Tutumie Muzuri Sehemu Zenye Kuwa Katika Kitabu Biblia Inafundisha
Wakati mwanafunzi wa Biblia anajifunza mambo yenye Biblia inafundisha kabisa na anayatumikisha, ataendelea kukomaa na kutoa matunda ya kiroho. (Zab. 1:1-3) Tunaweza kusaidia mwanafunzi wetu ili afanye maendeleo kwa kutumia muzuri sehemu fulani zenye kuwa katika kitabu Biblia Inafundisha.
Maulizo ya Utangulizi: Kila sura inaanza na maulizo na majibu ya maulizo hayo yanapatikana katika sura hiyo. Unaweza kumuuliza maulizo hayo ili kumuchochea mwanafunzi apendezwe na mazungumuzo ya siku ingine. Ao, unaweza kumuomba atoe mawazo yake juu ya kila ulizo. Kama hatoe mawazo ya kweli, haiko lazima ukatae mawazo yake. Maelezo yake yatakusaidia utambue mambo yenye unapaswa kukazia sana.—Met. 16:23; 18:13.
Nyongeza: Kama mwanafunzi anaelewa na anakubali mambo yenye mumejifunza, unaweza tu kumutia moyo ajisomee mwenyewe habari ya nyongeza yenye kupatana na mambo hayo. Katika funzo lenye kufuata, unaweza kumuuliza maulizo fulani ili kuhakikisha kama alielewa habari hiyo. Hata hivyo, kama unaona kwamba ni lazima kuchunguza habari hiyo pamoja naye, unapaswa kuchukua wakati fulani wa funzo ili kuzungumuzia nyongeza ao sehemu fulani ya nyongeza hiyo kwa kusoma mafungu na kuuliza maulizo yenye ulitayarisha.
Kisanduku cha Kujikumbusha: Kisanduku cha kujikumbusha chenye kupatikana kwenye mwisho wa kila sura kinatoa mara nyingi majibu ya maulizo ya utangulizi. Unaweza kutumia kisanduku hicho ili kuhakikisha kama mwanafunzi wako ameelewa na kuona kama anaweza kufasiria mawazo makubwa. Musome naye kwa sauti kila jibu na andiko lenye kutegemeza jibu hilo. Kisha, umuombe mwanafunzi wako atumie maandiko hayo ili kufasiria sababu gani jibu hilo ni la kweli.—Mdo. 17:2, 3.