Onyesha Kupendezwa Kibinafsi na Wengine—Kwa Kuwa Mwenye Kujipatanisha na Hali
1 Mtume Paulo aliacha mfano mzuri katika kubadilisha wakati wote utoaji wa habari njema ili upatane na malezi na uwezo wa akili wa wasikilizaji wake. (1 Kor. 9:19-23) Tunapaswa kujitahidi kufanya hivyohivyo. Kwa kufikiria kimbele, tunaweza mara nyingi kufanya utoaji mbalimbali wa kielelezo unaopatikana katika Huduma Yetu ya Ufalme upatane na mahitaji ya watu katika eneo letu. Tunapokaribia mlango, tunaweza kutambua alama zinazoonyesha yale yanayompendeza mwenye nyumba na kutia mambo hayo katika utoaji wetu. Hata hivyo, bado kuna njia nyingine ambayo kupitia hiyo tunaweza kuwa wenye kujipatanisha na hali katika huduma yetu.
2 Habari Yetu Ijengwe juu ya Yale Yanayosemwa na Mwenye Nyumba: Kwa kawaida, tunapotangaza habari njema, tunatokeza ulizo na kuomba wenye nyumba wajibu. Unaonaje jibu hilo? Je, unaelekea kutoa tu shukrani ya juujuu na kuendelea tu na habari uliyotayarisha? Au je, mambo unayosema yanaonyesha kwamba unafikiria maelezo ya wenye nyumba? Ikiwa unapendezwa kikweli na yale ambayo wengine wanasema, unaweza kutumia maulizo ya ziada kwa busara ili kujua kabisa kile kilicho katika akili yao. (Met. 20:5) Ni kwa kufanya hivyo ndipo unaweza kukazia sehemu za ujumbe wa Ufalme zinazozungumzia moja kwa moja mahangaiko ya msikilizaji.
3 Jambo hilo linaomba kwamba tuwe tayari kuzungumzia habari tofauti na zile ambazo tulipanga kuzungumzia hapo mwanzoni. Tukianza na habari kuhusu tatizo fulani linalozungumziwa katika magazeti ya ulimwengu na wakati huohuo mwenye nyumba anatokeza jambo fulani la kibinafsi linalomhusu, tutaonyesha kwamba tunapendezwa naye kikweli ili kushughulikia mahitaji yake, ikiwa tunabadili habari tukikazia mazungumzo ya Biblia juu ya yale yaliyo ya maana zaidi kwake.—Flp. 2:4.
4 Tupatanishe Utoaji Wetu na Hali: Wakati mwenye nyumba anapotokeza ulizo, tunaweza kuona kwamba ni jambo lenye kufaa kuendeleza mazungumzo wakati mwingine baadaye tunapokuwa na uwezekano wa kuchunguza habari za ziada kuhusu jambo hilo. Tunaweza pia kumtolea vichapo vinavyotoa habari kamili kuhusu jambo hilo. Yote hayo yanaonyesha kupendezwa kikweli katika kuwasaidia wengine wapate kumjua Yehova.—2 Kor. 2:17.