Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 11/12 uku. 2
  • Usijizuie Kuanzisha Funzo kwa Sababu Unawaza Hauna Uwezo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Usijizuie Kuanzisha Funzo kwa Sababu Unawaza Hauna Uwezo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Unaweza Kusaidia mu Kazi ya Kufanya Wanafunzi?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Unaweza Kuwa Mwalimu!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Kusudia Kuongoza Funzo la Biblia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Usisite Kuongoza Funzo la Biblia!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2012
km 11/12 uku. 2

Usijizuie Kuanzisha Funzo kwa Sababu Unawaza Hauna Uwezo

1. Sababu gani watu fulani wanajizuia kuanzisha funzo la Biblia?

1 Je, unajizuia kuanzisha funzo la Biblia kwa sababu unawaza hauna uwezo wa kuliongoza vizuri? Wakati fulani, watumishi waaminifu wa zamani, kama vile Musa na Yeremia, walijisikia kama hawana uwezo wa kutimiza migawo yao. (Kut. 3:10, 11; 4:10; Yer. 1:4-6) Kwa hiyo, ni kawaida kujisikia hivyo. Namna gani tunaweza kushindana na hali hiyo?

2. Sababu gani tusitosheke tu na mahubiri ya nyumba kwa nyumba na kuwaachia wengine kazi ya kuongoza mafunzo ya Biblia?

2 Tunapaswa kukumbuka kama Yehova hatuombe hata kidogo tufanye mambo yanayopita uwezo wetu. (Zab. 103:14) Kwa hiyo, kazi ya ‘kufanya wanafunzi’ na ‘kuwafundisha’ aliyotuomba tufanye haipite uwezo wetu. (Mt. 28:19, 20) Hilo si pendeleo ambalo Yehova amewatolea tu watu wenye uzoefu ao wenye ufundi mwingi kati yetu. (1 Kor. 1:26, 27) Ndiyo sababu tusitosheke tu na mahubiri ya nyumba kwa nyumba na kuwaachia wengine kazi ya kuongoza mafunzo ya Biblia.

3. Namna gani Yehova ametupatia uwezo wa kuongoza mafunzo ya Biblia?

3 Yehova Anatupatia Uwezo: Ni Yehova ndiye anayetupatia uwezo wa kufanya wanafunzi. (2 Kor. 3:5) Kupitia tengenezo lake, ametufundisha kweli za Biblia ambazo hata watu ambao wamesoma mingi katika ulimwengu huu hawajue. (1 Kor. 2:7, 8) Katika neno lake amelinda maandishi kuhusu njia za kufundisha za Yesu, Mwalimu Mukuu, ili tumuige, na anaendelea kutuzoeza kupitia kutaniko. Tena, Yehova ametutolea vyombo vya lazima ili vitusaidie kuwafundisha watu Biblia. Ametutolea vyombo, kama vile kitabu Biblia Inafundisha, vinavyofundisha kweli kwa njia nzuri na rahisi kuelewa. Inaweza kuwa rahisi kuongoza funzo la Biblia kuliko jinsi tunavyowazia.

4. Sababu gani tunaweza kuwa hakika kwamba Yehova atatusaidia?

4 Kwa musaada wa Yehova, Musa na Yeremia walitimiza migawo yao. (Kut. 4:11, 12; Yer. 1:7, 8) Sisi pia tunaweza kumuomba Yehova atusaidie. Tunapoongoza funzo la Biblia, tunamufundisha mutu kweli juu ya Yehova, na hilo linamufurahisha Mungu. (1 Yoh. 3:22) Ndiyo sababu, uwe na muradi wa kuongoza mafunzo ya Biblia; hiyo ni sehemu ya kazi ya kuhubiri yenye kufurahisha zaidi na yenye baraka nyingi.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine