Tujitayarishe Vizuri kwa Ajili ya Ukumbusho
Ni furaha na pendeleo kubwa kwa wafuasi wa Kristo kujitayarisha vizuri kwa ajili ya usiku wa kuazimisha kifo cha Yesu Kristo. (Luka 22:19) Ni mambo gani yenye kufaa tunayopaswa kufanya ili kujitayarisha kwa ajili ya Ukumbusho?
◼ Wakati na Mahali pa Kufanyia Ukumbusho: Kila mutu anapaswa kuelewa vizuri wakati na mahali ambapo Ukumbusho utafanywa. Ikiwa makutaniko mawili ao zaidi yatatumia Jumba la Ufalme lilelile, ni jambo la maana kufika pa wakati na kuondoka bila kukawia na bila msongamano, kwa kuwa hakuna wakati mwingi kati ya mikutano. Ni lazima kuepuka msongamano usio wa lazima kwenye mwingilio, kwenye vijia vya watu wote na mahali pa kuegeshea magari ao kinga.
◼ Vikaratasi vya Mwaliko: Je, wahubiri wote wana vikaratasi vyao vya mwaliko, na wanaelewa mambo yaliyo ndani? Je, umefanya mazoezi kuhusu jinsi ya kuvitolea watu? Ni nani ambaye utatolea kikaratasi cha mwaliko? Tunapaswa kujikaza ili kutolea watu vikaratasi vya mwaliko vyote.
◼ Usafirishaji: Watu fulani wenye kupendezwa na pia ndugu na dada wengine wanaweza kuwa na lazima ya msaada kwa ajili ya usafirishaji ao msaada mwingine. Ni mipango gani ambayo mumefanya ili kushugulikia mahitaji yao?
◼ Mkate na Divai: Muwe waangalifu kwamba mkate na divai visipitishwe mbele ya jua kutua. Mipango itafanywa ili kupelekea mkate na divai mtiwa-mafuta yeyote aliye mzaifu kimwili na ambaye hana uwezo wa kuhuzuria. Mutafute na kutayarisha mbele ya wakati aina ya mkate unaofaa na divai inayofaa.—Ona Mnara wa Mlinzi wa tarehe 15 mwezi wa 2, 2003, ukurasa wa 14-15, fungu 14, 17.
◼ Jumba la Ufalme: Jumba linapaswa kusafishwa kabisa mbele ya wakati. Sahani, bilauri, meza, na nguo ya meza vyenye kufaa vinapaswa kuletwa kwenye jumba na kupangwa mbele ya wakati. Ikiwa munapanga kutumia mahali pengine kuliko Jumba la Ufalme, muhakikishe kwamba kuna vifaa vya sauti vyenye kufaa ili wasikilizaji wote waweze kumsikiliza msemaji vizuri. Ndugu wakaribishaji na wale watakaopitisha mkate na divai wanapaswa kuchaguliwa na kupewa maagizo mbele ya wakati kuhusu kazi yao, utaratibu wa kufuata, na umaana wa kuvaa na kujipamba kwa heshima.
Kwenye tukio hilo la maana zaidi, yaani Ukumbusho wa kifo cha Yesu Kristo, tunataka kujitayarisha vizuri kila mmoja, na hata kutaniko lote nzima. Bila shaka, Yehova atawabariki sana wale wote wanaoonyesha shukrani kutoka moyoni kuhusu yale yote ambayo amewafanyia wanadamu kupitia zabihu ya Mwana wake mpendwa, Yesu Kristo.