Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w24 Mwezi wa 5 uku. 26-31
  • Urafiki Wenu wa Kimapenzi Uwasaidie Kukamata Uamuzi Muzuri

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Urafiki Wenu wa Kimapenzi Uwasaidie Kukamata Uamuzi Muzuri
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • URAFIKI WA KIMAPENZI UKO NA KUSUDI GANI
  • MUJIKAZE KUJUANA MUZURI
  • MAMBO INGINE YA KUFIKIRIA
  • NAMNA WENGINE WANAWEZA KUTEGEMEZA WENYE KUWA MU URAFIKI WA KIMAPENZI?
  • Namna ya Kupata Mutu Mwenye Anaweza Kuwa Bibi ao Bwana Muzuri
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Maamuzi Yenye Inaonyesha Kama Tunamutegemea Yehova
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2023
  • Kamata Maamuzi Yenye Itamufurahisha Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Itika Kama Kuko Mambo Yenye Haujue
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
w24 Mwezi wa 5 uku. 26-31

HABARI YA KUJIFUNZA YA 22

WIMBO 127 Ninapaswa Kuwa Mutu wa Namna Gani

Urafiki Wenu wa Kimapenzi Uwasaidie Kukamata Uamuzi Muzuri

‘Mutu wa siri wa ndani ya moyo. . . [ni] mwenye samani kubwa.’—1 PE. 3:4.

WAZO KUBWA

Mambo yenye ndugu na dada wenye wako mu urafiki wa kimapenzi wanaweza kufanya juu waweze kukamata maamuzi yenye hekima, na namna wengine mu kutaniko wanaweza kuwategemeza.

1-2. Watu fulani wanasema nini kuhusu urafiki wa kimapenzi?

URAFIKI wa kimapenzi unaweza kufurahisha. Kama uko mu uhusiano wa kimapenzi, bila shaka unapenda mambo iendelee muzuri. Na kwa watu wengi mambo inapitikanaka muzuri. Tsion,a dada wa mu inchi ya Etiopia anasema hivi: “Kipindi yenye miye na bwana yangu tulikuwa nachumbiana, ni moya kati ya vipindi vya maana sana mu maisha yangu. Tulizungumuzia mambo mazito, lakini kulikuwa pia mambo ya kuchekesha. Nilikuwa mwenye furaha sana wakati nilitambua kama nimepata mutu mwenye ninapenda na mwenye ananipenda.”

2 Lakini, Alessio, ndugu wa mu inchi ya Hollande anasema hivi: “Nilifurahia kujua muzuri bibi yangu wakati tulikuwa nachumbiana. Lakini mu ile kipindi tulipata pia magumu fulani.” Mu hii habari tutazungumuzia magumu yenye inaweza kutokea mu kipindi ya urafiki wa kimapenzi na kanuni fulani za Biblia zenye zinaweza kusaidia ndugu na dada wenye wako nachumbiana ili waweze kukamata maamuzi ya muzuri. Tutaona pia namna wengine mu kutaniko wanaweza kuwategemeza.

URAFIKI WA KIMAPENZI UKO NA KUSUDI GANI

3. Kusudi ya urafiki wa kimapenzi ni nini? (Mezali 20:25)

3 Wakati wa urafiki wa kimapenzi ni wakati wenye kufurahisha, lakini pia ni hatua ya maana yenye inaweza kuongoza ku ndoa. Siku ya ndoa, ndugu na dada wenye kuwa mu uhusiano wa kimapenzi wanafanya naziri mbele ya Yehova kama watapendana na kuheshimiana muda wote wa maisha yao. Mbele ya kufanya naziri yoyote, tunapaswa kufikiria naziri yetu kwa uzito. (Soma Mezali 20:25.) Ni vile pia kuhusu naziri ya ndoa. Urafiki wa kimapenzi unasaidia ndugu na dada wajuane muzuri, na wakamate uamuzi wa muzuri. Ule uamuzi unaweza kuwa kuoana na wakati fulani unaweza kuwa kuvunja urafiki. Kama ndugu na dada wanavunja urafiki wao wa kimapenzi, ile haimaanishe kama wamekosea. Lakini inaonyesha kama ule urafiki ulitimiza kusudi yake, uliwasaidia kujua ikiwa wanaweza kuoana ao hapana.

