kuwa nguvu kiroho kama inavyohitajiwa na hivyo kupambana na ‘siku zenye uovu.’—Efe. 5:15, 16.
3 Habari za Kujifunza: Index des publications de la société Watch Tower ao Watchtower Library inayopatikana kwenye CD-ROM inaweza kuwasaidia kupata habari zitakazofanya vipindi vya funzo viwe vyenye kufurahisha. Familia zinaweza kuzungumzia habari za Mnara wa Mlinzi, kama vile habari zinazotokea kwa ukawaida zenye vichwa: “Siri ya Furaha ya Familia,” “Wafundishe Watoto Wako,” na “Kwa Ajili ya Vijana Wetu.” Pia, Amkeni! ina mfululizo wa habari zenye kichwa “Vijana Huuliza” na habari zenye kuvutia sana kuhusu maajabu ya uumbaji.
4 Usomaji wa Biblia usio wa harakaharaka unaweza kusaidia wote katika familia kukazia akilini na mioyoni mwao kanuni na mafundisho ya Mungu. (Ebr. 4:12) Nyakati nyingine, munaweza kuangalia na kuzungumzia moja ya video zinazotolewa na tengenezo. Mambo mengi yanaweza kufikiriwa ambayo yanaweza kupangwa ili kujifunza. Munaweza pia kuuliza washiriki wa familia watoe maoni yao kuhusu habari ambazo wanapenda mujifunze.
5 Kwa Nini Funzo Ni la Maana Leo: Kufanya hali yetu ya kiroho iwe nguvu kutatutayarisha ‘kusimama imara na kuona wokovu wa Yehova.’ (Kut. 14:13) Wazazi wana lazima ya mwongozo wa Mungu ili kulea watoto wao “katikati ya kizazi kilicho kombo na kilichopotoka.” (Flp. 2:15) Leo, kwenye masomo mwenendo wa watoto wengi ni wenye kuharibika kabisa, watoto wetu wanahitaji msaada ili kushindana na hali hiyo. (Met. 22:3, 6) Watu waliooana wanahitaji kufanya urafiki wao pamoja na Yehova uwe wenye nguvu ili wawe “kamba yenye nyuzi tatu.” (Mhu. 4:12) Hivyo basi, na tutumie kwa hekima wakati unaobaki ili kujijenga wenyewe katika ‘imani yetu iliyo takatifu zaidi’!—Yuda 20.
[Maulizo ya Funzo]
1. Katika siku za leo, ni jambo gani ambalo Baraza Linaloongoza linahangaikia sana kutuhusu, na kwa nini?
2. Namna gani tunaweza kupanga ibada ya magaribi ya familia?
3, 4. Ni mapendekezo gani ambayo tunatolewa kuhusu habari ambazo tunaweza kujifunza na tutakazia nini akilini?
5. Kwa nini funzo la Biblia la pekee na la familia ni utendaji wa maana katika maisha yetu leo?