Wimbo wa Sulemani
1 Wimbo wa nyimbo,* ambao ni wa Sulemani:+
2 “Anibusu kwa busu za kinywa chake,
Kwa maana maonyesho yako ya upendo ni ya muzuri zaidi kuliko divai.+
3 Harufu ya mafuta yako ni yenye kupendeza.+
Jina lako ni kama mafuta yenye harufu ya muzuri yenye yanamwangwa.+
Ndiyo sababu vijana wanamuke wanakupenda.
4 Unishike tuende pamoja;* tukimbie.
Mufalme ameniingiza katika vyumba vyake vya ndani!
Tufurahi na kushangilia katika wewe.
Tusifu* maonyesho yako ya upendo kuliko divai.
Ndio maana wao* wanakupenda.
5 Mimi ni mweusi, lakini mwenye kupendeza, Enyi mabinti wa Yerusalemu,
Kama mahema ya Kedari,+ kama vitambaa vya mahema+ ya Sulemani.
6 Musinishangae kwa sababu mimi ni mweusi,
Kwa sababu jua limeniangalia sana.
Wana wa mama yangu walinikasirikia;
Walinifanya kuwa mulinzi wa mashamba ya mizabibu,
Lakini sikulinda shamba langu mwenyewe la mizabibu.
7 Uniambie, wewe mwenye ninapenda* sana,
Mahali unakulishia kundi lako,+
Mahali unawalalisha katikati ya muchana.
Sababu gani nikuwe kama mwanamuke mwenye amejifunika kitambaa cha kufunika kichwa*
Kati ya makundi ya wenzako?”
8 “Kama haujue, Ee mwanamuke mwenye sura na umbo ya muzuri sana kuliko wanamuke wote,
Uende ukifuata njia za kundi
Na ukulishe mbuzi wako wadogo karibu na mahema ya wachungaji.”
9 “Mupenzi wangu, ninakufananisha na farasi-dike* kati ya magari ya Farao.+
10 Mashavu yako yanapendeza kwa mapambo,*
Shingo yako kwa kamba za shanga.
11 Tutakutengenezea mapambo* ya zahabu
Yenye kupambwa kwa feza.”
12 “Wakati mufalme anakaa kwenye meza yake ya muviringo,
13 Mupenzi wangu ni kama mufuko wa manemane wenye harufu ya muzuri;+
Analala katikati ya maziwa yangu.
15 “Angalia! Uko mwenye sura na umbo ya muzuri, mupenzi wangu.
Angalia! Uko mwenye sura na umbo ya muzuri. Macho yako ni kama ya njiwa.”+
16 “Angalia! Uko mwenye sura na umbo ya muzuri,* mupenzi wangu, na unapendeza sana.+
Kitanda chetu kiko kati ya majani.
17 Nguzo za nyumba yetu* ni miti ya mierezi,
Miti ya sehemu ya juu ya nyumba yetu ni miti ya miberoshi.