Je, Unafaidika Kabisa na Mafundisho Yanayotolewa na Yehova?
1. Ni nini inayoonyesha kwamba Yehova anafurahia kuona watu wakifundishwa?
1 Yehova, ‘Mufundishaji wetu Mukuu,’ anapenda tufundishwe. (Isa. 30:20) Yehova alianza kufundisha baada ya kumwumba Mwana wake muzaliwa wa kwanza. (Yoh. 8:28) Baada ya Adamu kuasi, Yehova hakuacha kufundisha, lakini kwa upendo alifanya mupango wa kuwafundisha wanadamu wasiokamilika.—Isa. 48:17, 18; 2 Tim. 3:14, 15.
2. Ni programu gani ya mafundisho inayoendelea kutolewa leo?
2 Leo, Yehova anaongoza programu kubwa zaidi ya mafundisho katika historia ya wanadamu. Kama Isaya alivyotabiri, mamilioni ya watu ulimwenguni pote wanamiminika kwenye ‘mulima [wa mufano] wa nyumba ya Yehova.’ (Isa. 2:2) Kwa nini wanamiminika huko? Ili kufundishwa njia za Mungu, ndiyo, kufundishwa na Yehova! (Isa. 2:3) Katika mwaka wa utumishi wa 2010, Mashahidi wa Yehova walipitisha zaidi ya saa miliare 1.6 katika kuhubiria watu na kuwafundisha kweli ya Biblia. Pia, kila juma mafundisho ya kiroho yanatolewa katika makutaniko zaidi ya 105,000 ulimwenguni pote, na mutumwa mwaminifu na mwenye busara anachapisha vichapo vya Kikristo vyenye kufundisha watu katika luga zaidi ya 500.
3. Namna gani wewe umefaidika na mafundisho ambayo Yehova anatutolea?
3 Faidika Kabisa na Mafundisho Yanayotolewa na Yehova: Tumefaidika sana na mafundisho ambayo Mungu anatutolea! Tumejifunza kwamba Mungu ana jina na kwamba anatuhangaikia. (Zab. 83:18; 1 Pet. 5:6, 7) Tumepata majibu kwa maulizo fulani ya maana zaidi maishani. Maulizo kama vile kwa nini watu wanateseka na kufa? Namna gani ninaweza kupata furaha ya kweli? Kusudi la maisha ni nini? Pia Yehova ametutolea mafundisho kuhusu mwenendo muzuri unaotuwezesha ‘kuifanikisha njia yetu.’—Yos. 1:8.
4. Ni nafasi fulani gani za kujifunza ambazo watumishi wa Mungu wanaweza kufaidika nazo, na kwa nini tunapaswa kufaidika kabisa na mafundisho yanayotolewa na Yehova?
4 Pia, Yehova anafundisha watumishi wake wengi kwa njia ya kipekee ili kuwasaidia wapanue utumishi wao kwake. Ukurasa wa 4-6 unaonyesha masomo mbalimbali ambayo yamewafaidi wengine kati ya watumishi wake. Hata ikiwa hali zetu za sasa hazituruhusu tupate mazoezi hayo yanayoonyeshwa kwenye kurasa hizo, je, tunafaidika kabisa na mafundisho yanayotolewa na Mungu kulingana na hali zetu? Je, tunawatia moyo vijana, ambao mara nyingi walimu wao wa masomo ao watu wengine wanawachochea kufuatia masomo ya juu ya ulimwengu, wajiwekee miradi ya kiroho na kufuatia mafundisho yanayotolewa na Mungu, mafundisho ya hali ya juu zaidi kuliko yale yanayotolewa na ulimwengu? Kufaidika kabisa na mafundisho yanayotolewa na Yehova kutatusaidia tupate furaha maishani sasa na uzima wa milele wakati ujao.—Zab. 119:105; Yoh. 17:3.
Masomo Mbalimbali Yanayotoa Mazoezi Kupitia Tengenezo la Yehova
Masomo ya Kujifunza Kusoma na Kuandika
• Kusudi: Kufundisha watu kusoma na kuandika ili waweze kusoma na kujifunza Biblia yao wenyewe na kufundisha wengine kweli.
• Muda: Kulingana na uhitaji.
• Mahali: Jumba la Ufalme la mahali penu.
• Ni Nani Wanaoweza Kuhuzuria: Kila muhubiri asiyejua kusoma na kuandika na kila mutu anayependezwa.
• Jinsi ya Kujiandikisha: Wazee wa kutaniko wanapanga masomo ya kujifunza kusoma na kuandika kulingana na uhitaji wa kutaniko lao, na wanatia moyo wale wote wanaoweza kufaidika nayo wahuzurie.
Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi
• Kusudi: Kuzoeza ndugu na dada ili wawe wahubiri na walimu wa habari njema wenye matokeo mazuri.
• Muda: Mazoezi yasiyo na mupaka.
• Mahali: Jumba la Ufalme la mahali penu.
• Ni Nani Wanaoweza Kujiandikisha: Wahubiri wote. Pia, wengine wanaoshirikiana na kutaniko, ambao wanakubali mafundisho ya Biblia, na ambao maisha yao yanapatana na kanuni za Kikristo.
• Jinsi ya Kujiandikisha: Zungumuza na mwangalizi wa Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi katika kutaniko lenu.
Masomo ya Kujifunza Luga ya Kigeni
• Kusudi: Kufundisha wahubiri jinsi ya kuhubiri habari njema katika luga ya kigeni.
• Muda: Miezi ine ao tano. Kwa kawaida masomo yanafanywa kwa saa moja ao mbili kila Siku ya Posho asubuhi.
• Mahali: Kwa kawaida Jumba la Ufalme lililo karibu.
• Ni Nani Wanaoweza Kujiandikisha: Wahubiri wenye sifa nzuri wanaotaka kuhubiri katika luga ya kigeni.
• Jinsi ya Kujiandikisha: Masomo hayo yanapangwa na ofisi ya tawi kulingana na uhitaji.
Ujenzi wa Majumba ya Ufalme
• Kusudi: Kujenga ao kurekebisha Majumba ya Ufalme. Hayo si masomo, lakini kupitia mupango huo wale wanaojitolea wanafundishwa ufundi mbalimbali ili wasaidie katika kazi za ujenzi.
• Muda: Kulingana na hali za mutu mwenye kujitolea.
• Mahali: Mahali popote ambapo Biro ya Ujenzi wa Majumba ya Ufalme inaona kuna uhitaji wa kujenga. Watu fulani kati ya wale wanaojitolea wanaweza kualikwa washiriki katika kazi ya kutoa misaada katika eneo la mbali zaidi lililopatwa na musiba.
• Ni Nani Wanaostahili Kushiriki: Ndugu na dada wenye kubatizwa na wenye kukubaliwa na baraza la wazee. Wanaweza kuwa na ufundi wa ujenzi ao hapana.
• Jinsi ya Kujiandikisha: Kujaza fomu Construction des Salles du Royaume : Questions pour les volontaires (S-82) inayotolewa na wazee wa kutaniko ao katika Congo fomu Demande d’admission dans l’ordre international des serviteurs spéciaux à plein temps Témoins de Jéhovah en tant que serviteurs à la construction des Salles du Royaume (A-12) inayotolewa na ofisi ya tawi.
Masomo ya Mapainia
• Kusudi: Kusaidia mapainia ‘watimize kwa ukamili huduma yao.’—2 Tim. 4:5.
• Muda: Majuma mawili.
• Mahali: Panachaguliwa na ofisi ya tawi; kwa kawaida Jumba la Ufalme lililo karibu.
• Ni Nani Wanaostahili Kuhuzuria: Wale ambao wamefanya upainia wa kawaida kwa karibu mwaka mumoja.
• Jinsi ya Kujiandikisha: Mwangalizi wa muzunguko anaandika mapainia wanaostahili kuhuzuria na kisha anawajulisha.
Masomo ya Wanabeteli Wapya
• Kusudi: Masomo haya yametayarishwa ili kuwasaidia Wanabeteli wapya watimize vizuri utumishi wao wa Beteli.
• Muda: Saa moja kila juma kwa muda wa majuma 16.
• Mahali: Beteli.
• Ni Nani Wanaostahili Kuhuzuria: Wale ambao wamekubaliwa kuwa washiriki wenye kudumu wa familia ya Beteli ao wale wanaojitolea kutumika kwa muda murefu (mwaka mumoja ao zaidi).
• Jinsi ya Kujiandikisha: Wanabeteli wanaostahili kuhuzuria masomo hayo wanaandikishwa na Beteli.
Masomo ya Huduma ya Ufalme
• Kusudi: Kuzoeza wazee na watumishi wa huduma ili washugulikie vizuri madaraka yao ya uangalizi na usimamizi. (Mdo. 20:28) Masomo hayo yanafanywa kisha miaka michache. Ni Baraza Linaloongoza ndilo linaamua.