4. Juu ya nini tunapaswa kuwa na mawazo yenye kufaa juu ya urafiki wa kimapenzi?

4 Juu ya nini ni jambo ya maana tukuwe na mawazo yenye kufaa juu ya urafiki wa kimapenzi? Wakati ndugu ao dada mwenye hayafunga ndoa iko na mawazo yenye kufaa, hatafanya urafiki wa kimapenzi na mutu mwenye hana nia ya kuoana naye. Lakini haiko tu Wakristo wenye hawayafunga ndoa njo wanapaswa kuwa na mawazo yenye kufaa. Siye wote tunapaswa kuwa na mawazo yenye kufaa. Kwa mufano, watu fulani wanawaza kama ikiwa ndugu na dada wako mu uhusiano wa kimapenzi wanapaswa tu kuoana. Ile mawazo inaweza kuwa na matokeo gani juu ya Wakristo wenye hawafunga ndoa? Melissa, dada mwenye hayaolewa wa mu Amerika anasema hivi: “Wakati Wakristo wawili wako nachumbiana, wengine wanatazamia tu kama wanapaswa kuoana. Matokeo ni kama, Wakristo fulani wenye kuwa mu uhusiano wa kimapenzi, wanaendelea na ule uhusiano hata kama wanaona kuwa uhusiano wao hauendelee muzuri. Pia ile inafanya Wakristo fulani waepuke kabisa kuanzisha uhusiano wa kimapenzi. Zile hali zote zinaweza kuleta mahangaiko ya mingi sana.”

MUJIKAZE KUJUANA MUZURI

5-6. Ni mambo gani yenye ndugu ao dada mwenye iko mu uhusiano wa kimapenzi anapaswa kujua juu ya mwingine? (1 Petro 3:4)

5 Kama muko mu urafiki wa kimapenzi, ni nini itawasaidia kujua ikiwa mutaoana ao hapana? Mujikaze kujuana muzuri. Mbele uanzishe urafiki wa kimapenzi, inawezekana ulikuwa ulishajua mambo fulani juu ya ule ndugu ao juu ya ule dada. Lakini sasa uko na nafasi ya kujua “mutu wa siri wa ndani ya moyo.” (Soma 1 Petro 3:4.) Ile inatia ndani kujua mambo mingi juu ya hali yake ya kiroho, utu wake, na mawazo yake. Kisha wakati fulani, unapaswa kuwa na majibu ya hii maulizo: ‘Huyu mutu atakuwa bwana ao bibi muzuri kwangu?’ (Mez. 31:​26, 27, 30; Efe. 5:33; 1 Ti. 5:8) ‘Ninaweza kumupenda na kumuhangaikia vile inastahili, na yeye anaweza kunipenda na kunihangaikia vile inastahili? Kila mumoja wetu iko tayari kuvumilia uzaifu wa mwingine?’b (Ro. 3:23) Kadiri munaendelea kujuana muzuri, mukumbuke kama jambo yenye inaonyesha kama munastahili kuoana, haiko juu munapatana mu kila jambo, lakini juu kila mumoja iko tayari kujipatanisha na hali ya mwingine.

6 Wakati muko nafanya urafiki wa kimapenzi, ni mambo gani ingine yenye unapaswa kujua juu ya mwenzako? Mbele upendo wako kwa ule mutu ukuwe nguvu sana, inaweza kuwa muzuri muzungumuzie mambo fulani ya maana sana sawa vile miradi yake. Lakini munaweza pia kuzungumuzia mambo ya kipekee sawa vile mambo ya afya, makuta, ao mambo fulani ya mubaya yenye ilitokea zamani yenye imekuwa na matokeo juu ya mawazo yake, hisia zake, na tabia yake. Haiko lazima muzungumuzie mambo yote ku mwanzo wa urafiki wa kimapenzi. (Linganisha na Yohana 16:12.) Kama unaona kama hauko tayari kujibia maulizo fulani ya kipekee, uelezee mwenzako. Lakini, ujue kama kisha wakati ule mwenye anaweza kuwa bibi ao bwana yako, atakuwa na lazima ya kujua ile mambo ili akamate uamuzi muzuri. Kwa hiyo, wakati fulani itaomba uzungumuzie waziwazi ile mambo.

