Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Uwazoeze Wahubiri Wapya
Sababu Gani Ni Lazima Kufanya Hivyo: Wanafunzi wapya wa Yesu wanapaswa kujifunza kushika “mambo yote” yenye aliamuru, kama vile kuwafundisha wengine kweli ya Biblia. (Mt. 28:19, 20) Wanafunzi wengi wa Biblia wamekuwa na sifa za kustahili ili kupita kwenye Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi, na pengine wamekwisha kuhubiria watu wa familia ao marafiki zao. Kwa hiyo, kadiri wanaendelea kupendezwa na mambo yenye wanajifunza na kujua kwamba Yehova anapenda watu wote wasikie habari njema, hilo linaweza kuwapatia tamaa ya kufanya kazi ya kuhubiri. (Rom. 10:13, 14) Wakati mwanafunzi wa Biblia anafanya maendeleo ya kiroho na kukubaliwa kuwa muhubiri asiyebatizwa, inaomba apate mazoezi mazuri yenye itamusaidia asikuwe na wasiwasi ya kuchukua hatua hiyo ya lazima sana.—Lu. 6:40.
Tumikisha Shauri Hili Katika Mwezi:
Mufanye mahubiri ya nyumba kwa nyumba pamoja na mwanafunzi wako, na uende pamoja naye ili kurudilia watu ao kuongoza funzo la Biblia. Ikiwa hauna mwanafunzi wa kuzoeza, upange kuhubiri pamoja na muhubiri mwenye kuwa na uzoefu kidogo.