Fanya Yako Yote ili Kuanzisha Funzo la Biblia Siku ya Posho ya Kwanza ya Mwezi
Kuanzia Mwezi wa 5, 2011, wahubiri wametiwa moyo waanzishe mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya kwanza ya kila mwezi. Ili kutusaidia kufanya hivyo, habari yenye kichwa “Maulizo juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa” inatolewa kwa ukawaida katika gazeti la watu wote la Munara wa Mulinzi. Ndio sababu, kwenye mukutano kwa ajili ya mahubiri wa Siku ya Posho ya kwanza ya mwezi, munapaswa kukazia namna ambavyo habari hiyo inaweza kutumiwa ili kuanzisha mafunzo ya Biblia; munapaswa pia kufanya onyesho mukitumia habari hiyo.
Wazee wanaweza kuamua kila kikundi kijifanyie mukutano kwa ajili ya mahubiri Siku ya Posho ya kwanza ya mwezi, ao wanaweza kuamua vikundi vyote vikutane pamoja kwa ajili ya mukutano huo siku hiyo, labda kwenye Jumba la Ufalme. Hata hivyo, ikiwa makutaniko mengi yanatumia Jumba la Ufalme, programu hiyo ya pekee ya kuanzisha mafunzo ya Biblia haipaswe kupangwa siku ingine ili tu vikundi vyote viweze kukutana pamoja kwenye Jumba la Ufalme.