Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Kwa Ajili ya Kampanye ya Kuwaalika Watu Kwenye Ukumbusho
“Tunawaalika watu kwenye tukio moja la maana sana. Duniani kote, watu wengi sana watakutana tarehe 3 Mwezi wa 4 ili kukumbuka kifo cha Yesu Kristo na kusikiliza bila malipo hotuba yenye itazungumuzia faida ambayo kifo hicho kinatuletea. Mwaliko huu unaonyesha saa na mahali pa tukio hilo katika eneo letu.”
Munara wa Mulinzi 01/03/15
“Tarehe 3 Mwezi wa 4, itakuwa siku ya kukumbuka kifo cha Yesu Kristo. Katika eneo letu, watu fulani watakutana ili kukumbuka kifo hicho; hata hivyo, kuna watu wenye hawaamini kama kifo cha Yesu kiko na maana kabisa. Wewe unawaza namna gani? Unawaza kama tunaweza kupata faida kutokana na kifo na ufufuo wa Yesu? [Muache ajibu.] Ona mambo yenye Neno la Mungu linasema juu ya jambo hilo. [Soma 1 Wakorintho 15:22, 26.] Gazeti hili linazungumuzia faida yenye tutapata kutokana na zabihu ya ukombozi ya Yesu, ni kusema wakati unaokuja, hakutakuwa tena kifo.”
Amuka! Mwezi wa 3
“Tunawatembelea watu kwa muda mufupi ili kuwaonyesha toleo mupya la gazeti Amuka! [Muonyeshe kichwa cha gazeti.] Watu wana mawazo tofauti-tofauti juu ya ulizo hili la kwanza: ‘Mungu anakuwaka?’ Kati ya watu wenye wanaamini Mungu na watu wenye hawamuamini, unawaza ni wanani wako na tumaini nzuri juu ya wakati unaokuja? [Muache ajibu.] Ona ahadi ya Mungu yenye inawaletea watu wengi tumaini. [Soma Zaburi 37:10, 11.] Gazeti hili linazungumuzia faida ine za kutafuta kujua kama Mungu anakuwaka.”