Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Munara wa Mulinzi 01/02/15
“Leo, tunatolea kila mutu trakte hii katika eneo. Trakte hii inaonyesha faida ya Biblia. Kamata yako. [Mupatie musikilizaji trakte Una mawazo gani juu ya Biblia?] Watu fulani wanajiuliza ikiwa Biblia ina mashauri ambayo yanaweza kuwasaidia kwenye kazi yao. Sikiliza mawazo ya andiko hili. [Soma Mhubiri 3:13.] Gazeti hili lina mashauri ya Biblia yenye yanaweza kutusaidia kupata furaha kwenye kazi. Utapenda kulisoma?”
Amuka! Mwezi wa 2
“Tunawatembelea watu ili kuwatolea gazeti mupya la Amuka! Linajibia ulizo hili lenye kuvutia. [Umuonyeshe kichwa cha gazeti.] Ningependa kujua mawazo yako kuhusu andiko moja lenye kuwa katika gazeti hili. [Soma Methali 29:11.] Unawaza shauri hili la Biblia lina faida leo? [Acha mutu ajibu.] Gazeti hili linazungumuzia mashauri ine ya Biblia na linaeleza namna tunaweza kufaidika wakati tunayatumia.”