• Muda: Hivi karibuni masomo hayo yalifanywa kwa muda wa siku moja na nusu kwa ajili ya wazee na siku moja kwa ajili ya watumishi wa huduma.
• Mahali: Kwa kawaida Jumba la Ufalme lililo karibu ao Jumba la Mikusanyiko.
• Ni Nani Wanaostahili Kuhuzuria: Wazee na watumishi wa huduma.
• Jinsi ya Kujiandikisha: Wazee na watumishi wa huduma wanaostahili kuhuzuria wanaalikwa na mwangalizi wa muzunguko.
Masomo ya Wazee wa Kutanikoa
• Kusudi: Kusaidia wazee washugulikie vizuri madaraka yao katika kutaniko.
• Muda: Siku tano.
• Mahali: Panachaguliwa na ofisi ya tawi; kwa kawaida Jumba la Ufalme lililo karibu ao Jumba la Mikusanyiko.
• Ni Nani Wanaostahili Kuhuzuria: Wazee.
• Jinsi ya Kujiandikisha: Wazee wanaostahili kuhuzuria wanaalikwa na ofisi ya tawi.
Masomo ya Waangalizi Wasafiri na Wake zaob
• Kusudi: Kusaidia waangalizi wa muzunguko na waangalizi wa wilaya wawe na matokeo mazuri zaidi katika kutumikia makutaniko na ‘wafanye kazi kwa bidii katika kusema na kufundisha’ na kuchunga vizuri ndugu na dada ambao wanasimamia.—1 Tim. 5:17; 1 Pet. 5:2, 3.
• Muda: Miezi miwili.
• Mahali: Panachaguliwa na ofisi ya tawi.
• Ni Nani Wanaostahili Kuhuzuria: Waangalizi wa muzunguko na waangalizi wa wilaya.
• Jinsi ya Kujiandikisha: Waangalizi wasafiri wanaostahili kuhuzuria wanaalikwa na ofisi ya tawi.
Masomo ya Biblia kwa Ajili ya Ndugu Wasio na Wakec
• Kusudi: Kutayarisha wazee na watumishi wa huduma wasio na wake kwa ajili ya madaraka mengine. Wengi kati ya wale wanaomaliza masomo hayo wanapewa mugawo wa kutumikia mahali ambapo kuna uhitaji mwingi katika inchi yao. Wachache kati yao wanaweza kupewa mugawo katika inchi nyingine ikiwa wanajulisha ofisi ya tawi kwamba wako tayari kutumikia katika inchi nyingine.
• Muda: Miezi miwili.
• Mahali: Panachaguliwa na ofisi ya tawi; kwa kawaida Jumba la Mikusanyiko ao Jumba la Ufalme.
• Ni Nani Wanaostahili Kuhuzuria: Ndugu wasio na wake walio na umri wa miaka kati ya 23 na 62 ambao wana afya nzuri na wanaotaka kutumikia ndugu na kuendeleza kazi ya Ufalme mahali popote palipo na uhitaji. (Marko 10:29, 30) Wanapaswa kuwa wametumika kama wazee ao watumishi wa huduma kwa miaka karibu miwili bila kukatiza.
• Jinsi ya Kujiandikisha: Ikiwa masomo hayo yanafanywa katika eneo la tawi lenu, kuna mukutano unaofanywa kwenye mukusanyiko wa muzunguko kwa ajili ya wale wanaotaka kuhuzuria masomo hayo. Maelezo mengine yanatolewa katika mukutano huo.
Masomo ya Biblia kwa Ajili ya Ndugu na Wake zaod
• Kusudi: Kutolea ndugu na wake zao mazoezi ya pekee ili Yehova na tengenezo lake wawatumie zaidi. Kati ya wale wanaomaliza masomo hayo, wengi wanapewa mugawo wa kutumikia mahali palipo na uhitaji katika inchi yao. Wachache kati yao wanaweza kupewa mugawo katika inchi nyingine ikiwa wanajulisha ofisi ya tawi kwamba wako tayari kutumikia katika inchi nyingine.
• Muda: Miezi miwili.
• Mahali: Kwa sasa, darasa chache za kwanza-kwanza zinafanywa kwenye Kituo Kikubwa cha Mafundisho cha Mashahidi wa Yehova huko Patterson, New York, Amerika. Kisha, masomo hayo yatafanywa mahali mbalimbali patakapochaguliwa na ofisi ya tawi, kwa kawaida Jumba la Mikusanyiko ao Jumba la Ufalme.
