Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Kwa Ajili ya Kampanye ya Kuwaalika Watu Kwenye Ukumbusho
“Tunafika hapa ili kutolea familia yako mwaliko huu kwa ajili ya tukio la maana linalofanywa ulimwenguni pote kila mwaka. Mwaka huu litafanywa tarehe 26 Mwezi wa 3. Ni Ukumbusho wa kifo cha Yesu. Hotuba yenye kutegemea Biblia itatolewa, na itazungumuzia namna tunavyofaidika na kifo cha Yesu. Kuingia ni bila malipo. Mwaliko huu unaonyesha saa na mahali ambapo mukutano huo utafanyika katika eneo letu.”
Munara wa Mulinzi 01/03/13
“Watu fulani wameuliza ulizo hili, ‘Tunajua namna gani kwamba Yesu alifufuliwa kabisa?’ Je, umekwisha kujiuliza ulizo hilo? [Acha mutu ajibu.] Ona sababu gani ni lazima tupate jibu kwa ulizo hilo. [Soma 1 Wakorintho 15:14.] Gazeti hili linaeleza namna tunavyojua kwamba Yesu alifufuliwa kabisa.”
Amkeni! Mwezi wa 3
“Je, unakubaliana nami kwamba tunaishi wakati ambao si rahisi kuwalea watoto? [Acha mutu ajibu.] Wazazi wengi wamepata mashauri mazuri katika Biblia. Kwa mufano, andiko hili limewasaidia baba watafute nafasi za kuwapongeza watoto wao ili kuwasaidia wajikaze tena zaidi. [Soma Wakolosai 3:21.] Habari hii inaonyesha kanuni tano za maana zinazoweza kuwasaidia baba.”