‘Fanya Mambo Yote kwa Ajili ya Habari Njema’
1. Ni nini ambalo mhubiri wa Ufalme iko tayari kufanya kwa ajili ya wengine, na kwa nini?
1 Mtume Paulo alijisikia kuwa mwenye kulazimishwa kutangazia wengine habari njema. (1 Kor. 9:16, 19, 23) Vivyo hivyo, kuhangaikia hali njema ya milele ya watu kunatuchochea tujikaze sana kuwatangazia habari njema.
2. Tunapohubiri, ni mabadiliko gani tulio tayari kufanya, na kwa nini?
2 Hubiri Mahali na Wakati Ambapo Watu Wanaweza Kupatikana: Mvuvi mzuri wa samaki anatupa ndoani ao wavu wake si wakati na mahali panapompendeza, lakini wakati na mahali ambapo samaki wengi wanaweza kupatikana. Kwa kuwa sisi pia ni “wavuvi wa watu,” tunaweza kuhitaji kubadili programu yetu ili tuwakute watu katika eneo letu, na kwa kufanya hivyo tutafurahia sana kazi hiyo ya pekee ya kukusanya “samaki wa kila aina.” (Mt. 4:19; 13:47) Je, tunaweza kupanga kuhubiri saa za magaribi wakati watu wanapopatikana nyumbani ao saa za asubuhi barabarani? Paulo alikuwa na mradi wa “kutoa ushahidi kamili kuhusu habari njema,” na alitumia nafasi zilizofaa ili kufanya hivyo.—Mdo. 17:17; 20:20, 24.
3, 4. Tunapokuwa katika kazi ya kuhubiri, namna gani tunaweza kufanya mahubiri yetu yapatane na mahitaji ya watu, na tutapata matokeo gani?
3 Mahubiri Yako Yapatane na Mahitaji ya Watu: Mara nyingi wavuvi wa samaki wanabadili namna yao ya kuvua ili wapate samaki wa aina fulani. Namna gani tunaweza kuhubiri habari njema ya Ufalme kwa njia yenye kuvutia watu wa eneo letu? Tunapaswa kutumia hekima ili kuanzisha mazungumzo kuhusu jambo fulani lenye kuhangaisha watu wengi katika eneo na kisha tusikilize kwa uangalifu maoni yao kuhusu jambo hilo. (Yak. 1:19) Tunaweza kuwauliza ulizo lenye kufanya watufunulie maoni yao kuhusu jambo fulani. (Met. 20:5) Kwa kufanya hivyo, tunaweza kufanya utoaji wetu wa habari njema upatane na mahitaji ya watu kwa njia inayogusa maisha yao. Paulo alikuwa “mambo yote kwa watu wa namna zote.” (1 Kor. 9:22) Kufanya mahubiri yetu yapatane na mahitaji ya watu ni kwa lazima sana ili kugusa mioyo yao.
4 Sisi ni wenye furaha sana kuhubiria watu “habari njema za jambo bora”! (Isa. 52:7) Basi, ‘tufanye mambo yote kwa ajili ya habari njema’ ili kuhubiria watu wengi sana iwezekanavyo.—1 Kor. 9:23.