Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 2/06 uku. 1
  • Tokeza Nafasi za Kuhubiri

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tokeza Nafasi za Kuhubiri
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2006
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tumsifu Yehova Kila Siku
    Huduma Yetu ya Ufalme—2009
  • Sifuni Yehova kwa Kutoa Ushahidi wa Vivi Hivi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Unaweza Kutoa Ushahidi Wakati Haukupanga Kufanya hivyo!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Tumia Kila Nafasi Inayojitokeza ili Kutangaza Ujumbe wa Ufalme!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2006
km 2/06 uku. 1

Tokeza Nafasi za Kuhubiri

1 Kutaniko la Kikristo linafanyizwa na watu wenye hali tofautitofauti. Hata hivyo, sisi ni wenye kuungana katika azimio letu la kumsifu Yehova. (Zab. 79:13) Ikiwa afya mbaya au hali nyingine ngumu zinafanya iwe vigumu kwetu kushiriki katika kuhubiri habari njema, tunawezaje kutokeza nafasi za kuhubiri?

2 Katika Shughuli za Kila Siku: Katika kushughulika kwake na watu kila siku, Yesu alitumia vizuri nafasi zilizojitokeza ili kutoa ushahidi. Alizungumza na Mathayo, alipokuwa akipitia kwenye ofisi ya kodi, alizungumza na Zakayo, alipokuwa akisafiri, na alizungumza na mwanamke Msamaria, alipokuwa akipumzika. (Mt. 9:9; Luka 19:1-5; Yoh. 4:6-10) Katika shughuli zetu za kila siku, sisi pia tunaweza kubadili maongezi ya kawaida kuwa ushahidi. Kuwa na Biblia tayari, trakti au broshua, kutatuchochea kusema kuhusu tumaini letu.—1 Pet. 3:15.

3 Je, tatizo la kutembea linafanya iwe vigumu kwako kushiriki katika kazi ya nyumba kwa nyumba? Uwe tayari ili kutumia nafasi za kutolea ushahidi wakati wafanyakazi wa hospitali wanapokuja kukuona na wakati watu wengine wanapokujia au wanapowasiliana nawe. (Mdo. 28:30, 31) Ikiwa hali zinakulazimisha kubaki nyumbani, je, umejaribu kutoa ushahidi kwa njia ya simu au ya barua? Dada mmoja kwa ukawaida anaandikia washiriki wa familia yake wasio Mashahidi. Katika barua zake anatia mawazo yenye kutia moyo kutoka katika Biblia na mambo aliyojionea alipokuwa akitoa ushahidi.

4 Kazini au Shuleni: Tamaa yetu ya kumsifu Yehova itatuchochea pia ili tutokeze nafasi za kupanda mbegu za ukweli kazini au shuleni. Mhubiri mmoja mwenye umri wa miaka minane alielezea wanashule wenzake yale aliyosoma katika Amkeni! kuhusu mwezi. Mwalimu wake alipojua mahali alipopata habari hiyo, alianza kukubali kupokea Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Tukiwa kazini, tunaweza tu kutia kitabu Biblia Inafundisha mahali wengine wanapoweza kukiona, hilo linaweza kutokeza maulizo na kututolea nafasi ya kutoa ushahidi.

5 Je, unaweza kufikiria njia mbalimbali za kutokeza nafasi za kuhubiri katika shughuli zako za kila siku? Kwa kutumia vizuri nafasi zinazojitokeza kulingana na hali zetu, na tujitahidi kila siku ili ‘kumtolea Mungu dhabihu ya sifa.’—Ebr. 13:15.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine