Mfululizo wa Habari Mpya Ili Kuanzisha Mafunzo ya Biblia
1. Ni habari gani mpya zitakazopatikana katika toleo la watu wote la Mnara wa Mlinzi, na zina kusudi gani?
1 Kuanzia mwezi ujao, kutakuwa na mfululizo wa habari mpya katika toleo la watu wote la Mnara wa Mlinzi ili kutusaidia kuanzisha mafunzo ya Biblia. Ni yenye kichwa “Jifunze Kutoka Neno la Mungu.” Bila shaka watu fulani katika eneo watafurahia kusoma habari hizo, lakini kwa kweli kusudi la habari hizo ni kuanzisha mazungumzo pamoja na msikilizaji.
2. Habari hizo zitaandikwa namna gani?
2 Namna Habari Hizo Zitakavyoandikwa: Kichwa kikuu na vichwa vidogo-vidogo ni maulizo yatakayotumiwa ili kumuuliza msikilizaji wakati wa mazungumzo. Maandiko ya msingi yanatajwa tu, hayachukuliwe moja kwa moja, ili msikilizaji ajisomee yeye mwenyewe katika Neno la Mungu. Mafungu ni mafupi-mafupi hivi kwamba yanaweza kuchunguzwa mukiwa tu wenye kusimama kwenye mlango. Kila habari ina mawazo yaliyo katika kitabu Biblia Inafundisha ili kumsaidia mhubiri aendeleshe funzo katika kitabu hicho inapofaa.
3. Tunapohubiri nyumba kwa nyumba, namna gani tunaweza kutumia habari hizo ili kuanzisha funzo la Biblia tukiwa tu wenye kusimama kwenye mlango?
3 Namna ya Kuzitumia: Unapomtolea mutu gazeti, umuulize ulizo linaloweza kumchochea ili apendezwe na kichwa kikuu cha habari hizo. Kwa mfano katika gazeti la mwezi wa 1 habari hiyo inazungumzia umaana wa Biblia. Unaweza kuuliza: “Je, unaiona Biblia kama Neno la Mungu ao kama kitabu kizuri tu? [Acha mutu ajibu.] Nina wazo nzuri kuhusu habari hiyo.” Umuonyeshe ulizo la kwanza, soma fungu la kwanza, na soma andiko lililotajwa. Soma ulizo tena, na omba msikilizaji atoe maoni yake kuhusu ulizo hilo. Amua kiasi kinachofaa cha habari mtakayojifunza, mazungumzo yatategemea maulizo yaliyo na namba. Mbele ya kuachana na msikilizaji, elekeza uangalifu wake kwenye ulizo lifuatalo na fanya mipango ya kumurudilia ili kuzungumzia ulizo hilo. Umurudilie ili kuchunguza tena habari zingine kila juma mpaka wakati utakapomletea gazeti lingine. Namna nyingine ni kutumia njia ya moja kwa moja na kuanzisha funzo la Biblia. Kisha tumia habari iliyo katika gazeti ili kuonyesha jinsi funzo linavyofanywa.
4. Namna gani tunaweza kutumia habari hizo tunapowarudilia watu?
4 Pia, unaweza kutumia vizuri habari hizo mpya ili kuzungumza na watu unaopelekea magazeti kwa ukawaida na unaporudilia watu wengine. Unaweza tu kusema: “Kuna jambo jipya katika gazeti Mnara wa Mlinzi. Acha nikuonyeshe jinsi unavyoweza kulitumia.” Tunasali kwamba habari hizo mpya zitasaidia watu wengi zaidi ‘wapate ujuzi sahihi wa kweli.’—1 Tim. 2:4.