Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb19 Mwezi wa 8 uku. 5
  • Vijana​—Mukuwe “Wenye Bidii Kwa Ajili ya Matendo ya Muzuri”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Vijana​—Mukuwe “Wenye Bidii Kwa Ajili ya Matendo ya Muzuri”
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2019
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Umusifu Yehova kwa Kufanya Kazi ya Upainia
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2020
  • Urekebishaji wa Idadi ya Saa Zinazoombwa kwa Mapainia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Baraka Zinazotokana na
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Tutafute Mapainia Wasaidizi 100,000
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
Ona Habari Zaidi
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2019
mwb19 Mwezi wa 8 uku. 5

MAISHA YA MUKRISTO

Vijana​—Mukuwe “Wenye Bidii Kwa Ajili ya Matendo ya Muzuri”

Katika barua yenye kuongozwa na roho yenye Paulo aliandikia Tito, Paulo alisema kama vijana, kutia ndani Tito, wanapaswa kujikaza kuwa “mufano muzuri wa matendo ya muzuri katika mambo yote.” (Tit 2:6, 7) Mu ileile sura, alionyesha kama watu wa Yehova wamesafishwa ili wakuwe “wenye bidii kwa ajili ya matendo ya muzuri.” (Tit 2:14) Kuhubiri na kufundisha juu ya Ufalme wa Mungu ni kati ya ile matendo ya muzuri. Kama uko kijana, unaweza kutumia nguvu yako ili kufanya upainia musaidizi ao upainia wa kawaida? ​—Mez 20:29.

Kama unapenda kuwa painia, ufanye mipango yenye inaweza kukusaidia ufikie ule muradi. (Lu 14:28-30) Kwa mufano, utafanya nini juu uweze kutimiza mahitaji yako wakati utakuwa unafanya kazi ya upainia? Utafanya nini juu uweze kueneza saa za upainia? Umuombe Yehova akusaidie. (Zb 37:5) Zungumuza na wazazi wako na mapainia wenye uzoefu juu ya mipango yako. Kisha ukamate hatua mbalimbali juu ufikie muradi wako. Kwa kweli, Yehova atabariki bidii yenye unafanya mu kazi yake!

MUANGALIE VIDEO VIJANA WENYE KUMUHESHIMIA YEHOVA, NA KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:

  • Ni magumu gani yenye ndugu na dada fulani walipambana nayo juu watumike kazi ya upainia, na walifanya vile namna gani?

  • Wazazi wanaweza kufanya nini ili kusaidia watoto wao wakuwe mapainia wa kawaida?

  • Juu ya nini ni jambo la maana kukuwa na programu ya kuhubiri?

  • Ndugu na dada katika kutaniko wanaweza kufanya nini ili kusaidia na kutia moyo mapainia?

  • Wale wenye wanafanya kazi ya upainia wanapata baraka gani?

Dada kijana anazungumuza na baba yake kuhusu kazi ya upainia; ndugu kijana mwenye kuwa painia anajiandikia programu; dada kijana mwenye kuwa painia anahubiri pamoja na dada mwingine; dada kijana mwenye kuwa painia anaongoza funzo la Biblia

Ninaweza kufanya nini juu nifikie muradi wa kuwa painia?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine