Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Namna ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza ya Mwezi wa 3
“Tunatembelea watu ili kuwaelezea kwa muda mufupi kuhusu tukio la pekee. Tukio hilo ni ukumbusho wa kifo cha Yesu, na utafanywa tarehe 14 Mwezi wa 4. Watu fulani watakumbuka siku hiyo kwa sababu wanaona kifo cha Yesu kuwa cha lazima. Wengine hawaamini kama kifo cha Yesu ni cha lazima. Unawaza kifo cha Yesu ni cha lazima kwako?” Acha mutu ajibu. Umuonyeshe ukurasa wa mwisho wa Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 3, na muzungumuzie habari iliyo chini ya ulizo la kwanza na hata andiko moja. Umutolee magazeti, na upange kumurudilia ili kuzungumuzia ulizo linalofuata.
Munara wa Mulinzi 01/03/14
“Watu wengi wanajiuliza sababu gani Mungu hamalize ukosefu wa haki na mateso katika dunia. Unawaza ni kwa sababu Mungu hatuhangaikie ao ni kwa sababu anapenda watu wateseke? [Acha mutu ajibu. Kisha soma Yohana 3:16.] Hata kama watu wengi wanataja andiko hilo ili kuonyesha kwamba Mungu anatuhangaikia, hawaamini kabisa kwamba kifo cha Yesu kinaweza kuwaletea faida. Gazeti hili linaonyesha namna kifo cha Yesu kitafanya ukosefu wa haki na mateso viishe katika dunia.”
Amuka! Mwezi wa 3
“Tunatembelea watu kwa muda mufupi ili kuwasaidia waelewe muzuri andiko hili la Biblia. [Soma Mwanzo 1:1.] Watu fulani wanaamini kwamba mbingu na dunia viliumbwa, lakini wengine hawaamini jambo hilo. Wewe unawaza nini? [Acha mutu ajibu.] Wengi hawaamini kwamba vitu viliumbwa kwa sababu viongozi wa dini wanafundisha mambo ambayo Biblia haifundishe. Gazeti hili lina mafasirio ya Biblia yaliyo wazi na yenye kutegemeka yanayoonyesha kwamba hapo mwanzo Mungu aliumba mbingu na dunia.”