Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Ili Kuwatolea watu Mualiko wa Ukumbusho
“Tunawaalika watu kwenye tukio la maana sana. Tarehe 14 Mwezi wa 4, duniani pote watu wengi watakusanyika ili kukumbuka kifo cha Yesu Kristo na kufuata hotuba inayotegemea Biblia itakayoonyesha namna kifo hicho kinatuletea faida. Kwenye mualiko huu utaona mahali na saa ambapo ukumbusho utafanywa katika eneo letu.”
Munara wa Mulinzi 01/04/14
“Tunawatembelea ili kuzungumuza nanyi kwa muda mufupi kuhusu jambo ambalo watu wengi wanafanya. Karibu kila mutu, iwe ni wa dini gani, anasali. Unawaza Mungu anajibu sala, ao unawaza sala zinatusaidia tujisikie tu muzuri na kusahau magumu yetu? [Acha mutu ajibu.] Ona mawazo ya Biblia kuhusu sala. [Soma 1 Yohana 5:14.] Gazeti hili linaeleza namna sala inatusaidia kabisa.”
Amuka! Mwezi wa 4
“Tunawatembelea ili kuwatolea musaada wa Biblia kuhusu tatizo linalowapata watu wengi. Watu wengi wanahangaishwa sana kwa sababu ya hali yao ya maisha hivi kwamba wamefikiria hata kujiua. Wakati mutu anajikuta katika hali kama hiyo, unawaza kabisa anapenda akufe ao anahitaji kitulizo? [Acha mutu ajibu.] Ona ahadi ya Biblia ambayo imewasaidia watu wengi waendelee kuwa na tumaini. [Soma Ufunuo 21:3, 4.] Gazeti hili linazungumuzia mambo matatu yanayoweza kumusaidia mutu aendelee kuwa na hamu ya kuishi hata kama ana matatizo.”