Njia Tatu ili Kuwa Mwalimu Muzuri
1. Sababu gani tukusudie kufundisha vizuri zaidi?
1 Kila muhubiri ni mwalimu. Tunapomuhubiria mutu kwa mara ya kwanza, tunapomurudilia kwa sababu alipendezwa, ao tunapoongoza funzo la Biblia, kusudi letu ni kumufundisha mutu huyo jambo fulani. Na mambo tunayofundisha ni ya lazima sana. Tunasaidia watu waelewe “maandishi matakatifu” ambayo yanaweza kumufanya mutu awe “mwenye hekima kwa ajili ya wokovu.” (2 Tim. 3:15) Hilo ni pendeleo kubwa kabisa! Kwa hiyo, acheni tuzungumuzie njia tatu zinazoweza kutusaidia tuwe walimu wazuri.
2. Namna gani tunaweza kufundisha kwa njia rahisi?
2 Fundisha kwa Njia Rahisi: Habari fulani tunayofundisha inaweza kuonekana kuwa rahisi kwetu, lakini ngumu kwa mutu asiyejua habari hiyo. Kwa hiyo, unapoongoza funzo la Biblia, epuka kuzungumuzia mambo mengi yasiyo ya lazima. Zungumuzia tu mambo makuu. Mwalimu muzuri haseme sana. (Met. 10:19) Kwa kawaida ni vizuri kusoma tu maandiko ya musingi. Kisha kusoma andiko fulani, kazia tu sehemu ya andiko inayopatana na habari munayozungumuzia. Katika Mahubiri ya Mulimani, kama inavyoonyeshwa kwenye Mathayo sura ya 5 mupaka 7, Yesu alifundisha mambo ya lazima sana, lakini alifundisha mambo hayo kwa njia rahisi, na alitumia maneno machache yenye kuchaguliwa vizuri.
3. Kwa nini tutumie mifano, na mara nyingi ni mifano ya aina gani inayofaa?
3 Tumia Mifano: Mifano inachochea akili ya mwanafunzi, inagusa moyo wake, na inamusaidia aendelee kukumbuka mambo aliyojifunza. Usifikiri kama ili kutoa mufano muzuri ni lazima mufano huo uwe murefu. Mara nyingi Yesu alitoa mifano mifupi, na iliyo wazi. (Mt. 7:3-5; 18:2-4) Kuchora picha kwenye karatasi kunaweza pia kusaidia sana. Kujitayarisha vizuri kutakusaidia ufikirie mifano yenye kugusa moyo.
4. Namna gani tunaweza kutumia maulizo kwa njia yenye kugusa moyo?
4 Uliza Maulizo: Maulizo yanamusaidia mwanafunzi wako afikiri. Kwa hiyo, uwe muvumilivu unapomuuliza ulizo. Ikiwa wewe mwenyewe unatoa jibu mara moja, hautajua kabisa mambo ambayo mwanafunzi wako anaelewa. Ikiwa anajibu vibaya, kuliko kumuambia jibu mara moja, inaweza kuwa vizuri utokeze maulizo madogomadogo yatakayomusaidia apate jibu. (Mt. 17:24-27) Bila shaka, kati yetu hakuna yule aliye mwalimu mukamilifu. Ndiyo sababu, Biblia inatutia moyo tuchunguze kila siku namna tunavyofundisha. Kufanya hivyo kutatuletea faida za milele na kutawaletea pia wale wanaotusikiliza faida za milele.—1 Tim. 4:16.