Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Munara wa Mulinzi 01/04
“Leo, tunatolea kila mutu wa eneo trakte hii. [Umupatie musikilizaji trakte Una Mawazo Gani juu ya Biblia? na umuulize maulizo yenye kuwa kwenye ukurasa wa kwanza. Umuonyeshe jibu la Biblia katika 2 Timotheo 3:16, na umutie moyo ajikaze kusoma trakte hiyo.] Watu wengi hawajue kwamba Biblia inajibia muzuri sana maulizo haya. [Umuonyeshe ulizo la kwanza katika habari ya kwanza ya Munara wa Mulinzi.] Gazeti hili linaeleza namna unaweza kupata majibu katika Biblia yako mwenyewe.”
Amuka! Mwezi wa 4
“Leo, tunatembelea watu ili kuzungumuzia mabadiliko yenye watu wanaona katika familia nyingi. Zamani, wazazi walikuwa wanaongoza muzuri watoto wao, lakini leo, katika familia nyingi inaonekana mambo yamebadilika. Unawaza wazazi wa leo wanafundisha adabu watoto wao namna inastahili? [Umuache ajibu.] Kulingana na Biblia, kuwafundisha watoto adabu ni jambo la maana. [Umusomee Methali 29:17.] Gazeti hili linazungumuzia mashauri mazuri yenye Biblia inatoa juu ya kufundisha watoto adabu.”