Ili Mbegu Zikomae Inafaa Kuzimwangia Maji
1. Ni nini inayopaswa kutiliwa maji ili ikomae?
1 Mbegu zenye kupandwa katika shamba zinapaswa kutiliwa maji ili zikomae. Mbegu za ukweli tunazopanda katika mioyo ya watu wa eneo letu zinapaswa pia kutiliwa maji. (1 Kor. 3:6) Ikiwa tunataka watu wafanye maendeleo katika kweli, tunapaswa kuwarudilia, yaani kutilia maji mbegu hizo za mufano tulizopanda katika mioyo yao kwa kutumia Neno la Mungu.
2. Namna gani tunaweza kumutayarisha musikilizaji wetu ili afurahie mazungumuzo tutakapomurudilia?
2 Uliza Ulizo: Unapotayarisha habari utakayotumia katika mahubiri, unaweza pia kutayarisha ulizo lenye kuamusha kupendezwa ambalo utajibu utakapomurudilia mutu fulani uliyemuhubiria. Uliza ulizo hilo mwishoni mwa mazungumuzo yenu ya kwanza, na ufanye mupango wa kumurudilia ili kulijibu. Wahubiri wengi wanachagua habari ao ulizo fulani katika kitabu Biblia Inafundisha ili kuonyesha mutu jinsi funzo la Biblia linavyofanywa.
3. Ni habari gani unazoweza kuandika kuhusu mutu mwenye kupendezwa?
3 Andika Mambo Fulani: Baada tu ya kumuhubiria mutu, andika mambo fulani kuhusu mazungumuzo yenu. Andika jina lake na adresi yake. Pia, ni vizuri kuandika tarehe na saa ambapo ulizungumuza naye, habari mulizozungumuza, na vichapo ulivyomutolea. Je, alisema kwamba yeye ni mwamini wa dini fulani? Je, ana familia? Je, alionyesha mambo fulani yenye kumupendeza ao kumuhangaisha? Mambo kama hayo yatakusaidia kutayarisha habari zilizo za maana kwake ambazo mutazungumuzia utakapomurudilia. Pia, andika siku na saa utakapomurudilia na ulizo mutakalozungumuzia.
4. Kwa nini tunapaswa kuwa wavumilivu tunapowarudilia watu wanaopendezwa na ujumbe wa Biblia?
4 Uwe Muvumilivu: Shetani ataendelea kujikaza sana ili “kuliondoa neno” lililopandwa katika mioyo ya watu. (Marko 4:14, 15) Kwa hiyo, usivunjike moyo ikiwa haumukuti tena nyumbani mutu aliyeonyesha kupendezwa na kweli. Je, unaweza kumutumia barua ao kumwachia barua fupi chini ya mulango? Dada mumoja painia alianza kujifunza na mwanamuke fulani wakiwa wenye kusimama kwenye mulango lakini hakuweza tena kumukuta nyumbani, kwa hiyo akamutumia barua. Mwishowe dada alipomukuta nyumbani, mwanamuke huyo alimwonyesha kwamba aliguswa moyo sana na jinsi alivyomuhangaikia. Tunapotilia maji mbegu za ukweli tunazopanda katika mioyo ya watu, tunaweza kupata furaha tunapowaona wakifanya maendeleo na “kuzaa matunda mara 30 na 60 na 100.”—Marko 4:20.