Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 11/10 uku. 1-2
  • Mashamba Ni Meupe kwa Ajili ya Kuvunwa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mashamba Ni Meupe kwa Ajili ya Kuvunwa
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Matokeo ya Kazi ya Kuhubiri: ‘Mashamba Yamekwisha Kuwa Meupe, Tayari kwa Mavuno’
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
  • Shiriki Kikamili Katika Mavuno
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • “Lihubiri neno . . . kwa hima”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Je, Unaweza Kufanya Mengi Zaidi Katika Kazi ya Kuhubiri?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2009
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2010
km 11/10 uku. 1-2

Mashamba Ni Meupe kwa Ajili ya Kuvunwa

1. Ni kazi gani ya maana inayofanywa ulimwenguni pote leo?

1 Kisha kumhubiria mwanamuke Msamaria, Yesu aliwaambia wanafunzi wake: “Inueni macho yenu myatazame mashamba, kwamba ni meupe kwa ajili ya kuvunwa.” (Yoh. 4:35, 36) Mavuno ya kiroho yalikuwa yakifanywa, na Yesu alifikiria tayari jinsi kazi hiyo ya mavuno ingefanywa ulimwenguni pote. Akiwa katika cheo chake mbinguni, Yesu anaendelea kuongoza kazi ya mavuno. (Mt. 28:19, 20) Ni mambo gani yanayoonyesha kwamba kazi ya mavuno inaendelea kuongezeka na kufanywa kwa uharaka kadiri inavyokaribia kumalizika?

2. Ni mambo gani yanayoonyesha kwamba kazi ya mavuno inaendelea kuongezeka na kufanywa kwa uharaka ulimwenguni pote?

2 Mavuno ya Ulimwenguni Pote: Katika mwaka wa utumishi wa 2009, kulikuwa ongezeko la 3.2 % la wahubiri ulimwenguni pote. Kulikuwa ongezeko la 14 % katika inchi ambamo kazi yetu inakatazwa. Hesabu ya mafunzo ya Biblia yaliyoripotiwa kila mwezi ilikuwa 7,619,000—hesabu hiyo ni kubwa zaidi kuliko jumla ya wahubiri ulimwenguni na kwa kuilinganisha na hesabu ya mafunzo ya Biblia yaliyoripotiwa mwaka uliopita, ni karibu mafunzo elfu mia tano. Kwa kuwa kazi hiyo inaendelea kuenea kwa uharaka katika maeneo mengi, kuna uhitaji mwingi wa wamishonari waliozoezwa kwenye shule ya Gileadi. Katika inchi nyingi, mavuno ni mengi katika maeneo ya luga za kigeni. Ni wazi kwamba Yehova anaharakisha kazi katika kipindi hiki cha umalizio wa mavuno. (Isa. 60:22) Je, una maoni mazuri kuhusu “mashamba” katika eneo lenu?

3. Wahubiri fulani wanaweza kusema nini kuhusu mavuno katika eneo lao?

3 Mavuno Katika Eneo Lenu: Wahubiri fulani wanaweza kusema, “Eneo langu halizae matunda.” Ni kweli kwamba maeneo fulani hayaonekane kuwa yenye kuzaa matunda kwa kuyalinganisha na maeneo mengine ao hayazae matunda kama zamani. Kwa sababu hiyo, Mashahidi fulani wanaweza kusema kwamba mavuno yamefikia mwisho katika maeneo hayo na kwamba kazi yao sasa ni kuokota tu masalio. Je, ndivyo ilivyo?

4. Ni maoni gani yenye kufaa tunayopaswa kuwa nayo kuhusu kazi yetu ya kuhubiri, na kwa nini?

4 Kipindi cha mavuno ni kipindi chenye kazi nyingi tangu mwanzo mpaka mwisho wa mavuno. Ona jinsi maneno haya ya Yesu yanavyoonyesha uhitaji wa kutenda kwa haraka: “Mavuno ni mengi, lakini wafanyakazi ni wachache. Kwa hiyo, mwombeni Bwana wa mavuno awatume wafanyakazi katika mavuno yake.” (Mt. 9:37, 38) Yehova, Bwana wa mavuno, ndiye anayeamua ni wakati gani na ni mahali gani ambapo mavuno yatafanywa. (Yoh. 6:44; 1 Kor. 3:6-8) Basi, sisi tuna daraka gani? Biblia inajibu: “Asubuhi panda mbegu zako na mpaka jioni usiache mkono wako upumzike.” (Mhu. 11:4-6) Ndiyo, kwa kuwa mavuno yanakaribia mwisho, si wakati wa kuregeza mikono yetu!

5. Kwa nini tuendelee kuhubiri kwa bidii katika eneo linaloonekana kuwa halizae matunda?

5 Tuendelee Kuvuna: Hata ikiwa eneo letu limekwisha kuhubiriwa mara nyingi na linaonekana kuwa halizae tena matunda, tuna sababu nzuri ya kutumika kwa bidii na kutambua uhitaji wa kutenda kwa haraka. (2 Tim. 4:2) Mambo yenye kuogopesha yanayotendeka ulimwenguni yanaweza kuwafanya watu wabadili maoni yao na kufikiria kwa uzito wakati ujao. Vijana wanapokomaa, wanaweza kuona uhitaji wa kutafuta usalama na amani ya akilini. Kwa kuwarudilia watu mara kwa mara, hilo linaweza kuwachochea wengine wakubali ujumbe wetu. Kwa kweli, wale ambao hawakutusikiliza wakati uliopita wanaweza kutusikiliza wakati ujao. Hata wale wanaokataa ujumbe wetu kimakusudi wanahitaji kuonywa.—Eze. 2:4, 5; 3:19.

6. Ikiwa eneo letu si lenye kuzaa matunda, ni nini kitatusaidia tuendelee kuwa na bidii?

6 Ikiwa eneo letu si lenye kuzaa matunda, ni nini kitatusaidia tuendelee kuwa na bidii? Zaidi ya kuhubiri nyumba kwa nyumba, labda tunaweza kutumia njia zingine za kuhubiri, kama vile kuhubiri katika maeneo ya biashara ao kwa njia ya telefone. Ao tunaweza kubadili namna yetu ya kutolea watu ushahidi na kujaribu namna mpya. Tunaweza kubadili programu yetu na kuhubiri wakati wa mangaribi ao wakati mwingine ambapo watu wanaweza kupatikana nyumbani. Labda tunaweza kujifunza luga nyingine ili kuhubiria watu wengi zaidi. Tunaweza kupanua utumishi wetu kwa kuwa mapainia wa kawaida. Ao tunaweza kuhamia mahali ambapo kuna wavunaji wachache. Ikiwa tuna maoni yenye kufaa kuhusu kazi ya mavuno, tutajikaza kushiriki zaidi kwa kadiri tunavyoweza katika kazi hiyo ya maana.

7. Tutaendelea kufanya kazi ya mavuno mpaka wakati gani?

7 Wavunaji hawana wakati mwingi ili kukusanya mavuno, kwa hiyo hawapumzike ao kupunguza bidii mpaka kazi inapomalizika. Vivyo hivyo, tunapaswa kutambua uhitaji wa kutenda kwa haraka kuhusu mavuno ya kiroho. Tutaendelea kufanya kazi hiyo ya mavuno mpaka wakati gani? Wakati wote wa “umalizio wa mfumo wa mambo” na mpaka “mwisho.” (Mt. 24:14; 28:20) Kama Mhudumu mkuu wa Yehova alivyofanya, sisi pia tunataka kumaliza kazi ambayo tumepewa. (Yoh. 4:34; 17:4) Acheni basi tuendelee kufanya kazi yetu kwa bidii na kwa furaha, na tuwe na maoni mazuri kuhusu kazi hiyo mpaka mwisho. (Mt. 24:13) Kazi ya mavuno haijafikia mwisho!

[Wazo la fungu kwenye ukurasa wa 2]

Kipindi cha mavuno ni kipindi chenye kazi nyingi tangu mwanzo mpaka mwisho wa mavuno

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine