Kisanduku Cha Maulizo
◼ Muhubiri wa Ufalme anapaswa kutumia sana Internete ili kuhubiri ao kujifunza Biblia na mutu mwenye kuishi katika inchi ingine?
Wahubiri fulani wametumia Internete ili kuanzisha mafunzo ya Biblia katika inchi mwenye kazi yetu imekatazwa ao katika inchi mwenye kuwa wahubiri kidogo. Wakati fulani, wahubiri hao wamepata matokeo mazuri. Lakini, kuna hatari wakati wahubiri wanaandikiana na kuzungumuza pamoja na watu wa inchi ingine kupitia adresi ya Internete. (Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Mwezi 7, 2007 uku. 3.) Hata kama tuko na kusudi la kutolea watu wenye mioyo mizuri ujumbe wa Ufalme, mazungumuzo kama hayo inaweza kumufanya ndugu ao dada fulani akuwe na mashirika mabaya, na hata waasi-imani. (1 Kor. 1:19-25; Kol. 2:8) Zaidi ya hilo, katika inchi mwenye kazi ya Ufalme imetiliwa mipaka ao kukatazwa, mazungumuzo kwa njia ya internete inaweza kuchunguzwa na wakubwa wa inchi hiyo. Mazungumuzo kwa njia hiyo inaweza kutia ndugu na dada wa inchi katika hatari. Kwa hiyo, wahubiri hawapaswe kuenda kwenye Internete ili kutafuta watu wenye kuishi katika inchi ingine juu ya kuwahubiria habari njema.
Ikiwa tunahubiria mugeni mwenye kutoka inchi ingine wakati hatukupanga kufanya hivyo, tusijaribu kufuatia upendezi ikiwa amekwisha kurudia katika inchi yake. Tutafanya hivyo tu ikiwa tunapewa ruhusa na biro ya tawi. Lakini, tunaweza kumuonyesha namna anaweza kutumia adresi yetu ya jw.org ili kupata habari zaidi ao namna anaweza kuita ao kuandikia biro ya tawi yenye kuwa katika inchi yake. Tunaweza pia kumutia moyo aende kwenye Jumba la Ufalme lenye kuwa karibu na mahali kwenye anaishi. Ni kweli kwamba, katika inchi zingine hakuna Majumba ya Ufalme. Ikiwa anapenda Mashahidi wa eneo lake wamutembelee, tunaweza kujaza fomu Tafadhali Fuatia Upendezi (S-43) na kuipatia mwandishi wa kutaniko, mwenye ataituma kupitia adresi yetu ya jw.org. Biro ya tawi yenye inasimamia kazi ya kuhubiri katika inchi ya mutu mwenye kupendezwa, inajua muzuri hali za inchi hiyo na namna ya kumutolea musaada wa kiroho.—OnaHuduma Yetu ya Ufalme ya Mwezi wa 6, 2014, uku. 7, na Huduma Yetu ya Ufalme ya Mwezi wa 11, 2011, uku. 2.
Ikiwa mutu fulani mwenye tulikuwa tunatembelea anahamia katika inchi ingine, ao ikiwa tunajifunza Biblia na mutu wa inchi ingine mwenye tunajuana naye tu kwenye Internete, tunapaswa kufuata maagizo yenye kuzungumuziwa hapo juu. Lakini, tunaweza kuendelea naye mupaka wakati atakutana na wahubiri wa eneo lake. Kwa upande mwingine, ikiwa anaishi katika inchi mwenye kazi yetu imetiliwa mipaka ao imekatazwa, tunapaswa kuwa waangalifu sana wakati tunazungumuzia habari za Biblia kupitia barua, telefone, ao chombo fulani cha kielektroniki.—Mt. 10:16.