MAISHA YA MUKRISTO
Uwazoeze ili Waendelee Kumutumikia Yehova
Kwa kawaida wahubiri wapya wenye tangu mwanzo wanazoezwa muzuri kuhubiri kwa ukawaida na kwa bidii wanakuwa wahubiri wazuri. (Met 22:6; Flp 3:16) Ona namna fulani ya kumusaidia mwanafunzi tangu mwanzo, ili afikie kuwa muhubiri muzuri:
Wakati tu mwanafunzi wako anakubaliwa kuwa muhubiri, anza kumuzoeza. (km 8/15 uku. 1) Umusaidie aelewe kama ni jambo la lazima sana kazi ya kuhubiri ikuwe katika programu yake ya kila juma. (Flp 1:10) Zungumuzia mambo ya muzuri ya eneo lenu. (Flp 4:8) Umutie moyo ahubiri pamoja na musimamizi wa kikundi cha mahubiri na wahubiri wengine ili afaidike na uzoefu wao.—Met 1:5; km 10/12 uku. 6 fu. 3
Kisha mwanafunzi kubatizwa, endelea kumutia moyo na kumuzoeza, zaidi sana kama hayajifunza kitabu “Upendo wa Mungu.”—km 12/13 uku. 7
Wakati unahubiri na muhubiri mupya, tumia njia mwepesi ili kuanzisha mazungumuzo. Kisha kuona namna anaanzisha mazungumuzo, usikose kumupongeza kwa moyo wote. Umutolee mashauri ili kumusaidia kuwa muhubiri muzuri zaidi.—km 5/10 uku. 7