WIMBO 65
Fanya Maendeleo!
Maandishi
1. Fanya maendeleo ya kiroho.
Uhubiri kweli ya Ufalme wa Mungu.
Ongeza ufundi wa kufundisha.
Mutegemee Mungu.
Yesu alihubiri sana;
Na siye pia tutaweza.
Omba Yehova akusaidie
Ukuwe mwaminifu.
2. Uendelee, na usiogope!
Hubiria watu wote habari njema.
Utafute watu nyumba kwa nyumba.
Na umusifu Mungu.
Watu wakikuogopesha,
Endelea tu kutangaza
Kama Ufalme uko natawala.
Hubiri kwa bidii.
3. Endelea kurudilia watu,
Na ujikaze kuwafundisha muzuri.
Omba Mungu akupe roho yake
Ili ikuongoze;
Penda watu unafundisha.
Usikuwe na ubaguzi.
Uwasaidie waendelee
Kumupenda Yehova.
(Ona pia Flp. 1:27; 3:16; Ebr. 10:39.)