Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Kupendezwa na Musikilizaji
Sababu Gani Ni Lazima Kufanya Hivyo: Yesu alipendezwa na watu wakiwa mutu mumoja mumoja, na alihangaikia kila mumoja wao kwa upendo. Kwa mufano, siku moja inawezekana alitambua kwamba mwanaume fulani kiziwi alikuwa na wasiwasi ao haya mbele ya watu wengi, kwa hiyo, alimuponyesha mahali penye hapakuwa na watu. (Mk. 7:31-35) Yesu alionyesha kwamba aliwahangaikia wanafunzi wake; alitambua uwezo wao na hakuwafundisha mambo mengi sana. (Yoh. 16:12) Hata akiwa mbinguni, Yesu anaendelea kupendezwa na watu. (2 Tim. 4:17) Sisi wafuasi wa Kristo, tunapaswa kumuiga. (1 Pet. 2:21; 1 Yoh. 3:16, 18) Pia, tutapata matokeo mazuri katika mahubiri ikiwa tunapendezwa na musikilizaji wetu na ikiwa tunahangaikia hali, mapendezi, na matatizo yake. Atakuwa tayari kutusikiliza ikiwa anatambua kwamba hatukumutembelea tu ili kumutolea ujumbe fulani ao vichapo, lakini, tunapendezwa naye kabisa.
Tumikisha Shauri Hili Katika Mwezi:
Fanya vipindi vya mazoezi wakati wa ibada ya familia ao katika mahubiri ya nyumba kwa nyumba pamoja na ndugu ao dada unayehubiri naye kuhusu namna munaweza kuambatanisha mazungumuzo na jambo ambalo musikilizaji anasema.
Wakati wa mukutano kwa ajili ya mahubiri, ndugu anayeongoza anaweza kuzungumuzia ao kuonyesha njia mbalimbali za kuonyesha kwamba tunapendezwa na watu.