Mashahidi wa Yehova—Watu Wanaotenda kwa Imani, Sehemu ya 1: Kutoka Katika Giza
Biblia inaonyesha kama nuru inafananisha kweli lakini giza inafananisha uongo. (Zab. 43:3; Isa. 5:20) Shetani alileta giza duniani wakati alimudanganya Eva, na mwishowe akaingiza wanadamu wote katika giza. (Ufu. 12:9) Video Mashahidi wa Yehova—Watu Wanaotenda kwa Imani, Sehemu ya 1: Kutoka Katika Giza inaonyesha namna nuru ya kiroho ilivyoanza kuangaza kutoka katika giza. (Isa. 60:1, 2) Kisha kutazama video hii, je, unaweza kujibu maulizo yafuatayo?
(1) Namna gani giza kubwa lilienea kisha kufa kwa mitume? (2) Kuanzia miaka ya 1100, ni nini kilichowasaidia watu waelewe kama kanisa halikuwa likifundisha kweli? (3) Henry Grew na George Storrs walikuwa nani? (4) Katika maisha ya Charles Russell, ni matukio gani yaliyokuwa na uvutano juu yake? (5) Namna gani ndugu Russell, baba yake, na watu fulani waliojuana nao waliongoza darasa lao la kujifunza Biblia, na walifikia kuchukua maamuzi gani yanayopatana na maandiko? (6) Namna gani kikundi hiki cha wanafunzi wa Biblia kilifikia kujiunga na kikundi cha Nelson Barbour, lakini sababu gani kikundi cha ndugu Russell kilijitenga na kikundi cha Barbour? (7) Ni jambo gani lililotokea katika mwezi wa 7 mwaka wa 1879 ambalo lilianzisha kipindi kipya cha nuru ya kiroho? (8) Kisha hapo, wanafunzi wa Biblia ambao walikuwa wameongezeka walifanya nini ili kueneza habari njema? (9) Miaka mingi mbele, wanafunzi wa Biblia walitazamia nini katika mwaka wa 1914? (10) Wanafunzi wa Biblia walipambana na matatizo gani kisha kifo cha ndugu Russell? (11) Wanafunzi wa Biblia walifanya nini ndugu Rutherford na wenzake walipofunguliwa? (12) Namna gani kutazama video hii kumekusaidia kuelewa vizuri zaidi tengenezo la Yehova na kupendezwa nalo? (13) Namna gani video hii imekufanya uazimie zaidi kuendelea kuhubiri kwa bidii ijapokuwa vizuizi? (14) Namna gani tunaweza kutumia video hii ili kusaidia watu wa jamaa yetu, wale tunaojifunza pamoja nao Biblia, na watu wengine?
Wanafunzi wa Biblia wa zamani walituachia uriti wa kiroho wa maana kabisa! Katika ulimwengu wenye giza la kiroho, walikuwa wachukuaji wa nuru hodari na wenye bidii. Acheni basi tuwaige na ‘tuendelee kutembea kama watoto wa nuru.’—Efe. 5:8.