NAMNA YA KUJIFUNZA
Heshimia Programe Yako ya Kusoma Biblia
Uko na mambo mingi ya kufanya mupaka inakuwa nguvu kwako kuheshimia programe yako ya kusoma Biblia kila siku? (Yos. 1:8) Kama ni vile pima kufanya hivi:
Tia alarme ya kukumbusha. Utie alarme yenye itakuwa nakukumbusha kila siku wakati saa yako ya kusoma Biblia inafika.
Tia Biblia yako fasi ya kuonekana. Kama unasomaka Biblia ya karatasi, uitie fasi kwenye utakuwa naiona saa yote.—Kum. 11:18.
Usikilize usomaji wa Biblia wenye kurekodiwa. Usikilize ule usomaji wakati uko nafanya makazi yako ya kila siku. Dada Tara, mwenye ni mama, painia, na anatumikaka busiku, anasema hivi: “Kusikiliza usomaji wa Biblia wenye kurekodiwa wakati niko nafanya makazi ya mu nyumba, kunanisaidia niheshimie programe yangu ya kusoma Biblia.”
Usikose kusoma. Kama hali fulani inavuruga programe yako, usome hata mistari kidogo mbele ya kulala. Ile kidogo tu yenye unasoma kila siku itakusaidia.—1 Pe. 2:2.