Mufululizo wa Habari Mupya Katika Munara wa Mulinzi
Siku ya Posho ya kwanza ya kila mwezi, tumekuwa tukitumia mufululizo wa habari yenye kichwa “Neno la Mungu Linafundisha Nini?” kutoka katika Munara wa Mulinzi ili kuanzisha mafunzo ya Biblia. Kuanzia Mwezi wa 1, mahali pa habari hiyo tutatumia mufululizo wa habari mupya yenye kichwa “Maulizo juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa.” Habari hiyo itakuwa kwenye ukurasa wa mwisho wa Munara wa Mulinzi, gazeti la watu wote. Tunaweza kutumia habari “Maulizo juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa” katika mahubiri kama tulivyotumia habari “Neno la Mungu Linafundisha Nini?” (km 12/10 uku. 2) Kama siku zilizopita, mapendekezo kuhusu namna ya kuanzisha mazungumuzo Siku ya Posho ya kwanza ya mwezi yataendelea kupatikana katika Huduma Yetu ya Ufalme.