TUNGO LA MWEZI: “LIHUBIRI NENO, FANYA HIVYO KWA BIDII [KWA HARAKA].”—2 TIM. 4:2.
Tumia Kila Nafasi Inayojitokeza ili Kutangaza Ujumbe wa Ufalme!
1. Mufano wa Daudi unatufundisha nini?
1 Mufalme Daudi hakuruhusu hali ambazo alipambana nazo zimuvunje moyo. Kwa mufano, Daudi alipenda kumujengea Yehova hekalu. Lakini, wakati Yehova alimukataza kufanya hivyo, Daudi alibadilisha mipango yake na alianza kutayarisha vitu ambavyo Sulemani atatumia ili kujenga hekalu. (1 Flm. 8:17-19; 1 Nya. 29:3-9) Kuliko kuhangaishwa na mambo ambayo hangeweza kufanya, Daudi alihangaikia mambo ambayo angeweza kufanya. Namna gani tunaweza kuiga mufano wa Daudi wakati tunatafuta njia za kutangaza ujumbe wa Ufalme?
2. Namna gani tunaweza kujichunguza?
2 Fanya Mambo Ambayo Unaweza: Watu wengi wamerahisisha maisha yao ili wakuwe mapainia wasaidizi ao wa kawaida. (Mt. 6:22) Wewe pia unaweza kufanya hivyo? Ukijichunguza na kusali juu ya hali yako, unaweza kuona kwamba ‘mulango mukubwa unaoongoza kwenye utendaji’ uko wazi kwa ajili yako. Kama ni hivyo, uwe tayari kutumia nafasi hiyo!—1 Kor. 16:8, 9.
3. Hata kama hali zetu hazituruhusu tukuwe mapainia, tunaweza kutumia nafasi gani ili kutoa ushahidi?
3 Utafanya nini ikiwa hali yako haikuruhusu ukuwe painia? Tumia nafasi zingine ambazo zinajitokeza kwako. Kwa mufano, ikiwa kwenye kazi yako unatumika na watu ambao hawako Mashahidi, kwa nini usitumie wakati fulani unaofaa ili kuwahubiria? Ao, ikiwa uko mugonjwa, sababu gani usitumie nafasi hiyo ili kuwahubiria waganga? Kumbuka kwamba mupango umefanywa ili wale ambao hawajiweze kwa sababu wamezeeka sana ao wana matatizo makubwa ya afya, waripoti hata dakika 15, 30, ao 45 kwa mwezi, ikiwa hawana uwezo wa kufanya saa moja. Wakati unaandika ripoti yako ya mahubiri, usisahau kuhesabu pia wakati ambao ulipitisha kwa kuhubiri wakati haukupanga kufanya hivyo, vichapo ambavyo ulitolea watu na pia trakte na mialiko ya Ukumbusho na ya mikusanyiko. Unaweza kushangaa kuona namna muda huo ambao unaonekana kuwa mudogo unaongeza saa zako za mahubiri!
4. Unaazimia kufanya nini?
4 Hata tukuwe na hali gani, tutumie kila nafasi inayojitokeza ili kutangaza habari njema. Kwa kufanya hivyo, tutajionea furaha ambayo inatokana na kujua kwamba tunafanya yetu yote kwa ajili ya Ufalme.—Mk. 14:8; Luka 21:2-4.