7. Ndugu na dada wenye kuwa mu urafiki wa kimapenzi wanaweza kufanya nini juu wajuane muzuri? (Ona pia kisanduku “Wakati Unafanya Urafiki wa Kimapenzi na Mutu Mwenye Anaisha Mbali.”) (Ona pia picha.)

7 Unaweza kufanya nini juu ujue mutu muzuri kabisa? Jambo moya ya maana ya kufanya ni kuzungumuza waziwazi na bila kuficha kitu, kuuliza maulizo, na kusikiliza kwa uangalifu. (Mez. 20:5; Yak. 1:19) Ili kufanya vile, inaweza kuwa muzuri kufanya mambo fulani yenye inawapatia nafasi ya kuzungumuza. Sawa vile kula pamoya, kutembea pamoya mahali pa watu wengi, na kuhubiri pamoya. Munaweza pia kujuana muzuri wakati munapitisha wakati pamoya na marafiki na watu wa familia. Zaidi ya ile, panga kufanya mambo yenye inaweza kukusaidia kujua namna mwenzako anatendaka mu hali tofauti-tofauti na wakati iko na watu tofauti-tofauti. Ona mambo yenye Aschwin, wa mu inchi ya Hollande, alijaribu kufanya. Anasema hivi kuhusu urafiki wake wa kimapenzi pamoya na Alicia: “Tulifanya mambo yenye ingetusaidia kujuana muzuri. Mara mingi ilikuwa mambo ya kawaida, sawa vile kupiga chakula pamoya ao kufanya kazi za ku nyumba pamoya. Wakati tulikuwa tunafanya ile mambo, kila mumoja wetu aliona sifa za muzuri za mwingine na uzaifu wake.”

Picha: 1. Wenye kuchumbiana wako nazungumuza kwa furaha wakati wanaikala fasi ya kunywia café. 2. Wengine wenye kuchumbiana wako natayarisha chakula pamoya wakati wa kujifurahisha. 3. Ndugu na dada wako nazungumuza kupitia vidéoconférence. Wako najifunza habari “Nitazamie Nini Katika Ndoa?​​—Sehemu ya 1” ku jw.org. Ndugu iko Biblia yenye kuwa wazi mbele yake.

Ikiwa munafanya mambo yenye inawapatia nafasi ya kuzungumuza, inawezekana mujuane muzuri (Ona fungu ya 7-8)


Wakati Unafanya Urafiki wa Kimapenzi na Mutu Mwenye Anaisha Mbali

Kama uko nafanya urafiki wa kimapenzi na mutu mwenye iko mbali, unaweza kutumikisha mapendekezo mingi yenye kuwa mu hii habari wakati muko nazungumuza ku telefone ao kupitia vidéoconférence. Munapaswa kuzungumuza waziwazi na kusikiliza kwa uangalifu. Lakini inaweza kuwa nguvu kujua mambo fulani juu ya mwingine bila kupitisha wakati pamoya. Kwa hiyo, mutembeleane wakati inawezekana. Kuko pia mambo ingine yenye munapaswa kufikiria. Kwa mufano, uko tayari kuhama ao pengine kujipatanisha na desturi ao kujifunza luga ya mupya. Uko na makuta ya kukusaidia kusafiri ili kuenda kuona muchumba wako wakati muko nachumbiana, na ya kutembelea marafiki na watu wa familia kisha ndoa?—Lu. 14:28.

8. Namna gani kujifunza pamoya kunaweza kusaidia wale wenye kuwa mu urafiki wa kimapenzi?

8 Kujifunza pamoya mambo ya kiroho kunaweza pia kuwasaidia kujuana muzuri. Kama munaoana, itakuwa lazima mupange wakati wa kufanya ibada ya familia juu muweze kutia Mungu pa nafasi ya kwanza mu ndoa yenu. (Mez. 4:12) Hamuone kama ni muzuri mupange wakati wa kujifunza pamoya tangu sasa, wakati mungali mu urafiki wa kimapenzi? Ni kweli kama wale wenye wako mu urafiki wa kimapenzi hawayakuwa familia, na ndugu hayakuwa kichwa cha dada. Hata vile kujifunza pamoya kunaweza kusaidia kila mumoja wenu ajue hali ya kiroho ya mwingine. Max na Lyasa bibi na bwana wa mu Amerika, waliona faida ingine ya kufanya vile. Max anasema hivi: “Ku mwanzo tu wa urafiki wetu wa kimapenzi tulianza kuzungumuzia vichapo vyenye vilikuwa na habari sawa vile kufanya urafiki wa kimapenzi, ndoa, na maisha ya familia. Vile vichapo vilitusaidia kuzungumuzia mambo ya maana yenye hatungeweza kuzungumuzia siye wenyewe.”

