Kipindi cha Ukumbusho—Nafasi ya Kuhubiri Zaidi!
1. Tuna sababu gani zinazotufanya tufikirie kuhubiri zaidi katika mwezi wa 3, wa 4, na wa 5?
1 Je, unaweza kuhubiri zaidi katika kipindi cha Ukumbusho kinachokuja? Wakati huo wahubiri fulani wanaofanya kazi na wanafunzi watakuwa katika kipindi cha mapumziko, kwa hiyo wanaweza kutumia nafasi hiyo ili kuhubiri zaidi. Kuanzia tarehe 2 mwezi wa 4, tutakuwa na kampanye ya pekee ya kualika watu wenye kupendezwa ili waje tuhuzurie pamoja Ukumbusho utakaofanyika tarehe 17 mwezi wa 4. Kisha, tutajikaza kuwarudilia wale waliohuzuria Ukumbusho ili kuwasaidia wapendezwe zaidi na kuwaalika waje kuhuzuria hotuba ya pekee itakayotolewa katika juma tokea tarehe 25 mwezi wa 4. Kwa kweli, tuna sababu nyingi zinazotufanya tufikirie kuhubiri zaidi katika mwezi wa 3, wa 4, na wa 5.
2. Ni nini iliyo njia nzuri zaidi inayotutolea nafasi ya kuhubiri zaidi?
2 Tunaweza Kuwa Mapainia Wasaidizi?: Njia nzuri zaidi inayotutolea nafasi ya kuhubiri zaidi ni kuwa painia msaidizi. Kwa kuwa sisi wote tuna mambo mengi ya kufanya, ili kuwa painia msaidizi inaomba kufanya mpango mbele ya wakati na kubadili mambo fulani katika programu yetu. (Met. 21:5) Katika programu yetu ya kawaida, labda mambo yasiyo ya lazima sana tunaweza kuyafanya baadaye. (Flp. 1:9-11) Kwa nini usiwaelezee pia wengine katika kutaniko kwamba una nia ya kuwa painia msaidizi ili kuona ikiwa wanaweza pia kufanya kazi hiyo?
3. Ni mipango gani familia zinaweza kuchukua ili kuhubiri zaidi?
3 Wakati wa Ibada yenu ya Familia ijayo, inaweza kuwa vizuri kuzungumzia miradi muliyo nayo katika familia. (Met. 15:22) Mukiungana mkono, labda watu fulani wa familia wanaweza kuwa mapainia wasaidizi mwezi mmoja ao zaidi. Mutafanya nini ikiwa munaona kwamba haitawezekana? Familia inaweza kufanya mpango ili kuhubiri zaidi saa za mangaribi ao kupitisha saa nyingi katika mahubiri Siku ya Posho na Siku ya Yenga.
4. Tutapata baraka gani ikiwa tunahubiri zaidi katika kipindi cha Ukumbusho kinachokuja?
4 Yehova anaona yote tunayofanya ili kumtumikia na anafurahi tunapojinyima mambo fulani kwa sababu hiyo. (Ebr. 6:10) Tunapata furaha tunapomtolea Yehova na tunapotolea wengine. (1 Nya. 29:9; Mdo. 20:35) Je, tunaweza kuhubiri zaidi katika kipindi cha Ukumbusho kinachokuja ili tupate furaha na baraka nyingi?