MAISHA YA MUKRISTO
Ni Wakati Gani Nitakuwa pia Painia Musaidizi?
Hekalu lenye Ezekieli aliona linaonyesha kama watu wa Yehova watajitoa kwa kujipendea. Namna gani tunaweza kumutolea Yehova zabihu ya sifa?—Ebr 13:15, 16.
Njia moja ya muzuri ni kuwa painia musaidizi. Mwaka wa utumishi wa 2018 uko na miezi mingi yenye iko na Siku ya Posho tano na Siku ya Yenga tano. Hilo litasaidia sana wale wenye wanahubiri tu Siku ya Posho na Siku ya Yenga kwa sababu kazi yao inawachukua wakati wote. Tena, wahubiri wanaweza kuchagua kuwa mapainia wasaidizi wa saa 30 ao 50 Mwezi wa 3 na wa 4, na mwezi wenye mwangalizi wa muzunguko anatembelea kutaniko.
Tutafanya nini kama hali yetu haituruhusu tukuwe mapainia wasaidizi? Tunaweza kujikaza ili kuhubiri muzuri zaidi ao pengine kuongeza bidii. Hata kama tuko katika hali gani, upendo wetu kwa Yehova utuchochee tujitoe kabisa ili kufanya kazi yake katika mwaka wa utumishi wa 2018!—Hos 14:2.
Namna gani ninaweza kuiga bidii ya dada Sabina Hernández?
MUANGALIE VIDEO KWA MUSAADA WA YEHOVA NINAWEZA KUFANYA MAMBO MENGI, KISHA MUJIBIE MAULIZO HAYA:
Ni nini ilimuchochea dada Sabina afanye mengi katika kazi ya Yehova?
Mufano wa dada Sabina unakutia moyo namna gani?
Katika mwaka wa utumishi wa 2018, unaweza kuwa painia musaidizi mwezi ao miezi gani?