• Ni Nani Watakaostahili Kuhuzuria: Ndugu na wake zao walio na miaka kati ya 25 na 50 na wenye afya nzuri ambao hali zao zinawaruhusu kutumikia mahali popote palipo na uhitaji na walio na mwelekeo wa kusema: “Mimi hapa! Nitume mimi.” (Isa. 6:8) Pia, wanapaswa kuwa wameoana kwa miaka karibu miwili na kuwa katika utumishi wa wakati wote kwa miaka karibu miwili bila kukatiza.
• Jinsi ya Kujiandikisha: Ikiwa masomo hayo yanafanywa katika eneo la tawi lenu, mukutano kwa ajili ya wale wanaopendezwa na masomo hayo unafanywa kwenye mukusanyiko wa pekee wa siku moja. Maelezo mengine yanatolewa katika mukutano huo.
Masomo ya Biblia ya Gileadi ya Watchtower
• Kusudi: Kuzoeza mapainia na watumishi wengine wa wakati wote kwa ajili ya kazi ya umisionari.
• Muda: Miezi ine.
• Mahali: Kituo Kikubwa cha Mafundisho cha Mashahidi wa Yehova, huko Patterson, New York, Amerika.
• Ni Nani Wanaostahili Kuhuzuria: Ndugu na wake zao ambao wamebatizwa kwa miaka mitatu na walio na miaka kati ya 21 na 38 wanapojaza fomu ya kwanza. Wanapaswa kujua kusema Kiingereza, kuwa wameoana kwa miaka karibu miwili, na kuwa katika utumishi wa wakati wote kwa karibu miaka miwili bila kukatiza. Wanapaswa kuwa na afya nzuri. Mapainia wanaotumikia katika inchi ya kigeni (pia wale wanaotumika kama misionari); waangalizi wasafiri; Wanabeteli; na wale waliohuzuria Masomo ya Mazoezi ya Kihuduma, Masomo ya Biblia kwa Ajili ya Ndugu Wasio na Wake, na Masomo ya Biblia kwa Ajili ya Ndugu na Wake zao wanaweza pia kujaza ombi ikiwa wanatimiza sifa zinazohitajiwa.
• Jinsi ya Kujiandikisha: Katika tawi fulani, mukutano unafanywa kwenye Mukusanyiko wa Wilaya kwa ajili ya wale wanaopendezwa na masomo hayo. Maelezo mengine kuhusu masomo hayo yanatolewa katika mukutano huo. Ikiwa unataka kuhuzuria masomo hayo lakini mukutano huo haufanywe kwenye mikusanyiko ya wilaya katika inchi yenu, unaweza kuandikia biro ya tawi lenu ili kupata habari zaidi.
Masomo ya Washiriki wa Halmashauri ya Tawi na Wake zao
• Kusudi: Kusaidia washiriki wa Halmashauri ya Tawi washugulikie vizuri zaidi kazi yao ya kusimamia makao ya Beteli, kushugulikia mambo yanayohusu makutaniko, na kusimamia kazi inayofanywa na waangalizi wa muzunguko na wa wilaya katika maeneo yao, na pia kazi ya kutafsiri, kuchapisha, na kusafirisha vichapo na kazi zingine mbalimbali.—Luka 12:48b.
• Muda: Miezi miwili.
• Mahali: Kituo Kikubwa cha Mafundisho cha Mashahidi wa Yehova, huko Patterson, New York, Amerika.
• Ni Nani Wanaostahili Kuhuzuria: Washiriki wa Halmashauri ya Tawi ao Halmashauri ya Inchi ao wengine wanaoweza kupewa migawo hiyo kisha kuhuzuria masomo hayo.
• Jinsi ya Kujiandikisha: Washiriki wa Halmashauri ya Tawi ao wa Halmashauri ya Inchi wanaostahili kuhuzuria masomo hayo pamoja na wake zao wanaalikwa na Baraza Linaloongoza.
[Vielezi-chini]
a Kwa sasa, masomo hayo hayafanyike katika kila inchi.
b Kwa sasa, masomo hayo hayafanyike katika kila inchi.
c Kwa sasa, masomo hayo hayafanyike katika kila inchi.
d Kwa sasa, masomo hayo hayafanyike katika kila inchi.