MAMBO INGINE YA KUFIKIRIA

9. Wale wenye kuwa mu uhusiano wa kimapenzi wanapaswa kufikiria nini wakati wako naamua ni nani wataambia kuhusu uhusiano wao?

9 Munapaswa kuambia nani kuhusu uhusiano wenu? Nyie njo mutaamua. Ku mwanzo-mwanzo wa uhusiano wenu, ni muzuri muambie tu watu kidogo. (Mez. 17:27) Kama munafanya vile mutaepuka maulizo mingi kuhusu uhusiano wenu, na hamutajisikia kuwa munakazwa kukamata uamuzi. Lakini kama hamuambie mutu munaweza kuangukia mu mutego wa kujitenga juu munaogopa kama wengine watajua. Ile inaweza kuwa hatari. Kwa hiyo ni jambo ya hekima kuambia watu fulani wenye wanaweza kuwatolea mashauri ya muzuri na kuwasaidia mu njia mbalimbali. (Mez. 15:22) Kwa mufano, munaweza kuambia watu fulani wa familia yenu, marafiki wenye kukomaa kiroho, ao wazee wa kutaniko.

10. Wenye wako mu uhusiano wa kimapenzi wanaweza kufanya nini juu uhusiano wao umuletee Yehova sifa? (Mezali 22:3)

10 Munaweza kufanya nini ili urafiki wenu umuletee Yehova sifa? Kadiri urafiki wenu utaendelea kukomaa, ni vile kila mumoja wenu atavutiwa zaidi na mwenzake. Nini njo inaweza kuwasaidia muendelee kuwa na mwenendo safi? (1 Ko. 6:18) Muepuke mazungumuzo machafu, kupitisha wakati nyie wawili tu, na kunywa sana. (Efe. 5:3) Ile mambo inaweza kuamusha tamaa zenu za ngono na kufanya ikuwe nguvu kwenu kutii kanuni za Yehova. Hamuone kama itakuwa muzuri mukuwe nazungumuzia mipaka yenye munapaswa kukamata ili uhusiano wenu umuletee Yehova sifa? (Soma Mezali 22:3.) Ona mambo yenye ilisaidia Dawit na Almaz wa mu inchi ya Etiopia. Wanasema hivi: “Tulikuwa napitisha wakati pamoya fasi kwenye kulikuwa watu wengi ao pamoya na marafiki. Hakuna siku tulikuwa siye peke mu gari ao mu nyumba. Ile ilifanya tuepuke hali zenye zingeweza kututia mu jaribu.”

11. Ni mambo gani wenye kuwa mu urafiki wa kimapenzi wanapaswa kufikiria wakati wako naamua namna ya kuonyeshana upendo?

11 Tuseme nini juu ya kuonyeshana upendo? Kadiri upendo wenu unaendelea kukomaa, haiko mubaya kuonyesha upendo mu njia fulani zenye kufaa. Lakini kama tamaa yako ya ngono inakuwa nguvu sana, itakuwa nguvu sana kwako kukamata uamuzi muzuri. (Wim. 1:2; 2:6) Pia wakati muko naonyeshana upendo, inaweza kuwa mwepesi kukosa kujizuia na kufanya jambo fulani yenye haitamufurahisha Yehova. (Mez. 6:27) Kwa hiyo, ku mwanzo wa uhusiano wenu, muzungumuzie mipaka yenye mutaheshimia yenye kupatana na kanuni za Biblia.c (1 Te. 4:​3-7) Mujiulize hivi: ‘Kwenye tunaishi watu wataona namna gani matendo yetu ya kuonyeshana upendo? Hii matendo inaweza kuamusha tamaa ya ngono kwa mumoja wetu?’

12. Wale wenye kuwa mu urafiki wa kimapenzi wanapaswa kujua nini kuhusu matatizo ya kukosa kuelewana?

12 Namna gani munaweza kushugulikia matatizo na hali ya kukosa kuelewana? Mutafanya nini kama hamuelewane mara kwa mara? Ile inaonyesha kama hamustahili kuoana? Hatuwezi kusema vile kwa uhakika, juu wakati fulani bibi na bwana hawaelewanake. Ndoa yenye furaha inafanyizwa na watu wawili wenye wako na uwezo wa kutumika pamoya ili kumaliza matatizo yao ya kukosa kuelewana. Kwa hiyo, namna munashugulikia matatizo leo, inaweza kuonyesha ikiwa mutakuwa na ndoa yenye furaha. Mujiulize hivi: ‘Tunaweza kuzungumuzia mambo kwa utulivu na kwa heshima? Kila mumoja wetu anakuwaka tayari kukubali makosa yake na kujikaza kubadilika? Inakuwaka mwepesi kwetu kuacha kushikilia mawazo yetu, kuomba musamaha, na kusamehe?’ (Efe. 4:​31, 32) Lakini, kama mara kwa mara hamuelewane ao munazoea kubishana wakati muko mu urafiki wa kimapenzi, inawezekana mambo haitabadilika wakati mutaoana. Ikiwa unatambua kama ule ndugu ao ule dada hatakuwa bibi ao bwana muzuri kwako, kuvunja urafiki wa kimapenzi njo inaweza kuwa uamuzi muzuri zaidi kwenu.d

13. Ni nini inaweza kusaidia wale wenye kuwa mu urafiki wa kimapenzi kuamua muda wenye uhusiano wao utakamata?

13 Urafiki wenu wa kimapenzi unapaswa kuwa na urefu gani? Kukamata maamuzi haraka-haraka kunaletaka matokeo ya mubaya. (Mez. 21:5) Kwa hiyo, uhusiano wa kimapenzi unapaswa kukamata wakati wa kutosha ili mujuane muzuri. Lakini haupaswe kuwa murefu sana bila sababu. Biblia inasema hivi: “Tazamio lenye kucheleweshwa linafanya moyo ugonjwe.” (Mez. 13:12) Zaidi ya ile, kadiri munapitisha wakati mingi pamoya, inaweza kuwa nguvu kuzuia tamaa yenu ya ngono. (1 Ko. 7:9) Kuliko kukazia akili muda wenye mumefanya mu uhusiano wenu wa kimapenzi, ujiulize hivi: ‘Ni mambo gani ingine yenye ni lazima nijue juu ya mwenzangu ili niweze kukamata uamuzi?’

NAMNA WENGINE WANAWEZA KUTEGEMEZA WENYE KUWA MU URAFIKI WA KIMAPENZI?

14. Tunaweza kutegemeza wale wenye kuwa mu uhusiano wa kimapenzi mu njia gani ingine? (Ona pia picha.)

14 Kama tunajua ndugu na dada wenye wako mu uhusiano wa kimapenzi, tunaweza kuwasaidia namna gani? Tunaweza kuwaalika ili tutumie chakula pamoya, tunaweza kuwaalika mu ibada yetu ya familia, ao ili kujifurahisha pamoya. (Ro. 12:13) Mu hali za vile wanaweza kujuana muzuri zaidi. Wako na lazima ya mutu wa kuwasindikiza? Wako na lazima ya mutu wa kuwabeba mu gari? Ao wako na lazima ya fasi kwenye wanaweza kuzungumuza bila kusumbuliwa? Kama ni vile, unaweza kuwasaidia? (Gal. 6:10) Alicia mwenye tulishazungumuzia anakumbuka mambo yenye yeye na Aschwin walifurahia. Anasema hivi: “Tuliguswa moyo sana wakati ndugu fulani walisema kama tunaweza kuwatembelea ikiwa tuko na lazima ya fasi ili tupitishe wakati pamoya bila kuwa peke yetu.” Ikiwa wenye kuchumbiana wanakuomba uwasindikize, ona ile kuwa pendeleo. Lakini ukuwe pia na utambuzi ili usiwabane-bane sana wakati wako na lazima ya kuongea mambo yao ya kipekee.—Flp. 2:4.

Wenye kuchumbiana wanaikala pamoya wakati wa kujifurahisha. Wako nazungumuza wao wawili tu.

Kama tunajua ndugu na dada wenye kuwa mu uhusiano wa kimapenzi, tunaweza kutafuta njia za kuwategemeza (Ona fungu ya 14-15)


15. Marafiki wanaweza kufanya nini ingine ili kusaidia wenye kuwa mu urafiki wa kimapenzi? (Mezali 12:18)

15 Tunaweza pia kutegemeza wenye kuwa mu uhusiano wa kimapenzi kwa kusema mambo fulani ao kwa kuepuka kusema mambo fulani. (Soma Mezali 12:18.) Kwa mufano, tunaweza kupenda kuambia wengine kama fulani na fulani wako nachumbiana. Lakini pengine wangependa kuelezea wengine ile habari wao wenyewe. Hatupaswe kusema-sema mubaya wenye kuchumbiana ao kuwachambua juu ya mambo yao ya kipekee. (Mez. 20:19; Ro. 14:10; 1 Te. 4:11) Zaidi ya ile, hawatafurahia maneno ao maulizo yenye kuonyesha kama wanapaswa kuoana ao watafanya tu vile. Dada mwenye kuitwa Elise na bwana yake wanakumbuka hivi: “Tulisikia mubaya wakati wengine walituuliza kuhusu mipango yetu ya ndoa wakati siye wenyewe tulikuwa hatuyaizungumuzia.”

16. Tunapaswa kutenda namna gani kama wenye kuwa mu urafiki wa kimapenzi wanaamua kuvunja urafiki wao?

16 Sasa tutafanya nini ikiwa wenye kuwa mu urafiki wa kimapenzi wanaamua kuvunja urafiki wao? Hatupaswe kujiingiza mu mambo yao ao kuunga mukono upande fulani. (1 Pe. 4:15) Dada mwenye kuitwa Lea anasema hivi: “Nilisikia kama wengine walikuwa nasema-sema juu ya sababu yenye ilifanya miye na ndugu fulani tuvunje urafiki wetu. Ile iliniuma sana.” Kama vile tumeona kuvunja urafiki wa kimapenzi haimaanishe kama wale wenye walikuwa mu ule uhusiano wamekosea. Kwa ukawaida inamaanisha tu kama ule urafiki wa kimapenzi ulitimiza kusudi yake. Ni kusema, ulisaidia wale wenye walikuwa mu ule uhusiano kukamata uamuzi wa muzuri. Hata vile ule uamuzi unaweza kuwaumiza na unaweza kufanya wajisikie kuwa peke yao. Kwa hiyo, tunaweza kutafuta nafasi za kuwategemeza.—Mez. 17:17.

17. Wenye kuwa mu urafiki wa kimapenzi wanapaswa kuendelea kufanya nini?

17 Sawa vile tumeona, urafiki wa kimapenzi uko na magumu yake, lakini pia unaweza kuleta furaha. Jessica anakumbuka hivi: “Kusema kweli, kuko mambo mingi yenye inaomba kufanya mu kipindi ya urafiki wa kimapenzi. Lakini tulifurahi juu wakati na nguvu yenye tulitumia ili kujuana muzuri, haikukuwa ya bure.” Kama muko mu urafiki wa kimapenzi muendelee kujikaza ili kujuana muzuri.

UTAJIBU NAMNA GANI?

  • Urafiki wa kimapenzi uko na kusudi gani?

  • Namna gani wenye kuwa mu urafiki wa kimapenzi wanaweza kufikia kujuana muzuri?

  • Namna gani wengine mu kutaniko wanaweza kutegemeza wale wenye kuwa mu urafiki wa kimapenzi?

WIMBO 49 Tufurahishe Moyo wa Yehova

a Majina fulani imebadilishwa.

b Ili kujua maulizo yenye munaweza kuzungumuzia ona kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku ya 2, uku. 39-40.

c Kugusa-gusa viungo vya uzazi vya mutu mwingine ni mwenendo muchafu wenye unaomba wazee wa kutaniko wafanye halmashauri ya hukumu. Kugusa-gusa maziba ao kutumiana ujumbe muchafu ao mazungumuzo machafu ku telefone, kunaweza pia kufanya mutu aingie mu halmashauri ya hukumu kulingana na hali.

d Ili kujua mambo mingi, soma habari “Maswali Kutoka kwa Wasomaji” mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 15, Mwezi wa 8, 1999.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine