Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 6/13 uku. 1
  • Je, Uko Tayari Kupatanisha Mahubiri Yako na Hali?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Je, Uko Tayari Kupatanisha Mahubiri Yako na Hali?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2013
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ‘Fanya Mambo Yote kwa Ajili ya Habari Njema’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2009
  • Je, Unaweza Kupatanisha Programu Yako na Hali?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2006
  • Onyesha Kupendezwa Kibinafsi na Wengine—Kwa Kuwa Mwenye Kujitayarisha
    Huduma Yetu ya Ufalme—2006
  • Onyesha Kupendezwa Kibinafsi na Wengine—Kwa Kuwa Mwenye Kujipatanisha na Hali
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2013
km 6/13 uku. 1

Je, Uko Tayari Kupatanisha Mahubiri Yako na Hali?

1. Kwa kuwa hali ya ulimwengu inaendelea kubadilika, ni lazima tufanye mabadiliko gani?

1 Katika andiko la 1 Wakorintho 7:31, Biblia inalinganisha hali ya ulimwengu na muchezo unaochezwa kwenye jukwaa ambako tamasha (sehemu mbalimbali za muchezo) zinabadilika-badilika na wachezaji pia. Kwa kuwa hali ya ulimwengu inaendelea kubadilika, mara kwa mara ni lazima tubadilishe njia zetu za kuhubiri, wakati wetu wa kuhubiri, na mambo tunayozungumuzia. Je, uko tayari kupatanisha mahubiri yako na hali?

2. Sababu gani tunapaswa kupatanisha njia zetu za kuhubiri na hali ili tuendelee kutembea pamoja na tengenezo?

2 Njia Zako za Kuhubiri: Sikuzote, kutaniko la Kikristo limepatanisha njia ya kuhubiri na hali. Mwanzoni, wakati Yesu aliwatuma wanafunzi wake, aliwaambia wasichukue mufuko wa chakula ao feza kwa ajili ya mikoba yao. (Mt. 10:9, 10) Hata hivyo, baadaye alibadilisha maagizo hayo kwa sababu ya uadui ambao wanafunzi wake wangepambana nao wakati ujao na pia kwa kuwa kazi ya kuhubiri ilipaswa kupanuka na kufika katika maeneo mengine. (Lu. 22:36) Miaka iliyopita, tengenezo la Yehova lilikuwa likitumia njia mbalimbali za kuhubiri, kwa mufano, kadi za kutoa ushahidi, vipindi vya radio, na motokari zenye vikuza-sauti, kulingana na uhitaji uliokuwa wakati huo. Leo, kwa kuwa katika maeneo mengi ni vigumu kupata watu nyumbani, tumetiwa moyo kuhubiri zaidi mahali pa watu wengi na wakati hatukupanga kufanya hivyo. Pia, tumetiwa moyo kuhubiri nyumba kwa nyumba wakati wa mangaribi, watu wanapotoka kazini. Gari la kimbingu la Yehova linapobadilisha mwendo wake, je, wewe pia unabadilisha mwendo wako na kutembea pamoja nalo?—Eze. 1:20, 21.

3. Namna gani kupatanisha mahubiri yetu na hali ya watu wa eneo letu kunaleta matokeo mazuri?

3 Mambo unayozungumuzia Yako: Katika eneo lenu, ni mambo gani yanayowahangaisha watu? Mambo ya feza? Familia? Vita? Ni vizuri kujua magumu na hali zinazowapata watu wengi katika eneo letu ili tutayarishe mazungumuzo yenye kufaa. (1 Kor. 9:20-23) Wakati musikilizaji anaeleza magumu yake ao hali yake, kuliko kumujibia tu kijuujuu na kuendelea na mambo tuliyotayarisha, ni vizuri zaidi kupatanisha mazungumuzo na hali yake.

4. Sababu gani tunapaswa kupatanisha mahubiri yetu na hali bila kukawia?

4 Hivi karibuni, “tamasha” ya mwisho ya ulimwengu huu itaisha, na ziki kubwa itaanza. ‘Wakati unaobaki umepunguka.’ (1 Kor. 7:29) Kwa hiyo, ni lazima kabisa tupatanishe mahubiri yetu na hali, na kufanya hivyo bila kukawia, ili tutimize mambo mengi katika wakati mufupi unaobaki!

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine